Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Naamini kwa dhati kabisa nguvu ya Makonda haitokani na kuwa kwake katibu mwenezi wa CCM, lazima kuna chanzo kingine kinampa kujiamini kiasi hiki

Si Wapendi CCM, Simkubari Makonda kwa historia yake...!

Ila nakubaliana na anachokifanya, tena nilitamani angepata nafasi ya juu zaidi....!

Kama anaweza kuwafikia Wananchi na kuwasikiliza, hilo binafsi ni Muhimu sana, sisi hohehahe ndo tunataka, mtu atusikilize, pale tunapofukuzwa kwenye office za Umma, pale tunapoambiwa kama hujatoa kitu kidogo, kiwanja chako kinaenda kupotea, halafu anakuja mtu ananambia nieleze matatizo yako ntakusaidia, sisi tutampenda huyo....!

Kama nafasi yake haitambuliki kikatiba, hiyo sisi sio juu yetu, kama yeye sio kitu mbele ya Waziri ki cheo ama mbele ya Katibu Mkuu, hilo sisi hatujari, sisi tunajua kuna mtu ana nafasi huko CCM, anapita nchi nzima kujaribu kutatua changamoto zetu masikini...!

Hata kama kwa namna yoyote mkamwondoa, tutaendelea kuomba siku moja aje apatikane kiongozi kama yeye ambaye atatusikiliza...!

Kama anavunja Sheria hiyo sisi haituhusu, coz hata wanaofata sheria hawataki kutusikiliza...!

Makonda wewe ni Wapoti wangu, japo mimi sikukubari wewe kwa historia yako.... Ila piga kazi hivyo hivyo, mradi kuna Masikini wenzangu wanasaidika....!!!!
Ataweza kuwafikia na kutatua matatizo ya masikini wangapi? Nchi ina watu >60 million. Halafu, atatatua matatizo kwa kutumia watendaji hao hao “walioshindwa kazi” kwenye mfumo rasmi chini ya uongozi wa CCM? Halafu pia kwa gharama gani? Misafara yote hiyo?

Au ni kuwapa faraja ya kisaikolojia tu kama ile wanayotoa waganga wa kienyeji, mitume na manabii baada ya mifumo rasmi kushindwa kuwaponya/kuwafanikisha kama ilivyotarajiwa?

Kwa kweli huwa nastaajabu sana kuona kumbe kweli kuna watu wengi nchini wanaoamini kuwa kiongozi bora ni yule ambaye muda mwingi anazunguka kusikiliza matatizo ya mtu mmoja mmoja kwenye mikutano ya hadhara kisha kuagiza kupitia media watendaji husika wayatatue! Ukiondoa shere iliyomo katika hilo tukio-kituko, sijui Watanzania wangapi wanajiuliza gharama za hiyo misafara, tija yake, na hasara inayopatikana kwenye uchumi hasa ukifikiria suala la opportunity cost. Yaani yote hiyo ni ili kuwazuga na kuwapa faraja “wajinga”! Very sad!

Yaani kama vile hatukwenda shule wala kuelimika? Hatujui kabisa serikali ni kitu gani na inatakiwa kufanya kazi vipi? Kweli tunahitaji hizi exorbitant charades za kina Makonda?
 
Haya ni mawazo ya watu wasio na upeo kwenye mambo ya uongozi wa nchi, wanaodhani kuwa nchi inaongozwa kama kijiji. Hivi huoni kuwa tatizo la Tanzania ni rais na wateule wake wote akiwemo huyo Makonda? Makonda atawasikiliza wangapi? Kwa nini usililie mfumo ambao matatizo yatatuliwa kuanzia ngazi za chini na hayasubiri mtu mmoja anayezunguka? Kweli kukosa akili ni hatari sana.
Hio mifumo tayari ipo,
Ila wenye dhamana hawawajibiki positively!
Anatakiwa mtu anayewateua awe imara kuwasimamia Basi!
 
Umeongea point ya maana sana, kama professor wa political science! - nguvu ya Makonda iko katika ujinga wake mwenyewe, na ujinga wa Watanzania

Makonda na Watanzania wanahitaji kuelimika. Nani atatusaidia katika hili?

