Upo sahihi kabisa na wala haujakosea katika maelezo mtaji wake wa kufanya yote anautoa wapiInawezekana kabisa msomi akaanzisha biashara ya chipsi kisomi,
Sawa Jimmy muuza Viepe,We dogo una akili mgando, huamini kwenye hustles. Unaamini kwenye connections na huko kutiwa dole.
Pambana chalii, nilichogundua graduates wengi ni wavivu mno, hasa wale fresh from school.
Mpama mtaa uwachape ndo wanakubali kuhustle kitaa ila ile fresh kabisa hawezi zama kitaa nae atataka kazi za kiyoyozi.
Kama hana akili za kujiongeza Kwa nini usimpe kazi Yako?Inahuzunisha sana kuona kazi wafanyazo watoto waliosomeshwa kwa gharama wakiwa bodaboda na wachoma chips.
Mzazi kugharamia masomo ya mwanao ili aje kuwa mpambaniaji wa kazi hizo na za namna hiyo au kutokuja kuwa na future yoyote mtaani inaleta huzuni kwa mtoto mwenyewe hata kwa mzazi pia.
Wanasiasa hawafanyi ujinga huu kamwe wao na kizazi chao wanaandaliana future bora watoto wao. Hakuna mwanasiasa hata mmoja ataruhusu mwanae awe boda boda au mchoma chipsi wala kutanga tanga mtaani hovyo bila future yoyote ile.
Mzazi jukumu lako lisiishie kuzaa na kupeleka mtoto shule pekee bali muandalie na future bora mtoto wako.
[IMG alt="lukesam"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/275/275627.jpg?1500562796[/IMG]
lukesam
JF-Expert Member
Inawezekana wazee wetu walishakosea huko nyuma ila sasa ni muda wa kujisahihisha na kuwa bora kuliko wao.
- "Hatuwezi kuwa matajiri wote kama Bakhresa lakini ni vizuri sisi watu weusi tukajifunza kwao na jamii nyingine kama za wahindi.
Wazazi wa kiafrika wana tabia za kichoyo na kibinafsi, hata akiwa na duka lake hataki mtoto wake auze au ajue jinsi ya kuendesha biashara, anaogopa kuibiwa hata kijana wake hamuamini.
Watoto wetu wanahangaika sana kutafuta ajira kwasababu walienda shule kusomea taaluma za ndoto zao bila kujua baada ya kumaliza wataenda kufanyia kazi wapi. Tofauti na sisi, hawa wenye asili ya kihindi na matajiri wengine, watoto wao wanaenda shule kusomea taaluma ambazo wanajua wakitoka hapo wataenda kupata ajira kwenye miradi ya familia.
Tuweke nguvu katika kuanzisha miradi ya kifamilia, familia za kitanzania tuache ubinafsi. Ndio maana hata ukimshauri mtu aandike wosia au agawe mali zake akiwa hai anakushangaa, mzee kabisa anataka afe akiwa anamiliki mali zake zote.
Suluhisho la kusomea uhasibu au uchumi na kuishia kuwa muuza chipsi au bodaboda ni kuanzisha miradi ya kifamilia. Binafsi naona hii itapunguza sana tatizo la ajira na hali ya umaskini katika familia zetu.
Inaumiza sana kupoteza miaka mingi shuleni na kuishia kufanya kazi ambazo hata hazihitaji elimu".
Nadhani hujakulia kijijini , kule familia nzima mnaenda Shamba, wakati wa likizo inasaidia kuzalisha chakula mnachokula na urithi ni hayo mashambaHiyo nayo option nzuri kama familia haina uwezo kabisa wajaribu hata kazi wanazofanya wawapatie ujuzi watoto wao.
Wazazi wanao fanya biashara,kilimo hata ndogo ndogo wasiwafiche watoto wao waanze kuwaandalia mazoea na usimamizi bora wa hizo kazi mdogo mdogo
Sehemu ya usomi ni kujua pa kupata mitaji. Siku hizi kuna mpaka Venture Capitalist na Angel Capitalists maalum wamejikita kufanya biashara na watu wa Global South, hii mitaji ya $10,000 - 20,000 ni rahisi sana kupata kama una idea nzuri na unaweza kui present.Upo sahihi kabisa na wala haujakosea katika maelezo mtaji wake wa kufanya yote anautoa wapi
Sasa wewe unadhani wanatakiwa wamfundishe nini? Kazi Ile Ile ya kwao harafu yeye akimaliza shule yake aje kuongeza input kwenye mradi huo.Mkuu hii imekaa poa. Lakini changamoto kuna familia unaweza ukadondosha chozi kwa hali waliyo nayo. Hata hiyo kuandaa future ya mtoto wanaiandaaje zaidi ya kumpeleka shule tu?
