Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mzazi kumlazimisha mtoto wake kwenda kanisani ni sawa?

Mambo vipi wakuu,
Nimemaliza chuo mwaka jana, I am 24. nipo nakaa hapa nyumbani ila kuna tatizo la kiimani.

Mom analazimisha kila jumapili niende kanisani.
Kiuhalisia mimi saivi sina imani kabisa na kanisa au maswala ya Mungu naona kama ni utapeli na mambo ambayo binadamu walitengeneza tu hayana ukweli wowote.

Sasa nikaanza kamgomo kangu baridi ka kutoenda, kila ikifika j'pili nakuwa na kisingizio tofauti, mara naumwa, sijiskiii etc.

Sasa imeenda hivyo mwishowe mama akaamua anifungukie kuwa as long as bado naishi chini ya paa lake, kwenda kanisani ni lazima. Akajaribu kunidadisi kwanini sipendi kwenda, Mimi nkaona kabisa nikimwambia siamini tena maswala ya dini atapata presha bure.

Nkawa namuambia kuwa siamini katika kusali kanisani maana Mungu yupo moyoni na naweza kumuomba siku yoyote iwe juma3 au juma4, na nkamuambia kama biblia nnayo kwenye simu naisoma kila siku na nasali kila siku.
ila akawa haelewi anasema biblia inasema "wakutanapo wawili kuna Mungu...bla bla bla"

Sasa mimi nkamuambia "Nikuambie tu sasa ukweli, Mimi naona ibada ni kati yangu na Mungu wangu wala sio kati yangu mimi na wewe na mungu. Kwahyo kama unanilazimisha kwenda kanisani, ntaenda ili nikufurahihishe tu, ntakuwepo kimwili kanisani ila kiroho na kiakili sitakuwepo kanisani"
Akaanza kusema niende kwa ajili yangu sio kwa ajili yake
Nkamuambia "sasa mimi sijawiwa kwenda, ila wewe ndo umenlazimisha nifanyeje?"

Akakaa kimya. ila siku hiyo alikasirika siku nzima na ilikuwa jumapili akaanza mpaka kusema "Mimi ningekuwa na nyumba nyingine ningeenda kuishi nikawaacha maana haina maana kukaa na watu hamnitii"

Mimi nikamuambia "Lakini mama, Swala la kanisani sio la utii kwako, ni la kwangu na Mungu na wala hutakiwi kunilazimisha"

Akasema "Sisi ndivyo tulivyolelewa, na watoto wangu wote nimewakuza hivyo mpaka leo wanasali, wewe ndio unataka kupinga siwezi kukubali. Subiri ujitegemee ndiyo ukaidi, ila as long as bado upo chini yangu kanisani ni lazima"

Nikaendelea kutokwenda kibishi kibishi tu.

Lakini housegirl ndio siku moja akaja akayatibua tena..Tumemaliza kula usiku mara akaanza kusema kabla hatujalala ana jambo la kuniambia pale sebuleni.

Housegirl: "She, leo nikuambie tu mbele ya mama hapa, hili swala linaniumiza mno. mkubwa anakuambia kitu halafu unakaidi. Sio vizuri na leo imenifika shingoni lazima nikuambie. Sio vizuri unapomkaidi mama yako na kupinga kwenda kanisani au kwenda kwa kuchelewa sana.Huyu ni mkubwa na mkubwa akisema kitu wewe mtoto unatakiwa ufuate. Mungu anakupima, huenda ukimtii na ukaenda kanisani utafunguliwa hata mambo yako mengi kama kupata ajira"

Ukawa mjadala mrefu sana pale wakisapotiana na mama.

Sasa mimi nikaona hii ishakuwa kesi, ila nikaona usiwe ubishi usio na faida pale sebuleni, maana hata niseme kwa lugha ipi, hata niongee kigiriki na kiyunani. Hawa watu hawawezi kunielewa. Ni kwamba wako brainwashed na dini ya mzungu mpaka stage kwamba mimi ndio wataniona punguani.

Sasa nkamuangalia mama nkaona kama anaumia moyo sana kwa ajili yangu na kisa ni kwenda kanisani tu.
Isiwe kesi sana

Ikabidi sasa nitumie hekima tu niwajibu "Nimewasikia, Mungu hutumia watu wake kufikisha ujumbe, na leo amewatumia nyie kufikisha ujumbe kwangu. Kwahyo nimesikia na kwa utiifu kuanzia sasa nitaanza kwenda kanisani Amina"

Lakini kanisani naenda na simu, nakaa nyuma nachati ibaada nzima hadi muda wa kuondoka hata ukiniuliza muhubiri alikuwa jinsia gani au alikuwa amevaa nguo gani au amehubiri nini wala sijui.
Yani sipendi kabisa naona kama napoteza tu muda wangu huko.
Ikifika jumapili nakosa raha kabisa kwasababu hiyo.

Sasa wakuu, naombeni ushauri wenu, Nipo sahihi? Au nisimamie msimamo wa kutoenda? Au niendelee kwenda kwa kuwafurahisha tu? Au niwaambie nimeasi kabisa?

