Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara

Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara

Habarini ndugu

Baada ya kupata mtoto, ilibidi mzazi mwenzangu aje nyumbani kwetu kumleta mtoto Bibi yake amuone kwani alikuwa na shauku ya kumuona mjukuu wake.

Walikaa kwa kipindi cha miezi kadhaa, na walikaa kwa furaha na amani. Mama yangu alifurahi kwani mwanzo aliona na kusifia tabia nzuri na kujituma kwa binti yule.

Kadri siku zilivyokuwa zinasonga, nikahisi kuna jambo halipo sawa, kila nikiongea na Mama kuhusu mipango ya baadae alikuwa haonyeshi dalili za kubashiri ndoa yangu na binti yule. Nikajua tu hajaridhika nae.

Lakini naamini Mzazi wangu ananijua vizuri na anajua ni kipi kitanifaa na kuendana na mimi, nahisi kuna vitu amegundua kwa binti yule kwa muda aliokaa nae.

Mimi sina tatizo na mawazo na ushauri wa Mzazi wangu, lakini najiuliza je ni sahihi kuendelea kumuaminisha binti huyu kwamba nitamuoa ilihali najua Mzazi wangu hajaridhika nae?

Najiuliza nimwambie mapema kwamba haitowezekana kufunga ndoa hapo badae? Naogopa kumpa maumivu na kumfanya akose amani.......

Ni uamuzi gani wa busara napaswa kufanya wadau? Naombeni ushauri wenu bila kebehi na masihara..

Asanteni.....
Wazee wanaona mengi, labda ameona kwamba mchumba ni mchawi.

Ukitaka kujua, nenda kanywe dawa za kuona wachawi, kuna jamaa mmoja ofisini alikunywa hizo, kuingia ofisini anaona mmoja wa watumishi, dada mrwmbo, anatembea lakini makalioni unatoka moto unawaka, mwingine ana mafuvu ya watu mezani
 
Mwanamke pekee ambaye Mama yako atamkubali ni yule atakayekuchagulia yeye.

Mwambie akutafutie anayekufaa zaidi ya hapo wewe hutokaa umpate
 
ingia ofisini anaona mmoja wa watumishi, dada mrwmbo, anatembea lakini makalioni unatoka moto unawaka, mwingine ana mafuvu ya watu mezani
Mkuu hilo ni jambo la msingi kuzingatia, lakini katika uzi huu nimeandika kwa ufupi sana, ila naamini nikiambiwa sababu nitarudi tena kuleta mrejesho
 
Kila mtu ana uhuru wa kuleta uzi wowote kwa wakati wowote, ilimradi asivunje sheria za jukwaa
Watu smart wamekusoma,
Lengo lako ni kuleta Uzi na si kutatua tatizo hongera sana kwa uhuru wa kuleta uzi
 
Mwanamke pekee ambaye Mama yako atamkubali ni yule atakayekuchagulia yeye.

Mwambie akutafutie anayekufaa zaidi ya hapo wewe hutokaa umpate
Hawezi kujitafutia, mimi natafuta then yeye anamuona na kutoa mtazamo wake
 
Watu smart wamekusoma,
Lengo lako ni kuleta Uzi na si kutatua tatizo hongera sana kwa uhuru wa kuleta uzi
Hakuna tatizo linalohitaji utatuzi, kinacho hitajika ni kuona mawazo ya wengine ili kuimarisha uelewa na uwezo wa kuamua katika maswala ya ndoa na familia
 
MSIKILIZE MZAZI
WAZAZI NI WACHAWI😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Mimi ndyo naoa lakini lazima nipate maoni ya wazazi wangu
Uko sawa mkuu, lakini kinamama ni waoga sana anaweza akawa ameona dhaifu moja tu kati ya 10 likamfanya apate wasiwasi.

We kaa nae chini mzazi muulize kwanini amekua mzito wa kubariki maamuzi yako na mchumba wako. Jibu atakalokupa linaweza kukupa mwanga juu ya maamuzi yako
 
Uko sawa mkuu, lakini kinamama ni waoga sana anaweza akawa ameona dhaifu moja tu kati ya 10 likamfanya apate wasiwasi.

We kaa nae chini mzazi muulize kwanini amekua mzito wa kubariki maamuzi yako na mchumba wako. Jibu atakalokupa linaweza kukupa mwanga juu ya maamuzi yako
Na hilo ndilo jambo la msingi, kukaa na kumuuliza kama kuna kitu amekiona, akiniambia na mimi nitakuwa nimepata mwanga

Mimi muda mwingi sipo nyumbani na yeye ndyo anakaa nae muda mwing
 
Huyo mama yako siyo anaeoa. Yaani umekaa na binti wa mwenzio halafu unasema humtaki, mama ana moyo mdogo.
 
Atakuambia ni mvivu au ni mchafu na mengi kibao, haya yeye wa binti zake wamekamilika ?
Uvivu na uchafu siwezi kukubali kwani najua binti ni msafi na anajituma, labda kama kuna lingine
 
Back
Top Bottom