Siku za mbele, hapa hapa Tanzania na tena basi Afrika, tutakuwa na maendeleo makubwa katika maarifa ya nyanja na ugani wa sayansi ya umeme... Wala usihadaike na kiingereza cha Transista, rektifaya za silikoni, MOSFETI, Sakiti Vibanzi Jumuifu ndogo ama kubwa... Haya bado ni mambo ya pembezoni mwa 'ujuaji' wa mambo...
Labda bado haujaoneshwa ni namna gani hata sayansi ya umeme >
imedumazwa< kwa makusudi... Dhana za 'volti', 'ampia' na 'ukinzani' ni >
kujua mambo ya nishati ya umeme kwa sehemu<...
Maxwell Chikumbutsu wa Zimbabwe anachokisa<... Usomi wa 'kikasuku' ni ushamba taslim; ni 'mzigo'. Sisi watu wa Afrika leo hii, wengi wetu, tuna adha ya >'
Akili ya Kimaskini'<. Hii inatuacha na haiba ya kujibeza, kujikataa, kujiona hatutoshi na tumepungukiwa... Huu ni >
'udunya'< wa kujitakia... Mtu hauwi 'akilikubwa' kwa sababu unaongea, kuimba, kuzuga kama 'mzungu'; mzungu naye ni mtu, tena katika jamii ya wazungu kuna >
'wahuni' wenye ufundi wa michezo na hadaa za 'kula na vipofu'<...