Nani yuko sahihi hapa, kati yangu na mama?
😂,Sijui tukusaidie vipi🙆‍♀️,inakaa kama mamako ni mkristo mwenye itikadi kali,, hao huwa hawaelewi kitu, hata umweleweshe vipi,, anza kwenda kanisani au uondoke ukapange chumba kwingine
 
Hilo ni jambo la kimila na kiutamaduni ni taboo.
Sijajua kuhusu Tz maana mimi sio mwanasheria, ila nchi nyingi zinakataza kisheria incest.

Logic behind ni kuwa ukiruhusu incest unapunguza variations kwenye genetic pool, kwahyo kukitokea trait mbaya inakuwa dominant kwenye familia/ukoo.
Mfano ikitokea Asthma au ugonjwa wa akili unakuwa dominant kwasababu mnaoana ninyi kwa ninyi.

Kwahyo kiutamaduni ni immoral, na kisheria hairuhusiwi.

Unajua kuwa Dini ndio Utamaduni wenyewe unazungumzia mambo ya taboos?
 
Usipomuabudu Mungu
Utapata miungu ya kuabudu
Dah, kwani binadamu hawezi kuishi bila kuabudu??

Mbona mnamshisha binadamu na kumfanya kama kiumbe dhaifu kuliko nyani?

Nyani hawaabudu, mbona wanaishi? Wanapata mahitaji yao na maisha yanaenda.
Inamaana binadamu ndio kiumbe hafifu lazima atafute likitu la kuabudu sio?
 
Kanisa ni kituo cha kulelea maadili.

Sijasema Kanisa ni baya.
ila ukishakuwa mkubwa na maadili yako halina maana tena.
Yani ushanufaika na neno la Mungu na kanisa afu ukubwani unalikana
Unapomkana Mungu/imani yako umekana na Kanisa/watumishi wa Mungu
Usipeleke mtoto huko mfundishe Sayansi Mama Mungu si hayupo?
Malezi ya kumjua Mungu ya nini na ushaona hayupo?


Sema tu ur bored na routine ya kanisani
Ama km umemkataa Mungu mkatae na kila kitu chake uvuguvugu wa nini?

Unajicontradict
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Dah, kwani binadamu hawezi kuishi bila kuabudu??

Mbona mnamshisha binadamu na kumfanya kama kiumbe dhaifu kuliko nyani?

Nyani hawaabudu, mbona wanaishi? Wanapata mahitaji yao na maisha yanaenda.
Inamaana binadamu ndio kiumbe hafifu lazima atafute likitu la kuabudu sio?
Kama sasa Ibada yako ni upingaji wa uwepo wa Mungu
 
Yani ushanufaika na neno la Mungu na kanisa afu ukubwani unalikana
Unapomkana Mungu/imani yako umekana na Kanisa/watumishi wa Mungu
Usipeleke mtoto huko mfundishe Sayansi Mama Mungu si hayupo?
Malezi ya kumjua Mungu ya nini na ushaona hayupo?


Sema tu ur bored na routine ya kanisani
Ama km umemkataa Mungu mkatae na kila kitu chake uvuguvugu wa nini?

Unajicontradict
Mimi kusema Mungu hayupo haimaanishi dini haina umuhimu.
Dina ina mapungufu yake mengi na ina faida zake chache.

Naweza kuwapeleka ili wafunzwe uoga utotoni (uoga wa kutenda dhambi) lakini Nitajitahidi sana wanangu wasiliwe ubongo na dini na kugeuka misukule kama ya kwa mwamposa.

Maana ukishaliwa ubongo huko kutoka ni ngumu.

Wachache tulioweza kutoka tunashukuru.

So kuwapeleka wakiwa wadogo ni nzuri ila wakishafika miaka 12 kuendelea nawaachisha.
 
Mzazi yupo sawa sababu we ni mtoto wake hataki uharibikiwe na kingine bado unaishi chini ya wazazi wako unatakiwa ufate kile wanachokwambia

Kijana mdogo ushaona dini uliyozaliwa ndani yake uiamini

Acha kujipa usahihi na mzazi wako mzazi huwa hakosei hata siku moja
nakazia hapa
 
Kama sasa Ibada yako ni upingaji wa uwepo wa Mungu
Kwani mtu akipinga uwepo wa mungu,, huyo mungu atapata athari gani?,,
Maandiko yanasema, binadamu alipewa utashi wa kuamua mwenyewe na sio kushurutishwa,,
Kuabudu hakumuongezei kitu mungu,, wahindi wanaabudu ng'ombe, sanamu, etc wachina wanaabudi budha, na maisha yanakwenda.
Binaadamu yuko huru
 
