Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 5,122
- 5,104
Ataweza kuwafikia na kutatua matatizo ya masikini wangapi? Nchi ina watu >60 million. Halafu, atatatua matatizo kwa kutumia watendaji hao hao “walioshindwa kazi” kwenye mfumo rasmi chini ya uongozi wa CCM? Halafu pia kwa gharama gani? Misafara yote hiyo?Si Wapendi CCM, Simkubari Makonda kwa historia yake...!
Ila nakubaliana na anachokifanya, tena nilitamani angepata nafasi ya juu zaidi....!
Kama anaweza kuwafikia Wananchi na kuwasikiliza, hilo binafsi ni Muhimu sana, sisi hohehahe ndo tunataka, mtu atusikilize, pale tunapofukuzwa kwenye office za Umma, pale tunapoambiwa kama hujatoa kitu kidogo, kiwanja chako kinaenda kupotea, halafu anakuja mtu ananambia nieleze matatizo yako ntakusaidia, sisi tutampenda huyo....!
Kama nafasi yake haitambuliki kikatiba, hiyo sisi sio juu yetu, kama yeye sio kitu mbele ya Waziri ki cheo ama mbele ya Katibu Mkuu, hilo sisi hatujari, sisi tunajua kuna mtu ana nafasi huko CCM, anapita nchi nzima kujaribu kutatua changamoto zetu masikini...!
Hata kama kwa namna yoyote mkamwondoa, tutaendelea kuomba siku moja aje apatikane kiongozi kama yeye ambaye atatusikiliza...!
Kama anavunja Sheria hiyo sisi haituhusu, coz hata wanaofata sheria hawataki kutusikiliza...!
Makonda wewe ni Wapoti wangu, japo mimi sikukubari wewe kwa historia yako.... Ila piga kazi hivyo hivyo, mradi kuna Masikini wenzangu wanasaidika....!!!!
Au ni kuwapa faraja ya kisaikolojia tu kama ile wanayotoa waganga wa kienyeji, mitume na manabii baada ya mifumo rasmi kushindwa kuwaponya/kuwafanikisha kama ilivyotarajiwa?
Kwa kweli huwa nastaajabu sana kuona kumbe kweli kuna watu wengi nchini wanaoamini kuwa kiongozi bora ni yule ambaye muda mwingi anazunguka kusikiliza matatizo ya mtu mmoja mmoja kwenye mikutano ya hadhara kisha kuagiza kupitia media watendaji husika wayatatue! Ukiondoa shere iliyomo katika hilo tukio-kituko, sijui Watanzania wangapi wanajiuliza gharama za hiyo misafara, tija yake, na hasara inayopatikana kwenye uchumi hasa ukifikiria suala la opportunity cost. Yaani yote hiyo ni ili kuwazuga na kuwapa faraja “wajinga”! Very sad!
Yaani kama vile hatukwenda shule wala kuelimika? Hatujui kabisa serikali ni kitu gani na inatakiwa kufanya kazi vipi? Kweli tunahitaji hizi exorbitant charades za kina Makonda?