Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Kila Imani inamungu wao waliijitengenezea wenyewe

Lakini waumini wote wa hizo Imani ambao ni binaadam Mungu wao ni mmoja tu ambae ndio aliyewaumba wao , na vyakula vyao wanavyokula na hi Dunia wanayoishi

Jibu ni kwamba Mungu ni mmoja tu ila Kuna watu wengine hawamjui huyo Mungu wao ambaye ni mmoja tu

Na hawamjui Kwa sababu hawataki kumjua Kwa sababu Mungu alishaa jifunua kupitia manabii na vitabu
Ni kweli, kila dini ina mungu wake kabisa
 
hahahahah! Ukisema zinabadilika unamuondolea mungu hiyo sifa ya kujua kila kitu. Au hauamini kama kweli anajua kila kitu?
Kwani wewe ukitaka kwenda posta kupitia Morogoro road baadae ukajua kumbe Ali Hassan Mwinyi road hakuna foleni ukaamua kupitia huko, inakuondolea kupajua posta? au kuijua Morogoro road

Samahani kama sio mwenyeji dar kwa huu mfano, utambia niikupe mwingine kama hujaelewa
 
Hapendi mabaya sio wanaofanya mabaya ndio maana tukitubu tunaamini tunasamehewa angekua hatupendi asingetusamehe na asingepatikana asiye na mabaya sababu hatuna ukamilifu ndio maana tumepewa nafasi ya kujutia mabaya na kutubu.
Hayo mabaya kama hayapendi yeye si Mungu muweza wa vyote, Alishindwaje Kuto kuumba Dunia isiyo na mabaya??

Mabaya ambayo humsababisha mwanadamu ayafanye...
 
Kwani wewe ukitaka kwenda posta kupitia Morogoro road baadae ukajua kumbe Ali Hassan Mwinyi road hakuna foleni ukaamua kupitia huko, inakuondolea kupajua posta? au kuijua Morogoro road

Samahani kama sio mwenyeji dar kwa huu mfano, utambia niikupe mwingine kama hujaelewa
mimi nipo mwanza but i've got your point. Mkuu naongelea hatima ya mtu either jehanamu au peponi na kwa mfano wako umeongelea kupajua tu kwa majina na sio kufika au kupapitia


Kumbuka mungu ndio muumba sio tupo under him kabla hajakuumba anajua wewe ni wa jehanamu tu so huwezi change na ikitokea yeye alijua kuwa ni wa jehanamu ila ulipozaliwa ukatumia maombi kama ulivyodai ukaenda peponi hapo tunaiterm kama alikuwa hajui maana yeye kabla haujazaliwa alijua wewe ni wa jehanamu but umebadilisha ukawa wa peponi kwa maamuzi yako but something that's impossible


Hauwezi kuchange hatima anayoijua mungu since he is your designer you can never go beyond his expectations buddy!
 
Okay, swali langu ni hili.... Mtu pamoja na designed systems zote zilizopo kwenye mwili wake kwa ufahamu wako, zina Designer au hazina?
Kwanza unajuaje kwamba uliumbwa?

Kwa nini unadhani uliumbwa na kitu usicho kifahamu na hukijui?

Ukisema designer aliye kuumba wewe yupo ina maana unamjua ulishawahi kumuona.

Lakini hujui kama kweli yupo ila ni imani za watu tu, kwamba yupo.Pia hata kusema hayupo ni sahihi kwa vile ukitaka kudhibitisha ali kuumba huwezi unabaki kukisia.
 
Mi naona adhabu ziko wazi ivo ni maamuzi yako kuchagua ukosee au ufanye yanayompendeza sababu ukifanya mazuri kuna zawadi na ukifanya mabaya kuna adhabu. Na pia kuna option ya kutubu sababu hakuna mkamilifu ila yeye tu.

