Mzee Warioba ateuliwe tena kukamilisha kazi aliyotumwa na Watanzania

Mzee Warioba ateuliwe tena kukamilisha kazi aliyotumwa na Watanzania

Ni muda mwafaka Kwa Taifa letu:

1. Kupata Mawaziri wasiotokana na wabunge.

2. Wakuu wa wilaya na mikoa waondolewe, tupate viongozi wa kisiasa waliopigiwa kura kuanzia mbunge, diwani, mkuu wa Jimbo nk.

3. Viongozi watangaze Mali zao wanapoingia katika uongozi na wanapotoka.

4. Wazee wote walipwe pension bila ubaguzi unaowaacha waliofanya KAZI sekta binafsi, Nchi itabarikiwa.

5. Sauti ya wananchi iheshimiwe. TABIA hii ya kutowajibika Kwa viongozi wanaotuhumiwa Kwa RUSHWA ikome. Katiba mpya tuhakikishe inatatua shida hii.

6. Wezi wote walioliibia Taifa ktk miradi mbalimbali warudishe pesa zetu.

Tusipoteze Kodi za wananchi kuzungukwa Bure, Rasimu alosimamia Judge WARIOBA irudi mezani tufanye marekebisho.

Mzee Warioba ateuliwe kumalizia KAZI njema aliyoianza.
Umesahau na hili japo najua wote watalipinga ila mimi na wananchi wenzangu wenye akili timamu tunalitaka sana uwakilishi wa wananchi jimboni uwe na ukomo wa miaka 15 yani vipindi vitatu tu Tu dadeeeki
 
Umesahau na hili japo najua wote watalipinga ila mimi na wananchi wenzangu wenye akili timamu tunalitaka sana uwakilishi wa wananchi jimboni uwe na ukomo wa miaka 15 yani vipindi vitatu tu Tu dadeeeki
Na wabunge Bungeni wasizidi 80.

Majimbo yapunguzwe na tuchague wabunge Wachache lakini wenye uwezo wa kuisimamia Serikali.

Unaweza ona wabunge ni wengi mchango na hoja hafifu KAZI Yao ni kupasha viti joto.
 
Umesahau na hili japo najua wote watalipinga ila mimi na wananchi wenzangu wenye akili timamu tunalitaka sana uwakilishi wa wananchi jimboni uwe na ukomo wa miaka 15 yani vipindi vitatu tu Tu dadeeeki
Matokeo ya Urais yahojiwe mahakamani, na ikithibitika palikuwa na Hila, uchaguzi urudiwe.

Pia wananchi wote wawe sawa mbele ya SHERIA, pasiwepo na KINGA ya yeyote kutoshtakiwa.

Hii itasaidia kutokomeza RUSHWA Kwa zaidi ya 50%.

Bring back Rasimu ya Warioba 💪💪💪💪💪💪
 
Tulipotoa maoni juu ya kuandika KATIBA mpya, hatukuagiza maridhiano ya nusu mkate Kwa wanasiasa.

Mkate unatakiwa kugawanywa Kwa wananchi wote Ili;

1. Wananchi tupate madawa hospitalini.

2. Wazee walipwe pension zao Kwa wakati.

3. ELIMU Ipatikane Bora.

4. Wanafunzi wapate mlo mashuleni kama enzi za mwalimu.

5. Walimu mashuleni walipwe allowance na overtime wanapofanya KAZI wakiwa majumbani mwao kama kutunga na kusahihisha mitihani.

Ni DHAMBI kubwa MKATE kugawanywa Kwa wanasiasa pekee ilhali wananchi tunakula mlo mmoja tena Kwa kubahatisha!!!!

Bring back our WARIOBA 💪💪💪.
 
Mchakato utakuwa na impact ikiwa Mzee Warioba atarudishwa kukamilisha KAZI aliyoianza.

Bring back our WARIOBA 💪💪💪
 
Wafanyabiashara wa KARIAKOO Kwa kufanya mgomo kudai mazingira Bora ya biashara zao,

Wametuma ujumbe Nchi nzima Kwa kundi kubwa la wafanyabiashara kuungana pamoja na makundi mengine kudai KATIBA mpya, Rasimu alosimamia Judge WARIOBA ndiyo njia sahihi.

Bring back our WARIOBA 💪💪💪💪
 
Prof Kabudi amekosa sifa sababu ameyumba msimamo wake ktk masuala muhimu.

Bring back our Rasimu ya Warioba.

Bring back our WARIOBA kama mkt wa Tume amalizie KAZI iliyotukuka.

Ameeen!!!!
 
ikipatikana katiba mpya me ntakuwa mbunge mtarajiwa
Ukumbuke pia ukibahatika kuwa mbunge,

KIPO kipengele kinachowapa nguvu WAPIGA kura kumpiga chini mbunge wao asipotekeleza majukumu yake.

Yaani mbunge anatenguliwa b4 mitano kukamilika.

Pia sahau kuhusu V8, Toyota mkonga inatosha kbs.
 
Hivi huu mchakato umefikia wapi? Rais Samia ni kama ANAUKWEPA HIVI, anapoteza muda tu
 
Hivi huu mchakato umefikia wapi? Rais Samia ni kama ANAUKWEPA HIVI, anapoteza muda tu
Amerudisha mpira tena kwenye kikosikazi Cha mchongo,

Tunachopigania sasa ni pesa itengwe kwenye Bunge hili la budget. Ili mchakato uanze maana wanatuhadaa kutenga budget wakati kiuhalisia hakuna pesa ajili ya mchakato wa KATIBA iliyotengwa Hadi sasa.

Ikiundwa Tume, Judge WARIOBA akarudishwa,

Rasimu yake ikirudishwa mezani tukaanzia mjadala wa maboresho hapo,

Kufikia December mwaka huu, Moshi MWEUPE utaanza kuonekana kuashiria mema.
 
Mpumzisheni mzee WA watu. Ina Maana Hakuna mtu mwenye Kuweza kuendeleza huko juu. Ina Maana kumejaaa Vilaza tu mpk mnataka kumchosha mzee WA watu. Ameshawapa RAMANI basi malizieni
 
Mpumzisheni mzee WA watu. Ina Maana Hakuna mtu mwenye Kuweza kuendeleza huko juu. Ina Maana kumejaaa Vilaza tu mpk mnataka kumchosha mzee WA watu. Ameshawapa RAMANI basi malizieni
Ulimsikia Mzee Mandela wewe?

Vp kuhusu Desmond Tutu?

Hata Mbowe na Lissu hawatopumzika Hadi wakamilishe mission.

Magufuli je? Magu ndo hata USINGIZI hakuwa anapata maana aliheshimu KAZI aliyopewa.

Angepumzika Mandela, ingekuwaje kuhusu uhuru wa SA?

Kupumzika ni kukamilisha MISSION, tilimtuma KAZI, kama hajatukabidhi KATIBA mpya, Bado hajamaliza KAZI.

Mungu amlinde Mzee wetu, WARIOBA, ampe nguvu kama za kijana mwenye 30 yrs amalizie KAZI yake.

Amen
 
Kwani wengine hawapo
Mzee WARIOBA ndiye chaguo la Watanzania, alieaminiwa kupewa KAZI iliyotukuka ya kuipatia Nchi KATIBA mpya.

Bring back our WARIOBA 💪💪💪
 
Back
Top Bottom