Mzazi unasomesha mtoto aje kuuza chips na kuwa bodaboda. Inahuzunisha sana!

bora hata ya hao waliosomeshwa na wazazi na wanauza chips......sisi tumejisomesha wenyewe tena kwa mbinde saaaana na wazazi wanatulilia matatizo balaa
 
Kwani wewe mzazi unafanya shughuli gani?
 
Zote ni kazi isipokuwa inategema unafanya kwa namna gani, Hakimu Mahakama za Wilaya tunawalipa 1,700,000/-[milioni moja laki saba ]kwa mwezi na kwa siku 56,666.6/- [elfu hamsini na sita]

Muuza Maandazi pale Ferry-upande wa Kigamboni banda la tatu mkono wa kushoto anafunga 9,000,000/-[milioni tisa]kwa mwezi na Tshs 300,000/- [laki tatu] kwa siku.

Kwa Mwaka HAKIMU = 20,400,000/- [Milioni ishirini na laki nne]

Kwa Mwaka Muuza Maandazi Ferry = 108,000,000/- [milioni mia moja na nane]

Muuza maandazi wa Ferry halipi kodi wala hana TIN, TFDA , OSHA, NSSF, FIRE na manispaa wala hawaangaikinnaye maana ni mmchinga, ukishuka tu ferry banda la tatu lililojaa vitafunwa, .
Kila pantoni inaposhusha anauza si chini ya elfu 30 sasa ukitoa ghrama zote ndio inabaki laki tatu.
Wafanyakazi wanaingia kwa shifti.
 
Forced idleness ni ngoma moja nzito, very suffocating!. Kwa sasa tuwekexe kwenye proposals za kutatua changamoto za jamii. Nimeona wengi wanapitia huko kwa miaka hii. Huko Fursa zipo kila leo
 
Mwanangu unajua kijiwe cha chipsi kina pesa chafu?

Watu tunalaza 80,000 mpaka 100,000 after all expenditures daily we unachukulia poa chipsi.?

Najua kuna chipsi vibanda haviingizi hiyo hela, sawa. Lakini nanyi huko kazini si wote mnaingiza hela nzuri. Wengine wana degree tangu mwaka 2015 waajiriwe kwa mshahara wa 750,000 mpaka leo hii hawajapata nyongeza. Sijui ndio Samia mwaka jana kaongeza kidogo.

Sema wabongo mmekariri kila aliyepita shule lazima aajiriwe hata kama analipwa kiduchu ili tu mzazi afurahi kuona mwanawe yuko kwenye payroll na akisimama kujitambulisha aseme nafanya kazi sehemu fulani ilihali ni kapuku.

Cha msingi maokoto, nunua kigari chako, jenga nyumba huko Kibamba.
Shida mkiona mtu ana gari mnawaza anafanya kazi wapi? Ushawahi kufikiria mtu amejiajiri?
 
Kwa sisi wazee wa Physics tunasema the warkdone is equal to zero.
 
Upeo wako mdogo. Iko hivi umetoa wazo vizur ila kulilia kuajiriwa sio kwamba title na kuridhika na salary ya 750. Kuajiriwa kwa masikini ni assuarance ya kipato na mtaji.

Maana kitendo chakupata ajira nakuwa na uhakika wakulipwa ni chanzo cha mtaji wakumilik hata hivyo vibanda vya chips 10... Nika wanangu wana maisha sana sababu wanajielewa na wamewekeza sana biashara mbalimbali wana majumba magari lakin yote yametokana na ajira zao
 
Hope means nothing
 

Inaumiza sana asee ila kama mzazi huna budi kufanya sehemu yako.
 
Kibanda chako cha chipsi Kiko wapi nije kula leo
 
Kibanda chako cha chipsi Kiko wapi nije kula leo
Chips siyo chakula, sema "kibanda kipo wapi nije kutafuna vibanzi?"

Chips=Kibanzi
Chips siyo chakula, ni junk- kitafunwa.
Kama wewe ni mwanaume na unakula kama chakula ujue ukipiga paip utakuwa unatoa hewa tu lakini pia huwezi mfikisha Gilmans point.
 
Unaongea kweli???
 
Changamoto ya ajira inaanzia hapa. Wazazi wetu wengi ni masikini kipato cha chini kabisa na wametusomesha kwa kuunga unga. Hawana connection zakutosha na walizonazo hazina uzito tokana na walicho nacho, tunaelewa mtu kitu.
Sahihi mkuu. Amewazia upande mmoja. Upande wa pili ndio mgumu kwa hili analolisema
Shida inaanzia serikalini na viongozi wetu, serikali haijatengeneza ajira nyingi, serikali hijaweka mazingira rahisi mtu kujiajiri, anaetaka kujiajiri nchi hii kuna shughuli pevu mno.

NEPOTISM imetawala, mambo yanakwenda kiUNDUGUNAIZESHENI, viongozi wako bize wanaandaa kesho ya watoto wao sio ya taifa
 
Kutoamini uwepo wa Mungu ni kukata tamaa kwa kiwango cha mwisho Kiranga
 
Mzazi aandae vipi future wakati yeye mwenyewe nanga inapaa?

Anachoweza ni kupambania mtoto asome, akimaliza shule ajipambanie.

Ila kwa namna moja naona wazo lako la kutotumia magharama makubwa kusomesha linamake sense, coz asome shule za kawaida au English medium, akimaliza chuo kama huna connection anaishia pale pale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…