Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Nguvu ya Makonda iko kwenye ujinga wake. Namaanisha kuwa ni wale watu wajinga ambao unaweza kumwambia ''nenda kamzabe mama yako yako makofi'', na akaenda kufanya kweli. Kwa kifupi nataka kusema kuwa mwenyekiti amemchagua yeye kwa sababu anajua ni mjinga na yuko tayari kujitoa ufahamu afanye lolote bila kujali madhara yake. Hivi mtu mwenye akili zako unaweza kufanya ujinga anaofanya wa kudhalilisha watu na wakati kuna kesho? Hajiulizi kama Samia kesho hayupo ni nini kitampata? Kuna watu walikuwa wanasema baada ya kufa Magufuli basi atakuwa amejifunza, lakini ukweli ni kwamba ndiyo amezidisha. Tuombe Mungu uzima uje uone mwisho wake utakavyokuwa mbaya.
Umeongea point ya maana sana, kama professor wa political science! - nguvu ya Makonda iko katika ujinga wake mwenyewe, na ujinga wa Watanzania

Makonda na Watanzania wanahitaji kuelimika. Nani atatusaidia katika hili?

Lakini nahisi bado kuna zaidi ya ujinga wa Watanzania na wa Makonda vinavyomfanya ajiamini kiasi hiki.
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
🪑🇹🇿
Iyena iyena !!
Mafisadi Chamani kama wapo wataisoma namba !!
Makonda shikilia hapo hapo 😅😅🙏🙏🔥
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Kama Ulimwelewa TPDF Kwenye Ile Kauli Yao Basi Uipeleke Na Huku 75% ya Akili Yako
 
🪑🇹🇿
Iyena iyena !!
Mafisadi Chamani kama wapo wataisoma namba !!
Makonda shikilia hapo hapo 😅😅🙏🙏🔥
Jibu lako ni signature yangu; Usimdharau mjinga, mwelimishe. La sivyo atajikusanya na wajinga wenzake na watatumia nguvu yao ya wajinga wengi kukuchagulia mbunge au hata raisi mjinga kama wao .
 
Umeongea point ya maana sana, kama professor wa political science! - nguvu ya Makonda iko katika ujinga wake mwenyewe, na ujinga wa Watanzania

Makonda na Watanzania wanahitaji kuelimika. Nani atatusaidia katika hili?

Lakini nahisi bado kuna zaidi ya ujinga wa Watanzania na wa Makonda vinavyomfanya ajiamini kiasi hiki.
Wahenga walisemaga “ there is no great genius without some touch of madness “ 😅🙏🙏
 
Anachokifanya Makonda ni kuendelea kuivua chupi serikali na chama chake.

CCM ndio wenye Dola Kwa maana ya serikali na watendaji wote wako chini ya serikali ya CCM, kushindwa kufanya kazi kwa hao wafanyakazi na kuleta matokeo ni failure ya CCM na Serikali yake.

Ujinga uliopandikizwa na CCM kwenye jamii ndio unaofanya hao watendaji na Makonda wawe salama huko barabarani, vinginevyo kwa madhara waliosababisha walipaswa kupigwa mawe kila wapitapo.
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Nakubaliana na wewe kwamba,kichwa kimezidi urefu wa mikono.Lakini naomba uwe muwazi tu,mbona Makonda wananchi wanamkubali sana,ni nini kipo nyuma ya kupendwa kwake na wananchi wa kawaida?
Ni ukweli ulio wazi kwamba ameziba pengo lililoachwa wazi na watawala,ambao kimsingi wameshinwa kabisa kutimiza wajibu wao.Aliyemtuma sina shaka yeyote kwamba analijua hili na kwa makusudi kabisa,anamtoa Makonda kafara ili afanye kazi ambayo yeye kashindwa.

Makusudi ni nini?Makusudi ni kujiweka mbali na wapigaji(kundi la wahuni),ili itakapofika 2025 aongeze nafasi yake ya kushinda uchaguzi.Kama atafanikiwa sijui,lakini Magufuli alipendwa na wananchi wa kawaida sana kwa sababu aliji-identify nao.Labda niseme wazi bila kumung'unya maneno,Makonda anapata nguvu kutoka kwa kiongozi wajuu kabisa wa nchi,Samia.
 
Unajua wewe ni mtu ninaemuona kibaraka mmoja wa kujipendekeza ambae anatafuta kila namna ya kujipendekeza kwa Samia na CCM yake angalau wakurushie ugali wa uteuzi wa namna fulani, lakini hata wao wamekudharau ndio maana hadi leo bado unahangaika na propagaganda zako na hakuna hata anaekujali.

Endelea, labda kuna siku kuna mjinga fulani atakukumbuka.

Sasa kama una akili kawaambie hao watu unaojikuwadi kwao kwamba wenye akili wanasema hivi, ziara na kujitutumua kwa Makonda hakusaidii bali kunabomoa CCM mbele ya watu wenye akili, na anasababisha migongano ndani ya chama na serikali. Kwa mfano, akimwamrisha waziri live mbele ya watu, aende mahali fulani, kumbe huyo mtu ana appointment na raisi, itakuwaje? Anamdhalilisha raisi mbele ya wateule wake, lakini hilo hamlioni nyie.