So it's your choice and you must pay the price for your selection
Lakini hamna kitu ambacho binadamu atafanya kinachostahili kuungua milele. Hii adhabu imewekwa na dini ili kuendesha watu. Hazikuwepo katika agano la kale. Ndo maana wanajua kwa hii adhabu wote mtakubali kuendeshwa na wanaosema dini imewafata wao
 
Kina nani wanasema upinde wa mvua ni msamaha wa Mungu,... Na kina nani wanasema mvua inamwagika kutoka madirisha ya Mbinguni?
Ukisoma Sayansi juu juu utasema hakuna Mungu Muumbaji..., Lakini ukiiingia deep zaidi Utajua kuna Mungu Muumbaji. View attachment 2603884
Ndo maana ninakuambia husomi Biblia. Soma story ya Nuhu afu utaona hivi vitu. Wakristo wengi wanakubali dini Yao ya ukweli wakati hawajawahi soma Biblia kiundani. Ni sawa na kusaini mkataba bila kuusoma.
 
mimi nipo mwanza but i've got your point. Mkuu naongelea hatima ya mtu either jehanamu au peponi na kwa mfano wako umeongelea kupajua tu kwa majina na sio kufika au kupapitia


Kumbuka mungu ndio muumba sio tupo under him kabla hajakuumba anajua wewe ni wa jehanamu tu so huwezi change na ikitokea yeye alijua kuwa ni wa jehanamu ila ulipozaliwa ukatumia maombi kama ulivyodai ukaenda peponi hapo tunaiterm kama alikuwa hajui maana yeye kabla haujazaliwa alijua wewe ni wa jehanamu but umebadilisha ukawa wa peponi kwa maamuzi yako but something that's impossible


Hauwezi kuchange hatima anayoijua mungu since he is your designer you can never go beyond his expectations buddy!
Bro. Hii paradox inaitwa paradox of omniscient na freewill. Huwezi sema Mungu anajua kila kitu afu at the same time ukasema binadamu wanamaamuzi.
 
Lakini hamna kitu ambacho binadamu atafanya kinachostahili kuungua milele. Hii adhabu imewekwa na dini ili kuendesha watu. Hazikuwepo katika agano la kale. Ndo maana wanajua kwa hii adhabu wote mtakubali kuendeshwa na wanaosema dini imewafata wao
siamini pia kama kweli kuna huo moto wa milele
 
Bro. Hii paradox inaitwa paradox of omniscient na freewill. Huwezi sema Mungu anajua kila kitu afu at the same time ukasema binadamu wanamaamuzi.
sijasema kuwa binadamu wana maamuzi binadamu hatuna maamuzi ila ni kwa maelezo ya jamaa anayedai kuwa mtu anaweza kuichange kwa kuomba

ila point yangu ni kuwa hatma ambayo mungu anaijua juu ya mtu ni hiyo hiyo mwanadamu hawezi kuichange
 
Hizi sheria, ni Designer Mkuu wa Universe ndo ameziweka, Kwa wanadamu ndo maana kwa Kila dini unaona sheria za maadili zinafanana maana Kila mtu amewekewa utashi wa kujua jema na mabaya.
Kuna kitu ukifanya unahisi msuto Fulani hivi ila ukizidi kufanya na kurudia ile aibu inakutoka sasa ile aibu ndo Muumba ameweka.
Designer yupi sasa mkuu?????? Mbona sheria za dini hazifanani.Sheria za Allah ni tofauti na sheria za Yehova na ni tofauti na sheria za Mbakaso
 
Binafisi siamini katika habari za moto wa milele kwamba kuna sehemu roho za binadamu zitachomwa milele.

Hizi habari za mbinguni na motoni ni aina ya reward and punishment system iliyowekwa ili kuleta hofu na kuweza kutawala watu kwa njia nyepesi. Kwamba ukifanya kama tunavyotaka utazawadiwa na ukifanya kinyume basi utaadhibiwa.

Na ili kukamata watu zaidi wakamtengeneza mungu wa kufikirika na kusema yeye ndio mwazilishi wa hayo yote, na kulazisha watu wamuani huyo mungu na kumuacha Mungu wa kweli.

Kwa kifupi Mungu hayupo kama wanavyo muelezea kwenye vitabu vingi vya kiimani.