Labda kama watamfundisha shughuli ambazo wao wanafanya ili nae aje kuendeleza. Kama ni kupasua mawe basi nae aishi humo, kama ni uvuvi aishi humo pia.
So sad for sure
Upo Kama Mimi aisee, babangu ndo pekee anaeelewa hii situation.....Mungu ampe kheri zaidi na zaidi.Tuliosoma na tunapitia haya tunaelewa maumivu yake. Binafsi napitia haya. Baba yangu ni rafiki mfariji pekee anayeelewa maumivu yake na anasikitika sana.
Wote wataenda Ferry? Wenye fursa hizo ni wachache ila majority ni fukara tuu.Zote ni kazi isipokuwa inategema unafanya kwa namna gani, Hakimu Mahakama za Wilaya tunawalipa 1,700,000/-[milioni moja laki saba ]kwa mwezi na kwa siku 56,666.6/- [elfu hamsini na sita]
Muuza Maandazi pale Ferry-upande wa Kigamboni banda la tatu mkono wa kushoto anafunga 9,000,000/-[milioni tisa]kwa mwezi na Tshs 300,000/- [laki tatu] kwa siku.
Kwa Mwaka HAKIMU = 20,400,000/- [Milioni ishirini na laki nne]
Kwa Mwaka Muuza Maandazi Ferry = 108,000,000/- [milioni mia moja na nane]
Muuza maandazi wa Ferry halipi kodi wala hana TIN, TFDA , OSHA, NSSF, FIRE na manispaa wala hawaangaikinnaye maana ni mmchinga, ukishuka tu ferry banda la tatu lililojaa vitafunwa, .
Kila pantoni inaposhusha anauza si chini ya elfu 30 sasa ukitoa ghrama zote ndio inabaki laki tatu.
Wafanyakazi wanaingia kwa shifti.
Shida inaanzia serikalini na viongozi wetu, serikali haijatengeneza ajira nyingi, serikali hijaweka mazingira rahisi mtu kujiajiri, anaetaka kujiajiri nchi hii kuna shughuli pevu mno.
NEPOTISM imetawala, mambo yanakwenda kiUNDUGUNAIZESHENI, viongozi wako bize wanaandaa kesho ya watoto wao sio ya taifa
Ndio mtaala Mpya unaenda kufanya hayoHuko huko chuo wapewe mafunzi yakujitegemea kama wafanyavyo VETA
We jamaa unastahili kupewa PhD ya heshima.Unauliza kama kutoamini kuwa kuna nguvu ya Mungu ni sawa? Au ni kuamini kitu kilicho kweli?
Tushaona imani unaweza kuamini hata uongo, kitu cha muhimu ni ukweli. Kwa nini unajikita kwenye imani bado?
Hayo ni maswali mawili tofauti.
Swali la kwanza, kuamini, au kutoamini kwamba kuna nguvu ya Mungu (hizi ni pande mbili za shilingi moja ile ile) sio tu ni sawa, hii ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania. Pia, hii ni haki ya binadamu iliyopitishwa katika Universal Declaration of Human Rights. Azimio hili limepitishwa na Umoja wa Mataifa December 10 1948.
KIla mtu ana haki ya kibinadamu ya kuamini au kutoamini nguvu za Mungu wake anavyotaka. Na katika kuongelea imani, maadam tunaongelea imani tu, hakuna imani iliyoishinda nyingine, maadam haiingilii uhuru wa wengine.
Kwa hivyo, ukitaka kuamini nguvu za Mungu wako ambaye ni mti wa mbuyu, una haki hiyo, na hilo ni sawa. Ukitaka kuamini Mungu wako ni Yesu Kristo Masiha, una haki hiyo, na hilo ni sawa. Ukitaka kuamini Mungu wako Allah, ni haki yako, na hilo ni sawa, ukitaka kuamini miungu yako isiyo na idadi, una haki hiyo, na hilo ni sawa, ukitaka kutoamini Mungu yeyote, kama mimi, ukasema hizi habari za Mungu zote ni ujinga mtupu, hiyo nayo ni haki yako ya kibinadamu, ni sawa tu.
Na mimi, licha ya kutoamini Mungu yeyote, tukiwa katika habari za imani, natetea haki za watu wote kuamini wanavyotaka, au kutoamini, ilimradi kuwe na mipaka mizuri ya kutoingiliana.