Lakini nahisi bado kuna zaidi ya ujinga wa Watanzania na wa Makonda vinavyomfanya ajiamini kiasi hiki.
Ninyi ndio wajinga lakini watanzania siyo wajinga . Watanzania wanatambua kazi njema na yakutuka inayofanywa na Mheshimiwa Makonda katika kuwatetea na kuwasemea watanzania.watanzania wanaona namna ziara za Mheshimiwa Makonda zilivyochochea uwajibikaji kwa viongozi mbalimbali waliokuwa wanafanya kazi kwa mazoea na kukaa maofisini tu bila kutoka kwenda kuwasikiliza wananchi.

Hata hivyo napenda kukwambia kuwa kaa ukijiandaa maana huyo ipo siku moja utamtizama kupitia Tv akiapishwa kuwa Rais wa Tanzania.
 
Ataweza kuwafikia na kutatua matatizo ya masikini wangapi? Nchi ina watu >60 million. Halafu, atatatua matatizo kwa kutumia watendaji hao hao “walioshindwa kazi” kwenye mfumo rasmi chini ya uongozi wa CCM? Halafu pia kwa gharama gani? Misafara yote hiyo?

Au ni kuwapa faraja ya kisaikolojia tu kama ile wanayotoa waganga wa kienyeji, mitume na manabii baada ya mifumo rasmi kushindwa kuwaponya/kuwafanikisha kama ilivyotarajiwa?

Kwa kweli huwa nastaajabu sana kuona kumbe kweli kuna watu wengi nchini wanaoamini kuwa kiongozi bora ni yule ambaye muda mwingi anazunguka kusikiliza matatizo ya mtu mmoja mmoja kwenye mikutano ya hadhara kisha kuagiza kupitia media watendaji husika wayatatue! Ukiondoa shere iliyomo katika hilo tukio-kituko, sijui Watanzania wangapi wanajiuliza gharama za hiyo misafara, tija yake, na hasara inayopatikana kwenye uchumi hasa ukifikiria suala la opportunity cost. Yaani yote hiyo ni ili kuwazuga na kuwapa faraja “wajinga”! Very sad!

Yaani kama vile hatukwenda shule wala kuelimika? Hatujui kabisa serikali ni kitu gani na inatakiwa kufanya kazi vipi? Kweli tunahitaji hizi exorbitant charades za kina Makonda?
Bila shaka wewe ni wala viongozi wavivu,wazembe na waliokuwa wanafanya kazi kwa mazoea.ndio maana unatetea ujinga wa baadhi ya viongozi na watumishi wa umma kufanya ufisadi katika ofisi za umma,kudhulumu wananchi haki zao.kufanya hujuma na kila aina ya uozo.watanzania ambao ndio wenye nchi wataet kumuunga mkono Mheshimiwa Makonda kwa kazi kubwa anayoifanya na pia watanzania wataendelea kuwapiga vita na kuwapuuza watu aina yako na wenye mawazo finyu kama wewe.
 
Niite jina lolote, lakini mimi ni mojawapo ya watu ambao huwezi hata kabisa kunishawishi kwamba hii nguvu na mbwembwe ambazo Makonda amekuwa akizionyesha zinatokana na kuwa kwake na cheo cha katibu mwenezi wa CCM. Tusidanganyane hapa.

Makonda sio katibu mwenezi wa kwanza CCM, na wamekuwapo wengine huko nyuma, lakini ni mara ya kwanza tunapata katibu mwenezi wa CCM ambae anaonyesha kujiamini kupita mamlaka yanayostahili ya katibu mwenezi wa CCM.

Leo hii katibu mwenezi awapigie simu mawaziri, amkebehi mwanasheria mkuu wa serikali, awaamrishe wakuu wa mikoa, ma-RPC, eti kwa sababu yeye ndie msemaji mkuu wa chama, hilo tu? Haiwezekani.