Kuna watu Makonda anawaumbua bila kuona kwamba anapofanya hivyo anamuumbua aliyewateua.

Makonda anachofanya katika ziara zake ni kuonyesha udhaifu wa serikali ya CCM katika kusimamia uongozi wa nchi na kutatua matatizo ya wananchi. NI watu semi-iliterate ambao wataona anatatua matatizo. Wewe kwa akili yako, Makonda akipita Mbeya na kusikiliza watu kumi siku hiyo, anakuwa ametatua matatizo ya wananchi wa Mbeya? Umesoma lakini wewe?

Mie ngoja nikuambie ukweli. Kinachowaangusha Chadema na kushindwa kuwaondoa CCM madarakani ni kwa sababu hadi leo Chadema hawajatambua wapiga kura wa Tanzania ni kama nilivyosema kwenye signature yangu hapa chini,

Usimdharau mjinga, mwelimishe. La sivyo atajikusanya na wajinga wenzake na watatumia nguvu yao ya wajinga wengi kukuchagulia mbunge au hata raisi mjinga kama wao .

na hii ni kutia ndani watu kama wewe Mwashambwa. Chadema wanapaswa kubadilika na kuongea na wajinga wa nchi hii katika lugha iliyo nyepesi mjinga kuelewa, kama wanavyofanya CCM, japo CCM hawafanyi kwa lengo la kuelimisha wajinga, bali kuwadumaza katika ujinga wao ili waendelee kuwa wajinga katika pindi za uchaguzi. Kuna watu tunajua hilo.
Sahihi kabisa !
 
Umeongea point ya maana sana, kama professor wa political science! - nguvu ya Makonda iko katika ujinga wake mwenyewe, na ujinga wa Watanzania

Makonda na Watanzania wanahitaji kuelimika. Nani atatusaidia katika hili?

Lakini nahisi bado kuna zaidi ya ujinga wa Watanzania na wa Makonda vinavyomfanya ajiamini kiasi hiki.
Makonda katumwa na Samia ili kulaghai watu waone kuwa kumbe raia ni kiongozi mzuri sana ila tu watu aliowachagua ndiyo wabaya. Kwa kifupi anajaribu kutenganisha failures za serikali na rais ili ionekane kwamba tuna rais mzuri sana ila wateule wake siyo wazuri. Anatumia zile technique za Magufuli baada ya kuona kuwa watu walizipenda sana. Tatizo lililojitokeza ni kwamba Samia kama rais, hana uwezo na stamina ya kuzunguka huko na huko huku akifanya ghilba za aina hiyo. Akaona njia rahisi ni kumchukuwa mjinga mjinga fulani ili amtumie kama ''mbwa''. Nakuhakikishia hiyo kazi angepewa mtu mwenye akili na busara zake, asingekubali kufanya maigizo ya kijinga namna hii. Kwanza anatengeza uadui na watu wengi sana ambao hajui kesho wanaweza kuja kuwa na vyeo na uwezo wa kumshughulikia. Samia ni binadamu, wiki ijayo anaweza asiwepo, Makonda ataweka wapi uso wake? Si watagawana nyama wamle?
 
Nakubaliana na wewe kwamba,kichwa kimezidi urefu wa mikono.Lakini naomba uwe muwazi tu,mbona Makonda wananchi wanamkubali sana,ni nini kipo nyuma ya kupendwa kwake na wananchi wa kawaida?Ni ukweli ulio wazi kwamba ameziba pengo lililoachwa wazi na watawala,ambao kimsingi wameshinwa kabisa kutimiza wajibu wao.Aliyemtuma sina shaka yeyote kwamba analijua hili na kwa makusudi kabisa,anamtoa Makonda kafara ili afanye kazi ambayo yeye kashindwa.Makusudi ni nini?Makusudi ni kujiweka mbali na wapigaji(kundi la wahuni),ili itakapofika 2025 aongeze nafasi yake ya kushinda uchaguzi.Kama atafanikiwa sijui,lakini Magufuli alipendwa na wananchi wa kawaida sana kwa sababu aliji-identify nao.Labda niseme wazi bila kumung'unya maneno,Makonda anapata nguvu kutoka kwa kiongozi wajuu kabisa wa nchi,Samia.
Hakika Umenena !
Hapo ile kambi mbaya inayotaka kuleta kauzibe itakuwa imeshaufyata !
Everything is happening for a reason !!
 
Hiyo Nguvu Imeonekana Wazi Wazi Ila Ndiyo Itakayokipasua Chama Vipande Viwili
Kwasasa Wote Wapo Kimya Ila Wanangoja 2025 Ndiyo Watatoa Kucha Zot
Kugombea Fito Za Nafasi Ya Rais Wa JMT, Subirini Muda Utaongea Yote
Mnayoyajua /Msiyoyajua Yatawekwa Hadharani Na Mtashangaa Sana
 
Inawezekana. Mara nyingine naamini walokole wanatumia nguvu fulani zilizojificha kufanya mambo yao! Lakini chama chenye mchanganyiko wa dini mbalimbali, haikiwezi kudumu kwa kuendeshwa na nguvu za kilokole!
Nani mlokole??
 
Back
Top Bottom