Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Wewe umepotoka kwa kutoamini katika MUNGU WA KWELI.

Mama yako naye amepotoka kwa kukulazimisha wewe kuabudu udanganyifu aliorithi kutoka kwa wazazi wake. Ni udanganyifu sababu kila kanisa linalo abudu siku ya Jumapili siyo kanisa la KWELI la MUNGU.

Hata kama mama yako angekuwa anaabudu katika kanisa la KWELI la MUNGU, bado hatakiwi kukulazimisha kuifwata njia yake.
MUNGU wa KWELI halazimishi watu kumwabudu, bali wamwabuduo humwabudu kwa hiari yao wenyewe, tena katika roho na KWELI.

Hivyo, utaona ni jinsi gani nyote wawili, wewe na mama yako mmepotoka.
Hahah...yani kila mtu anavutia kwake. Akija muislam anavutia kwake, msabato nawewe unavutia kwako 😂 hizi dini ni vichekesho
 
Mara nyingi hatufanyi vitu kwaajili yetu binafsi bali tunafanya vitu kwaajili ya watu tunaowapenda...ni suala la muda tu, tafakari kwa dhati
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]nimecheka sana aisee
 
Mkuu utamaduni ni somo paaana sana lenye aspects nyingi sana kama language,arts, rituals, norms, beleifs, customs, taboos, ethics nk. Nk.
Hapo religion ni aspect mojawapo tu ya utamaduni.
Tena ni aspect ndogo sana maana inafall ndani ya aspect ya beleifs, na imani zipo nyingi za kidini na zisizo za kidini.

Mfano hata hapa bongo kuna viimani vingi mfano jicho likicheza kuna mgeni au jambo fulani litatokea, mvua na jua kuna simba anazaa, ukioga baharini unaondoa gundu, watu wafupi wote ni wabishi nk. Nk.
ila sio imani za kidini.

So dini ni kakipengele kadogo sana kwenye swala la utamaduni.
Ambako ndani yake kuna taboos zake.

Lakini Taboos nje ya dini zipo nyingi kuliko hata hizo za ndani ya dini.
Mfano ni taboo kwa wamasai kula samaki, jamii nyingi ni taboo kula mbwa, ni taboo kubusu wazazi mdomoni, ni taboo kukiss hadharani nk. Nk.
Vyote hivi havihusiani na dini.

Kukubaliana na mtu sio taboo...ila pale mtakapo kubaliana kukataa kitu fulani na ikawa ndani ya utamaduni wenu wa maisha ya kawaida kuwa hairuhusiwi kufanya jambo fulani kwenye jamii basi hiyo by definition ni taboo.

Hata wewe nyumbani kwako ukisema hairuhusiwi mtu wa hapo kuvaa nguo nyeusi, itakuwa taboo ya nyumbani kwako.

Umeeleza vizuri Sana.

Ikiwa unamarifa haya yote ni kwanini unashindwa kuelewa Sababu za Mama kukulazimisha uende Kanisani tena Kanisa analosali yeye ilihali unaishi kwake?

Kwa sasa ninaamini umejua kuwa ni halali Kwa Mama yako kuingilia Uhuru wako uwapo katika utawala na himaya yake. Si ndio?
 
Umeeleza vizuri Sana.

Ikiwa unamarifa haya yote ni kwanini unashindwa kuelewa Sababu za Mama kukulazimisha uende Kanisani tena Kanisa analosali yeye ilihali unaishi kwake?

Kwa sasa ninaamini umejua kuwa ni halali Kwa Mama yako kuingilia Uhuru wako uwapo katika utawala na himaya yake. Si ndio?
Sio halali...Lakini kwakuwa yeye anaamini ni halali namimi sitaki kupishana naye nitamfuata kumfurahisha tu.
 
Mungu ana nafasi yake.

Utamtafuta mwenyewe kwa machozi.

Hapo upo kwenye comfort zone.

Ila muavuli wa mama yako ukiondolewa na ukakutana na machungu ya dunia.

Utautafuta huu uzi uufute.

Dunia bila ulinzi wa kiroho ni chungu mno.

Heshimu nafasi ya Mungu.
 
Mungu ana nafasi yake.

Utamtafuta mwenyewe kwa machozi.

Hapo upo kwenye comfort zone.