Leo hii katibu mwenyezi apewe bajeti, misafara ya magari, kuliko inavyokuwa kwa makamu mwenyekiti wa CCM au katibu mkuu wa CCM, kwa sababu gani? Kwamba katiba ya CCM imebadilishwa kisiri na hawa wote wameambiwa kuanzia sasa bosi wenu ni katibu mwenezi wa CCM? Pamoja na mawaziri? Wakuu wa mikoa? Mwanasheria Mkuu? Wenyeviti wa CCM wa mikoa?

Sote tunajua msemaji mkuu wa chama chochote anasema yale chama kilichoamua katika vikao vyake rasmi. Kuwa msemaji wa chama haina maana wewe ndio unakuwa unakisemea chama, hata siku moja. Kuwa katibu mwenyezi sio katika mpangilio wa vyeo vya chama, ni nafasi tu. Huwezi hata kusema katibu mwenezi wa CCM ni mkubwa kuliko mwenyekiti wa CCM wa mkoa. Lakini sio hivyo kwa Makonda. Yeye amejipa madaraka ambayo nadhani yanazidi hata ya kuwa makamu mwenyekiti wa CCM, au katibu mkuu wa CCM. Kujiamini huko kunatoka wapi? Mamlaka haya yanatoka wapi? Kwamba siku zote hatukujua kuwa katibu mwenezi wa chama ni mtu mkubwa namna hii? Ni kweli?

Nyie watu wa CCM, nyie mawaziri, nyie wakuu wa mikoa, tuambieni ukweli. Kinachowafanya muufyate Makonda akiunguruma ni nini hasa, Ukatibu mwenezi wa CCM? Na kwa nini sasa wenye akili tukiwauliza mbona mambo yako hivi, mnaishia kutabasamu tu bila kusema lolote? Kuna kitu gani msichotuambia?

Na niwaambie wazi nyie watu wa CCM. Kama nguvu ya Makonda sio ya kikatiba ndani ya CCM, kama kuna chanzo kingine kisicho rasmi kinampa nguvu na kujiamini kiasi hiki, basi anguko la CCM liko karibu sana!
Mawazo huru!

Dola itakua imemwambia mama hatoshi,Kuna mtu anahitajika afanye kazi yako ,mtu kivuli,yaani Raise kiutendaji lakini sio kikatiba!!

Ndio makonda akaonekana anafaa na yeye ndio ana sauti nani apite au akatwe hapo 2025!!

Makonda ni Raid kivuli kabla hajawa Rais rasmi!

Source:- trust me broo!
 
Makonda katumwa na Samia ili kulaghai watu waone kuwa kumbe raia ni kiongozi mzuri sana ila tu watu aliowachagua ndiyo wabaya. Kwa kifupi anajaribu kutenganisha failures za serikali na rais ili ionekane kwamba tuna rais mzuri sana ila wateule wake siyo wazuri. Anatumia zile technique za Magufuli baada ya kuona kuwa watu walizipenda sana. Tatizo lililojitokeza ni kwamba Samia kama rais, hana uwezo na stamina ya kuzunguka huko na huko huku akifanya ghilba za aina hiyo. Akaona njia rahisi ni kumchukuwa mjinga mjinga fulani ili amtumie kama ''mbwa''. Nakuhakikishia hiyo kazi angepewa mtu mwenye akili na busara zake, asingekubali kufanya maigizo ya kijinga namna hii. Kwanza anatengeza uadui na watu wengi sana ambao hajui kesho wanaweza kuja kuwa na vyeo na uwezo wa kumshughulikia. Samia ni binadamu, wiki ijayo anaweza asiwepo, Makonda ataweka wapi uso wake? Si watagawana nyama wamle?
Acha ujinga wako wa kiwango cha juu.yaani wewe ni mtu wa hovyoo sana ,sijuwi hata kama unajielewa. Kwa hiyo Mheshimiwa Makonda ashindwe na aogope kufanya kazi kwa weledi na kuwabana wezi,wala rushwa ,wazembe kazini na mafisadi eti kwa kuogopa kwamba kesho watakuwa ni viongozi? Kwa hiyo wewe kwako cheo ni muhimu sana kuliko maisha ya mama ya watanzania? Kwako cheo kinacholihakikishia shibe tumbo lako mwenyewe ndio furaha kwako kuliko mateso ya wananchi wanaodhulumiwa haki zao na kunyanyaswa?

