Mwenyezi Mungu akujalie akili ya kuona mbali. Kwa aina ya maisha unayotaka kuishi, utakuwa ni mwanamke wa hovyo kupindukia.
Maana sifa mojawapo ya mke mwema, ni ucha Mungu wake. Sasa sijui mwenzetu utakuwa binti maisha yako yote!
Vipi na wewe siku ukiwa mama? Utawahamasisha watoto wako kusali, au mtashinda wote nyumbani mkichati na ma boyfrend wenu?
kuna idea mbili tofauti hapa kwanza bado upo kwenu kwahiyo kibongo bongo lazima ufuate kanuni za hapo kwenu pili mara nyingi wazazi wengi wakiafrica huwa wanategemea hata kama mtoto ni mtu mzima ufuate yeye anachofikiria ni bora kwake hata kama wewe unaona hakina logic mfano kuna kipindi nilikua nimemaliza chuo na sikua na kazi ya kueleweka ambayo mzazi kwenye fikira zake aliona inafaa kulingana na elimu aiyoniseomesha lakini akawa haelewi kwamba ajira ni ngumu kwahiyo nikawa napiga vibarua hapa na pale siku moja kanifuata huko nilikokua nimepanga kaniambia twende kwa mganga akanifanyie zindiko eti nimerogwa niikataa na nikamsihi asiniambie kitu kama hicho tena. Kiukweli aliongea na kulalamika sana na kusema watoto hatusikiizi wazazi. Lakini point sio heshima ni kuangalia kama mtu mzima kipi unaona kinakufaa na kipi hakikufai.Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.
Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.
Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.
Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.
Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"
Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"
Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"
Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"
Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"
Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.
Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.
Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"
Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.
Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.
Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana
Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"
Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.
Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?
Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
You're such a moron
Kabla ya huku mlihudhuria wapi?Kwa mwamposa
Mleta mada hujitambui, yawezekena unatumia ngada au unasumbuliwa na ujuaji wa kijinga au usomi uchwara. Wewe mtu mzima gani unaishi kwenu, alafu unaambiwa na mzazi wako ufuate taratibu za mji wake unashupaza shingo. Au unataka wakati wanapoenda kanisani ubaki unamtafuna housegirl. Hapo Mzee akitangulia mbele za haki na wewe utatanguliza tumbo lako kudai urithi wakati sasa hivi unasema wewe ni mtu mzima hupangiwi Wala kulazimishwa. Kuwa na adabu kwa baba yako, na wewe utafanyiwa upuuzi km huu na watoto wako. Wazazi wako ni Mungu wa pili wanakuongoza kwa mema. Acha ujuaji na usera wa kijinga. Umeniudhi sana km Mzazi.
Mara useme wewe kwake ni mtoto, hapa tena unasema we ni mtu mzima uliezidi 18 yrs.Sawa sasa kwanini haniachi?
Mtu mzima aliyezidi 18 ni wa kulazimisha dini kweli?
Huwezi weka philosophical au theological zako kwenye nyumba za watu. Ungekuwa mtu mzima na unaelimu kama usemayo usingeishi kwenu
Utu uzima sio umri pekee Bali ni majukumu pia.
Hata angekuwa anaabudu mashetani anamamlaka ya kukuambia uabudu hayo mashetani na ukafanya
Dictionary ya jamii,ukiwa mtu mzima unaenda kujitegemea
Mkuu nakushauri uhame tu hapo home ukajitegemee ili uishi upendavyo. Kuna wenzio hawana hata mama wa kuwakumbusha kwenda kanisani,wewe unae unamfanyia dharau na bado ati unaenda kanisani na kuchat ibada nzima mkuu laana nyingine ni za kujitakia. Punguza dharau na ujuaji.
Jishushe,mpe thamani sahihi mzazi wako.