Hilo ni swali la kwanza, kutoamini katika nguvu ya Mungu katika maisha ya binadamu ni sawa?
Kwa kuwa tumekubaliana awali kwamba ukweli ni muhimu kuliko imani, kwa sababu ukweli upo mmoja tu, na imani unaweza kuamini hata uongo, tunapata swali la pili tofauti. Swali la kuangalia ukweli.
Je, ukiamini katika nguvu za Mungu unaamini katika ukweli? Huyo Mungu yupi kweli?.
Jibu ni, kwa kuanzia Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na uoendo wote anayesemwa kuwa ni muumba wa vyote, Mungu huyu hayupo, anaweza kuoneshwa kimantiki kwamba huyu ni muhusika wa hadithi ya kutungwa na watu tu, na hivyo, kuamini katika nguvu zake ni sawa na kuangakia sinema ya James Bond 007 na kujirusha kutoka ghorofani ukiamini kwamba utaruka kwa nguvu za Ki James Bond kutika katika filamu ya Casino Royale.
Mzazi anakuwa anakuwa hajui mkuuInahuzunisha sana kuona kazi wafanyazo watoto waliosomeshwa kwa gharama wakiwa bodaboda na wachoma chips.
Mzazi kugharamia masomo ya mwanao ili aje kuwa mpambaniaji wa kazi hizo na za namna hiyo au kutokuja kuwa na future yoyote mtaani inaleta huzuni kwa mtoto mwenyewe hata kwa mzazi pia.
Wanasiasa hawafanyi ujinga huu kamwe wao na kizazi chao wanaandaliana future bora watoto wao. Hakuna mwanasiasa hata mmoja ataruhusu mwanae awe boda boda au mchoma chipsi wala kutanga tanga mtaani hovyo bila future yoyote ile.
Mzazi jukumu lako lisiishie kuzaa na kupeleka mtoto shule pekee bali muandalie na future bora mtoto wako.
[IMG alt="lukesam"]https://www.jamiiforums.com/data/avatars/m/275/275627.jpg?1500562796[/IMG]
lukesam
JF-Expert Member
Inawezekana wazee wetu walishakosea huko nyuma ila sasa ni muda wa kujisahihisha na kuwa bora kuliko wao.
- "Hatuwezi kuwa matajiri wote kama Bakhresa lakini ni vizuri sisi watu weusi tukajifunza kwao na jamii nyingine kama za wahindi.
Wazazi wa kiafrika wana tabia za kichoyo na kibinafsi, hata akiwa na duka lake hataki mtoto wake auze au ajue jinsi ya kuendesha biashara, anaogopa kuibiwa hata kijana wake hamuamini.
Watoto wetu wanahangaika sana kutafuta ajira kwasababu walienda shule kusomea taaluma za ndoto zao bila kujua baada ya kumaliza wataenda kufanyia kazi wapi. Tofauti na sisi, hawa wenye asili ya kihindi na matajiri wengine, watoto wao wanaenda shule kusomea taaluma ambazo wanajua wakitoka hapo wataenda kupata ajira kwenye miradi ya familia.
Tuweke nguvu katika kuanzisha miradi ya kifamilia, familia za kitanzania tuache ubinafsi. Ndio maana hata ukimshauri mtu aandike wosia au agawe mali zake akiwa hai anakushangaa, mzee kabisa anataka afe akiwa anamiliki mali zake zote.
Suluhisho la kusomea uhasibu au uchumi na kuishia kuwa muuza chipsi au bodaboda ni kuanzisha miradi ya kifamilia. Binafsi naona hii itapunguza sana tatizo la ajira na hali ya umaskini katika familia zetu.
Inaumiza sana kupoteza miaka mingi shuleni na kuishia kufanya kazi ambazo hata hazihitaji elimu".
Hahaa. Kwa nini mkuu, mbona vitu vya kawaida tu?We jamaa unastahili kupewa PhD ya heshima.
Kazi nyingi ndogo ndogo Zina pesa kuliko hizo kubwa Kwa sababu hizi hazina Cha TRA Wala leseni ni Nguvu zako tuu.Wabongo bwana..sijui mnaona hizo kazi ndogo hazina hela ama vpi...mnadhan kukaa ofisin kuvaa vizuri ndo kuwa na hadhi inayoendana na elimu yako?...na ndo maana wasomi wengi wanaogopa kufanya vikazi hv vidogovidogo wanaogopa kudhalilika
Kuna dogo mmoja nipo nae pale mtaani..ni form 4 tu...kahangaika sana kujitafuta lkn mambo yakawa hayamwendei poa...