Huu ujinga mnauandika na kuwaza mkiwa mmelewa? Umeandika huu ujinga ukiwa mgonjwa au mzima? Kwa hiyo wewe unataka watumishi wazembe na wasiotimiza majukumu yao wachekewe tu kwa kuogopa kukosana nao? Kwanini unamawazo ya kijinga kiasi hiki? Wewe hufai hata kuongoza familia yako maana mawazo yako ni mfu na hujitambui kabisa. Halafu ukome kutukana viongozi wetu.
 
Hiyo Nguvu Imeonekana Wazi Wazi Ila Ndiyo Itakayokipasua Chama Vipande Viwili
Kwasasa Wote Wapo Kimya Ila Wanangoja 2025 Ndiyo Watatoa Kucha Zot
Kugombea Fito Za Nafasi Ya Rais Wa JMT, Subirini Muda Utaongea Yote
Mnayoyajua /Msiyoyajua Yatawekwa Hadharani Na Mtashangaa Sana
Acha kujidanganya wewe. Fomu ya urais ndani ya CCM Ni moja tu kwa ajili ya Rais Samia.
 
Inawezekana. Mara nyingine naamini walokole wanatumia nguvu fulani zilizojificha kufanya mambo yao! Lakini chama chenye mchanganyiko wa dini mbalimbali, haikiwezi kudumu kwa kuendeshwa na nguvu za kilokole!
hakuna kitu kiitwacho "nguvu za kilokole". Kuna nguvu za Mungu Aliye hai, Yehova.

KWA BWANA YESU KILA GOTI LITAPIGWA!
 
Hio mifumo tayari ipo,
Ila wenye dhamana hawawajibiki positively!
Anatakiwa mtu anayewateua awe imara kuwasimamia Basi!
Mifumo ipo lakini haiendani na uhalisia. It is a top bottom approach, and the president acts as a micro-chip, which controls everything! Inatakiwa wananchi wawe ndiyo wanaochagua na kuwajibisha viongozi wao wa karibu. Haya mambo ya rais kuteua na kuwapelekea wananchi viongozi haufanyi kazi na ndicho kinachotokea sasa.
 
Nguvu ya Makonda iko kwenye ujinga wake. Namaanisha kuwa ni wale watu wajinga ambao unaweza kumwambia ''nenda kamzabe mama yako yako makofi'', na akaenda kufanya kweli. Kwa kifupi nataka kusema kuwa mwenyekiti amemchagua yeye kwa sababu anajua ni mjinga na yuko tayari kujitoa ufahamu afanye lolote bila kujali madhara yake. Hivi mtu mwenye akili zako unaweza kufanya ujinga anaofanya wa kudhalilisha watu na wakati kuna kesho? Hajiulizi kama Samia kesho hayupo ni nini kitampata? Kuna watu walikuwa wanasema baada ya kufa Magufuli basi atakuwa amejifunza, lakini ukweli ni kwamba ndiyo amezidisha. Tuombe Mungu uzima uje uone mwisho wake utakavyokuwa mbaya.
Kwa wewe unayetegemea watu ill maisha yako yaende kulamba makalio sawa! Makonda anamtegemea Mungu!
 
We umeingia chaka. Kuna nani mwenye nguvu nchi hii zaidi ya Rais? Msitafute namna ya kukweza hilo kabila lenu la kishamba. Yule mtu wenu aliyewakweza ameshatutoka au hamuamini bado?
Mtu ajikweze halafu ajiite muuaji akili huna wasukuma ndo hawataki hiyo comment
 
Mleta mada ni mtu asiejua chochote kuhusu nafasi za kiuongozi ndani ya ccm,yaani umesema mwenyekiti wa ccm mkoa ni mkubwa kuliko katibu wa Nec,itikadi,mafunzo na uenezi?,
 
Back
Top Bottom