Temea chini nuksi hiyo isikuvae.
Kama una makandokando ya kutohudhuria misiba ya kwenye nzengo unayoishi, jitahidi ndugu nenda, siku hiyo ua shughuli zako.
Jamii inayokuzunguka ndiyo wanaokupima nyendo na tabia zako.
Hapa siyo Ulaya utasema kuna vikundi vya mazishi na wafariji wa kukodi.
Ukiona jamii inakutenga siku ya msiba wako, cha kufanya kuwa mpole, usilete ujuaji ama ngebe zako kabisa.
Hapo huwa imelengwa faini ya kujikosha na kurejeshwa kundini.
Kwa hiyo faini itakayoamriwa ndugu watakuchangia na ikishatolewa, watu wataendelea kushirikiana na wewe kama kawaida.
Mi niliona hayo kwa ndugu yangu, ilibidi wanandugu tuchangishane kununua huyo ng'ombe aliotozwa na nzengo katikati ya msiba, watu wamegoma kuzika mpaka ng'ombe alipotoka ndiyohali ya hewa ikarejea kawaida.
Mambo ya kijamii ni marahisi pia ni magumu sana usiombee yakukute mr.