Siku moja nipo likizo akaja home kunisalimia..baada ya mazungumzo ya hapa na pale akaniambia changamoto zake za ujasiriamali( alikuwa anauza maji stand pugu b4 haijaamishwa)..sasa katika kupiga stori tu nikamwambia kwa nn asipige biashara ya chips(ilikuwa kama utani tu hata sikuitilia maanani)
Bhana wee..yule dogo wiki iliyofata akanifata akaniambia amepata eneo...kafungua kibanda..utani utani tu...
Wiki iliyopita j2 nilirudi likizo home..nikamfata pale kijiweni kwake(saa 4 huyo usiku)..akaniambia bro..mm hapa nafunga sa 10 asubuhi...nauza mpk nashngaa...kwa siku akitoa kila kitu anakunja si chini ya 90k..yani hiyo ni siku hajauza sana...kuna siku anapiga mpk 140k huko(hasa weekend)
Sasa kwa mwez hyo ni sh ngap?ww unaekaa ofisin unalipwa laki 7 kila siku kugombania daladala na yeye anaetoka kwake anaenda kazini kwa miguu dk 0 kashafika nan anaishi vizur?
Hzi biashara ndogondogo zinalipa..inshu ni location..ukiipatia location..utashangaa mwenyewe mpk unajiuliza siku zote ulikuwa WAPI
Nimetoa mfano wa Ferry tu , sasa nakupa mwengine>Wote wataenda Ferry? Wenye fursa hizo ni wachache ila majority ni fukara tuu.
But kujiajiri kama una pa kuanzia au location Ina afadhari ila kujiajiri Kwa kujikimu Bora Ajira.
Kiranga! Hivi hili la wengi wa viongozi wetu kutokea familia masikini kisha tukawapa madaraka makubwa mfano Uwaziri, Ukatibu wa Wizara na hata Urais, je wewe binafsi waona ni zuri jambo hili? Pia, umewahi kufikiri kujihusisha na siasa za hapa nyumbani TZ?Hahaa. Kwa nini mkuu, mbona vitu vya kawaida tu?
Umasikini nini?Kiranga! Hivi hili la wengi wa viongozi wetu kutokea familia masikini kisha tukawapa madaraka makubwa mfano Uwaziri, Ukatibu wa Wizara na hata Urais, je wewe binafsi waona ni zuri jambo hili? Pia, umewahi kufikiri kujihusisha na siasa za hapa nyumbani TZ?
Hii dhana ilinichanganya sana. Kwa muktadha huo wa 'tafsiri ya masikini', basi nimepata suluhu. Shukrani mkuu[emoji120]Umasikini nini?
Inawezekana mtu akawa na umasikini wa mali halafu akawa na utajiri wa mawazo wa kuweza kuongoza?
Nina tatizo kubwa sana na wazo la kumpa au kumzuia mtu uongozi kwa kuangalia yeye masikini au tajiri.
Kwanza kabisa, kidemokrasia, kumnyima mtu uongozi kwa sababu yeye ni masikini ni kuwanyima watu wengi nafasi za uongozi. Kwa hiyo hii si demokrasia.
Pia, uwezo wa uongozi si lazima uendane na uwezo wa kiuchumi. Hivyo, ukisema masikini asiongoze, unaweza kujinyima talent ya watu wengi wanaoweza kuongoza.
Lakini zaidi, hata ukisema uwape matajiri tu uongozi, huna guarantee kwamba mtu kuweza kujitajirisha yeye ndiyo kigezo cha kuweza kuitajirisha jamii, kwa sababu mtu anaweza kuwa mbinafsi anayeweza kujitajirisha yeye vizuri, lakini asiijali jamii. Na hapo utajiri wake unakuwa disqualification actually.
Kwa hivyo, ningependa watu kupewa uongozi on the merit, kwa kuangalia uwezo wao wa kuongoza, bila kujali wao ni matajiri au masikini.
Kwa msingi huu, mtu tajiri, ambaye ni mwizi, kapata utajiri wake kwa wizi, anakuwa disqualified kuongoza, na mtu ambaye amekuwa masikini, licha ya kuwa alikuwa na nafasi kubwa sana ya kuiba akajizuia, anaonekana atafaa sana kuongiza, kwa sababu ana sifa ya uadilifu.
Tunatakiwa kuupiga vita umasikini kiasi kwamba tuwe na nafasi nyingi za kuukwepa umasikini bila kupitia uongozi. Tupate viongozi ambao wanataka kuongoza ili kutatua matatizo ya jamii, si kujitajirisha.