Pamoja na kwamba siungi mkono kutokusali; ila kwa ulivyo andika tu, you are so bright na unahitaji kuelekezwa kwa hoja za nguvu na sio kwa mazoea. Nakushauri pamoja na kutowiwa kwenda kanisani nakushauri Usome; kama ulisha soma Biblia jaribu kusoma Vitabu vya Dini tofauti.
Hii inaweza kukusaidia kwani bottom line; Mungu yupo, siku ya mwisho ipo, ambapo watu watahukumiwa kutoa haki kwa walioikosa hapa duniani ILA namna gani ya kumjua Mungu sahihi wa kumfuata ndio kazi hapo......SOMA!
Hakuna siku ya mwisho, siku yako ndio mwisho ila kwa wengine bado wataendelea kuishi, na hukumu pia hakuna hukumu hiyo, malipo ni hapa hapa ukiiba kabla hujaondoka ulimwengu huu lazima ulipe malipo ya uwizi
 
Unajua kuwa Dini ndio Utamaduni wenyewe unazungumzia mambo ya taboos?
Ni kweli dini ni utamaduni...Lakini utamaduni sio dini.
Dini ni subpart ndogo ya utamaduni.

Utamaduni una mambo mengi, Taboos zipo ndani ya utamaduni. Na zingine ndani ya dini.

Mfano kuna kabila mwanamke hatakiwi kula map*mbu ya ng'ombe au mbuzi...Hiyo ni Taboo lakini haihusiani na dini yoyote.

So kitu kuwa Taboo usiforce kinahusiana na dini automatically.
Hata babu zetu hawakuoana wao kwa wao kabla ya dini kufika na mashua.
 
Mimi kusema Mungu hayupo haimaanishi dini haina umuhimu.
Dina ina mapungufu yake mengi na ina faida zake chache.

Naweza kuwapeleka ili wafunzwe uoga utotoni (uoga wa kutenda dhambi) lakini Nitajitahidi sana wanangu wasiliwe ubongo na dini na kugeuka misukule kama ya kwa mwamposa.

Maana ukishaliwa ubongo huko kutoka ni ngumu.

Wachache tulioweza kutoka tunashukuru.

So kuwapeleka wakiwa wadogo ni nzuri ila wakishafika miaka 12 kuendelea nawaachisha.
Dhambi ni misimamo/sheria za Mungu
Atheists mnaamini Mungu hayupo so kwenu hamna dhambi

Woga wa dhambi wa nini Mama na Mungu hayupo?
We staki nataka wa Mungu
 
Kwani mtu akipinga uwepo wa mungu,, huyo mungu atapata athari gani?,,
Maandiko yanasema, binadamu alipewa utashi wa kuamua mwenyewe na sio kushurutishwa,,
Kuabudu hakumuongezei kitu mungu,, wahindi wanaabudu ng'ombe, sanamu, etc wachina wanaabudi budha, na maisha yanakwenda.
Binaadamu yuko huru
Hakuna athari
Kwani Mungu yupo?
Heri we umemkana full
Kuliko mwenzio anasema Mungu hayupo ila watoto atawapeleka kanisani😅
 
Dhambi ni misimamo/sheria za Mungu
Atheists mnaamini Mungu hayupo so kwenu hamna dhambi

Woga wa dhambi wa nini Mama na Mungu hayupo?
We staki nataka wa Mungu
Actually natumia lugha yako ili unielewe kirahisi.
Nimesema dhambi kwa context ya kanisani, lakini mimi naangalia Morality in generall, kujua mema na mabaya.

Kuiba, kuzini, kuua, kudanganya nk. Nk.
Ni vitu vya morality, Visingefundishwa kanisani nisingepeleka watoto kanisani...

Na hata mm nkiwa na muda wa kukaa kuwafundisha hivi vitu sitowapeleka.
Ikitokea organization ya kufundisha morality kwa watoto bila dini ntawapeleka huko.

Morality ya kufundishwa in form of stories na vitisho...kama wanavyofanya kanisani.
 
Ni kweli dini ni utamaduni...Lakini utamaduni sio dini.
Dini ni subpart ndogo ya utamaduni.

Utamaduni una mambo mengi, Taboos zipo ndani ya utamaduni. Na zingine ndani ya dini.

Mfano kuna kabila mwanamke hatakiwi kula map*mbu ya ng'ombe au mbuzi...Hiyo ni Taboo lakini haihusiani na dini yoyote.

So kitu kuwa Taboo usiforce kinahusiana na dini automatically.
Hata babu zetu hawakuoana wao kwa wao kabla ya dini kufika na mashua.

Taboo lazima ihusiane na Dini,
Taboo inahusiana na miungu na ukishasema miungu moja Kwa moja unataja Dini.
Taboo ni miiko. Na miiko inahusianishwa na Imani Fulani Kwa miungu.

Embu nitajie Taboo yoyote unayoijua ambayo haiendani na Dini?
Vinginevyo hujui maana ya DINI
T
 
😂,Sijui tukusaidie vipi🙆‍♀️,inakaa kama mamako ni mkristo mwenye itikadi kali,, hao huwa hawaelewi kitu, hata umweleweshe vipi,, anza kwenda kanisani au uondoke ukapange chumba kwingine
Dah, kazi ninayo
 
Back
Top Bottom