Sipo 50 by 50....soma vizuri post zangu utanielewa.Kama huamini kuwa hayupo ina maana kuna mambo kadhaa yanakufanya usiwe 100% na imani kwamba Mungu hayupo, hebu nielezee mambo yapi yanakufanya uwe na imani kwamba yawezekana Mungu yupo? na mambo yapi yanakufanya uamini yawezekana Mungu hayupo? Ina maana upo 50 by 50,
Kuna tofauti kati ya kuconvince na kulazimishaSi sahihi hata kidogo... lakini je kuna ubaya wowote kujaribu kumconvince mtu aone uwepo wa Mungu??
Sawa endelea kuiamini zaburi ambayo hata hujui nani kaiandika.Bible inasema, "Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu" Zaburi 53 :1a
Kuna sehemu nimesema ukristo haufai?? Ukristo unafaa.Ungekuwa unaishi kwako usingeandika haya pengine ujuaji wa dini nyingine imekuingia unatafuta muumini mwenzako hapa aamini unacho amini lengo lako sio kuandika kuwa hutaki kwenda kanisani lengo ni kuwaambia watu kuwa Ukristo haufai na wanapotea ila ujumbe wako hujaufika vizuri. Usizunguke mbuyu
Kwahyo kabla ya wazungu waafrka tulisali rozali ya bikra maria na kumsifu yesu kristo?Suala la dini (Imani) ukisema ni matokeo ya kuwa Brainwashed na wazungu inaakisi namna ambavyo hujui kudadisi mambo.
Kifupi, miaka maelfu wanadamu wamekuwa na ugomvi na concept ya kuabudu. Msingi wa ugomvi ni:-
1. Kuabudu Mungu mmoja ni sahihi ama sio sahihi? Huyu Mungu mmoja ni nani?
2. Kuabudu miungu wengi ni sahihi ama sio sahihi? Hawa miungu wengi ni akina nani?
Kwamba kuna asiyeabudu kabisa? Huyu hayupo. Sana sana utakuta amezama kwenye kundi la kuabudu miungu wengi.
Kundi utakalochagua ni kama bundle la simu hivi (yaani unapata SMS kadhaa, muda wa maongezi dakika kadhaa, GB kadhaa nk). Wewe Tu!
Kuhusu wewe kukosa Imani na kumbishia mzazi wako kuhusu kwenda ibadani pamoja, Mama yako yupo sahihi 100%. Ikiwa yeye akiondoka kwao ili aishi atakavyo, nawe fuata hizo nyayo uishi upendavyo.
Ukiwa kwako hiyo kesi ya twende kanisani itakuwa imekufa kishujaa.
SawaNeno langu kwako ni hili,wa swahili husema "' Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu"'
kwa upande wangu naona mama yako anakuwazia mema anatamani akufunze njia ipasayo,ila ulimwengu unakutamani ukufundishe ndo maana unaona mtu aliyekubeba miezi tisa na kukutunza hadi leo una akili ya kumkosoa,unamuona anakupoteza.
Nimalizie kwa kusema mkataa pema pabaya panamngoja.
Ninachojua ni kwamba as long as bado unaishi kwake ni vyema ukamtii.
Hayo yote yanafanywa kwa watotoNi sawa,kwa sababu ana wajibu wa kulea,mbona huulizi uhalali wa mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda shule ,kunywa dawa akiumwa,kula anapokataa kula?
Usisahau naye alizaliwa.Kama alinizaa hata nizeekeje bado ni mtoto wake.
Im sorry.Kwani wewe ni jinsia gani?
maana kuna imani imeingia isiyohusisha kwenda kanisani wala msikitini
nayo si nyingine bali ni ushoga na usagaji,sasa ni heri umwambie mzazi wako kwamba umejiunga huko
akuondoe hapo nyumbani usiendelee kunajisi nyumba.
Ungekuwa kwangu ningekuwa nimeishakusend hayupo muda mrefu,sema mama yako ni mvumilivu sana.
90+Kwan we unaona ngapi