Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Mkuu She nafikiri uko sahihi kuwaambia ukweli kuwa huamini tena. Ila mzazi anapoudhika kwa swala la kiimani huwa ni hatari.

Kwa sisi Waislam huwa tunaambiwa tuwatii wazazi wetu kwenye kila lililo jema, ila watakapotuamrisha maovu basi kwa adabu tuyakatae.

Uko sahihi kuwa suala la imani ni kati yako na Muumba wala mama halimhusu kwakuwa ushakuwa mtu mzima sasa.

Lakini kwakuwa uko chini ya paa lake sioni kama una chaguo, Ushauri wangu ni kuwa endelea kwenda Kanisani wakati huohuo jaribu kutumia njia nzuri kumuelewesha mama ni nini unafikiri kuhusu Dini na Mungu, tena mueleze kwa upole na adabu zote nina amini utaipata njia sahihi.

‘By the way i have been there’
 
Mrembo She Quoted you nasikitika sana kuona unalazimishwa kusali ikiwa hupendi kufanya hivyo.

Mrembo hii ni Africa ukweli ni kuwa una haki ya kuamua usali au usisali ila shida ni hizi akili za wazazi wetu mapopoma wanaohisi kuwa hata ukishakuwa mtu mzima lazima akuendeshe ilimradi yeye inambidi kuwa mshauri tu .

Sasa hiko hivi hapo kwenu ili kuitunza amani kubali tu kwenda huko kanisani ila nenda kujipumzisha poteza muda kama wao watakavyo hii ni kutokana na kuwa huna kwako bado.

Ila ukipata kwako ishi utakavyo ila kuhusu kukulazimisha kusali sikubaliani na mama yako ila ndiyo hivyo sasa upo kwake tii ili maisha yaende.

Ila nje ya mada vipi utaki kuolewa ?[emoji3] Maana yuko mwamba hapa yeye na mambo ya kanisani ni mbingu na ardhi .

Ikiwa uko ready yuko pale anakusubiri pm ukuambie jambo[emoji39]

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unaweza kuvuka salama wewe ila wanao wakawa na changamoto[emoji847].
Bora uende sometimes kutimiza hata connection za normalities. Siku ukifa halafu watu wakaamua kufunika tu wakasepa familia yako itajiskia vibaya sana. Au ukifiwa na mwanao watu wanashindwa process, hadi inabidi ndugu zako wa kanisani au msikitini watu wawadhamini tu ili kudumisha mahusiano. Dini zinasaidia kudumisha mahusiano kati ya wanadamu mkuu apart from spiritual matter.
Afadhali wewe umekuwa muwazi .
Huo ndio umuhimu mkubwa wa dini kwa Africa hasa usipokuwa tajiri. Mahusiano ya kijamii.Ndoa, kusaidiwa katika shida kubwa na kuzikana.
Ni aina fulani ya uoga wa maisha pia.
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
Mungu hajawahi shindwa kwa mwanadamu kuna sehemu atakubana, maisha yatakubana, kila mlango wa mafanikio utakuwa umebana hapo sasa utakuwa huna kimbilio zaidi ya kwenda church mwenyewe bila kulazimishwa niliwahi kuwa kama wewe way back ila kuna mahali nilibanwa sikuwa na namna na sasa nafurahia uamuzi wangu wa kumfuata Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu..
 
Mimi ni islamic mrembo ila maamuzi ya niswali au nisiswali najaribu kuyaweka kuwa private sio niingiliwe na binadamu yeyote.

Japo kipindi hiko nimewahi kulazimishwa fulani kwa jina la" Da'hwa " ila Mnyazi ni mwema vita nilivishinda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmh hongera sana.
Ni wanadini wachache wenye mawazo huru kama wewe.

So far kwenye huu uzi, watu wasio na dini ndio nimeona wako open minded (pamoja na kuwa wengi wao wamesema sipo sahihi, ila wametoa sababu zinazo make sense) ila wanadini wao wapo kulazimisha wanachoamini wao tu.
Ukizingatia sijaomba ushauri kuhusu kuamini Mungu au La, ilikuwa mjadala kuhusu swala la uhuru wa kiimani.

Kama imani inalazimishwa basi haina maana tena, maana imani ni kuamini, na huwezi kulazimisha mtu aamini unachotaka.

Wewe kwa mindset yako utafika mbinguni (kama ipo) kuliko hao mashehe wanaoshinda msikitini.
 
Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.

Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?

Wajibu wa mzazi Ni kumlea, kumuongoza Na kumsimamia Mtoto wake.

Wajibu wa Mtoto Ni kumtii mzazi Na kufuata maelekezo ya mzazi ili akabidhiwe kwenye "dunia" iliyo Salama kwake.

Kumbuka asiyefunzwa Na mamaye hufunzwa Na ulimwengu, Na kamwe hapaswi kuja kumlalamikia mzazi wake yakimkuta: kumbuka 'asiyesikia LA MKUU huvunjika guu'.

Mama yako ana nia mzuri sana Na we we, Na Kwa vile umemaliza chuo karibuni, yawezekana umesoma zaidi Yake.

Anachokuzidi Ni kwamba yeye Ni Mzazi, ambaye amepewa kibali Na Mungu kukulea Na kukusimamia akikuongoza katika mema anayoyajua.