Ila muavuli wa mama yako ukiondolewa na ukakutana na machungu ya dunia.

Utautafuta huu uzi uufute.

Dunia bila ulinzi wa kiroho ni chungu mno.

Heshimu nafasi ya Mungu.
Wewe wasema
 
Mungu hajawahi shindwa kwa mwanadamu kuna sehemu atakubana, maisha yatakubana, kila mlango wa mafanikio utakuwa umebana hapo sasa utakuwa huna kimbilio zaidi ya kwenda church mwenyewe bila kulazimishwa niliwahi kuwa kama wewe way back ila kuna mahali nilibanwa sikuwa na namna na sasa nafurahia uamuzi wangu wa kumfuata Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu..
And you were lucky,ni heri ulifikia kupata neema ya kumgeukia Yesu,maana kama ungepotea kabla ya kuufikia wokovu na kumjua yeye saa hizi ungekuwa unateketea...
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Bado unaishi kwa mama?...
 
Sio halali...Lakini kwakuwa yeye anaamini ni halali namimi sitaki kupishana naye nitamfuata kumfurahisha tu.

Wewe unaamini sio halali, Naye anaamini ni halali.
Hivyo ambaye yupo kwenye himaya ya mwenzake ndio afuate sheria za mwenzake.

Na hapo Wewe ndio sio halali Kwa sababu upo kwenye himaya ya Mzazi wako.

Halali na haramu inaletwa na SHERIA.
Sijui mama unalijua Jambo hilo
 
Ukikaa miaka minne kitaa bila ajira, utajua Mungu yupo au hayupo, kusali ni muhimu au siyo muhimu.
 
Sipo 50 by 50....soma vizuri post zangu utanielewa.
Mungu huyu wa hizi dini mbili hayupo kwa asilimia 100%
Mungu halisi anaweza kuwepo na sina uhakika kama yupo, ila ushahidi uliopo/ambao haupo nampa asilimia 0.000000001% ya kuwepo.
Hata hio 0.000000001% tayari kuna imani ndogo juu ya uwepo wake, Yesu alisema imani ndogo mfano wa punje ya haradali unaweza fanya mambo makubwa mno, sasa hio sio completely zero, imani yako ndogo hio imepelekewa na sababu zipi?
 
Zaidi ya 18 ni mtu nzima na katiba inatambua. Unachagua imani yoyote unayotaka. Tena nakupongeza kwa kugundua Ukristu ni uzungu na Uislamu ni Uarabu. Tulipokea hizi imani bila kuhoji, sasa ni wakati wako wa kuhoji. Waambie una imani katika mababu zako waliokufanya uwe duniani, hao ndio kiungo chako na Mungu wa kweli. Ila usibishane nao maana hawatakuelewa.
 
Jehanam ipo kwa ajili ya wanao kaidi, na paradiso ni kwa ajili ya wanao tii UKO HURU KUCHAGUA mahali upapendapo,
 
Mzazi yupo sawa sababu we ni mtoto wake hataki uharibikiwe na kingine bado unaishi chini ya wazazi wako unatakiwa ufate kile wanachokwambia

Kijana mdogo ushaona dini uliyozaliwa ndani yake uiamini

Acha kujipa usahihi na mzazi wako mzazi huwa hakosei hata siku moja
Kwa kuongezea mimi nadhani inategemea pia na aina ya kanisa, kiukweli kuna makanisa yameibuka yamechangia sana kuchanganya na kuharibu imani za waumini hasa vijana. Imagine unaenda kanisani kama kwa yule sijui Nabii aliyechorwa tattoo na mke wa mtu na kupelekea kuvunja ndoa ya muumini wake hapo unatajia nini? Kumbuka vijana wa sasa ni wa dadisi sanaa... Kuna kijana Wa rafiki yangu kamaliza form 4 mwaka juzi amegoma kuendelea na shule (form 5) au chuo na amehamia kwa mchungaji wa haya makanisa ya mwendokasi eti naye anataka kuwa mchungaji..
 
Kwa mwamposa
Nilitegemea aina hii ya makanisa. Nina swali je umewahi kufikiria kwenda yale makanisa kama ROMA au Lutheran? I mean yale makanisa ya zamani ambayo tulikuwa nayo kabla ya haya ya mwendokasi??
 
Back
Top Bottom