Tafakari haya kabla ya kufikiri umkubalie au umkatalie "maelekezo" Yake, ukikumbuka ombi LA Mkubwa Ni amri..
 
Mkuu She nafikiri uko sahihi kuwaambia ukweli kuwa huamini tena. Ila mzazi anapoudhika kwa swala la kiimani huwa ni hatari.

Kwa sisi Waislam huwa tunaambiwa tuwatii wazazi wetu kwenye kila lililo jema, ila watakapotuamrisha maovu basi kwa adabu tuyakatae.

Uko sahihi kuwa suala la imani ni kati yako na Muumba wala mama halimhusu kwakuwa ushakuwa mtu mzima sasa.

Lakini kwakuwa uko chini ya paa lake sioni kama una chaguo, Ushauri wangu ni kuwa endelea kwenda Kanisani wakati huohuo jaribu kutumia njia nzuri kumuelewesha mama ni nini unafikiri kuhusu Dini na Mungu, tena mueleze kwa upole na adabu zote nina amini utaipata njia sahihi.

‘By the way i have been there’

Okay nmekupata, ila kwa umri wa wazazi sitajaribu kuwaelewesha..maana ni umri unaoaminika wa kumrudia muumba.
Kwahyo haitakuwa na maana wataona kama najaribu kuwapotosha niwanyime raha za mbinguni.

How did you solve your case?
 
Mungu hajawahi shindwa kwa mwanadamu kuna sehemu atakubana, maisha yatakubana, kila mlango wa mafanikio utakuwa umebana hapo sasa utakuwa huna kimbilio zaidi ya kwenda church mwenyewe bila kulazimishwa niliwahi kuwa kama wewe way back ila kuna mahali nilibanwa sikuwa na namna na sasa nafurahia uamuzi wangu wa kumfuata Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu..
Usidhani maisha yako yanareflect maisha ya kila mtu...Kuna nchi hata haziamini Mungu na wananchi wanaendelea kufanikiwa na kututawala eg. China
 
Kwa nini kusema kuwa ana degree imekuuma sana??! Inferiority complex inakusumbua.
Tafuta degree na wewe kama huna ili mtu akisema ana degree usiumie.
Kuweka Protocol ni ubaguzi?[emoji23][emoji23][emoji23]
Ati Una degree[emoji3]
Mbona Mama Yako akikulisha hapo NYUMBANI hauiti ubaguzi?
Wewe upo chini ya wazazi, mzazi kapewa mamlaka ya kukulea, kukulisha, kukupa malazi n.k.
Mzazi akukupa chakula husema anaingilia Uhuru wako.
Akikuvisha hausemi anaingilia Uhuru wako.
Alipokuwa anakusomesha haukusema anaingilia Uhuru wako.

Anakuambia uende Kanisani Ari ndio anaingilia uhuru wako? Yaani kuna watu wapumbavu kweli.

Uhuru unaoutaka hauwezi kuipata ukiwa chini ya wazazi. Protocol haipo hivyo.

Na sio tuu wazazi hata siku ukiolewa, unakuwa chini ya Mumeo. Yeye ndio ataamua wapi uende kuabudu. Suala la kuamini utajua mwenyewe akilini na moyoni mwako.

Suleiman aliwahi kusema; Mpumbavu hata umtwange kwenye kinu upumbavu wake hautamtoka.
 
Hata ungekuwa umelelewa kwenye dini 20, una uwezo finyu sana wa kufikiri nje ya chungu cha dini, wewe ni mlevi wa dini.
Akili mbili ni shida.
Mimi nimelelewa kwenye dini zote mbili, uislam na Ukristo. Nazifahamu dini hizo.

Ninaishi maisha nje ya Dini nikiwa Kwa watu wasioamini katika Dini/nikiwa kwenye mamlaka Yao.
Ninaishi maisha ya kidini Kwa waaminio mambo ya Dini/nikiwa kwenye mamlaka Yao.

Ila pia ninaishi maisha yangu ninayoyataka nikiwa katika himaya yangu.

Ninyi msiotumia akili ndio mnaishi kwenye mamlaka za watu na kutaka kuishi mtakavyo ndio mnaonyesha jinsi mlivyowajinga
 
Kwa nini kusema kuwa ana degree imekuuma sana??! Inferiority complex inakusumbua.
Tafuta degree na wewe kama huna ili mtu akisema ana degree usiumie.
Yaan namshangaa sanaaa huyu Taikon, nilikua namuona akili kubwa, ila ktk huu uzi ndo kajivua nguo zaid
 
Mifano yako ni pointless
Inashangaza mtu unafikisha miaka 20 bado hujui mambo madogo Kama hayo?

Hata Rais Samia akifika NYUMBANI kwako lazima afuate sheria zako bila kujali Urais wake.

Ndio maana Hata Magufuli alipokuwa akiingia msikitini alikuwa anavua viatu licha ya kuwa yeye ni Mkristo na haamini katika kivua viatu ukiingia Nyumba za Ibada.

Elewa kuwa kila Jambo linamipaka yake.
Hata Wewe ukiwa na familia yako ukaweka sheria, mama au Baba yako akija kwako atafuata sheria za Nyumba yako.
Bila kujali anaamini au haamini.

Hataki aondoke.
Sijui wapi unakwama
 
Back
Top Bottom