Kuna mtu aliwahi kuniambia njia nzuri ya kujifunza mambo ya kiimani ni through experience, achana na mambo ya kusoma rundo la vitabu ambavyo vimeyumbishwa na wanadamu kwa maslai binafsi.
 
Kila Imani inamungu wao waliijitengenezea wenyewe

Lakini waumini wote wa hizo Imani ambao ni binaadam Mungu wao ni mmoja tu ambae ndio aliyewaumba wao , na vyakula vyao wanavyokula na hi Dunia wanayoishi

Jibu ni kwamba Mungu ni mmoja tu ila Kuna watu wengine hawamjui huyo Mungu wao ambaye ni mmoja tu

Na hawamjui Kwa sababu hawataki kumjua Kwa sababu Mungu alishaa jifunua kupitia manabii na vitabu
MUNGU YUPI SASA??????MUNGU WA WAARABU AU MUNGU WA WAYAHUDI AU MUNGU WA WABANTU????????NA VITABU VIPI SASA??????VITABU VYA WAARABU AU WAYAHUDI AU WAHINDU AU WABUDHA????
 
Binafisi siamini katika habari za moto wa milele kwamba kuna sehemu roho za binadamu zitachomwa milele.

Hizi habari za mbinguni na motoni ni aina ya reward and punishment system iliyowekwa ili kuleta hofu na kuweza kutawala watu kwa njia nyepesi. Kwamba ukifanya kama tunavyotaka utazawadiwa na ukifanya kinyume basi utaadhibiwa.

Na ili kukamata watu zaidi wakamtengeneza mungu wa kufikirika na kusema yeye ndio mwazilishi wa hayo yote, na kulazisha watu wamuani huyo mungu na kumuacha Mungu wa kweli.

Kwa kifupi Mungu hayupo kama wanavyo muelezea kwenye vitabu vingi vya kiimani.

Kuna mtu aliwahi kuniambia njia nzuri ya kujifunza mambo ya kiimani ni through experience, achana na mambo ya kusoma rundo la vitabu ambavyo vimeyumbishwa na wanadamu kwa maslai binafsi.
umenena vyema brother!

These stories were just created in the mindsets of ancient people but in real situation they do not exist.
 
Nafikiri kuna baadhi ya biblia za lugha zingine zina vitabu zaidi ya 66,

SIna reference ya kwenye Biblia lakini tufanye tu mfano wa kibinadamu.

Kama Adam angeumbwa akiwa na option ya utii pekee bila kuwekewa option ya uovu pembeni basi huyo Adam angekuwa mkamilifu/timilifu sana.

Pia angekuwa hasinzii,hachoki,hahisi njaa n.k
Tunarudi palepale wewe na adam ni mfano kwa nini unataka ukamilifu usio wako... utashi wako ndio ukamilifu wako... kutenda makosa na kulazishwa kukili na kuomba msamaha kwa maelekezo ya aliyekuumba, kudhibitiwa ukikaidi au kumiminiwa baraka ikimpendeza aliyekuumba ndio ukamilifu wako.. unadai ukamilifu upi ili iweje kwa manufaa ya nani? Anaekumiliki anataka uwe hivyo we unakuja na tuakili twako twa kibinadamu kumpangia almight? Kweli?

Ukijifanya janja janja unakula burn, we mwenyewe Mello akiamua kwa utaratibu wake anakupa ban ya kipindi atakacho na hauna la kumfanya zaidi ya kulalama... unampangia Modurator utaweza kweli? Ukiona unaonewa sana ungana na wasio mwamini Almight uwe na amani moyoni hahahaha. Wapo wakina kilanga and alike.
 
MUNGU YUPI SASA??????MUNGU WA WAARABU AU MUNGU WA WAYAHUDI AU MUNGU WA WABANTU????????NA VITABU VIPI SASA??????VITABU VYA WAARABU AU WAYAHUDI AU WAHINDU AU WABUDHA????
Waarabu, wazungu, Wayahudi na wabantu wote Mungu wao ni mmoja ndio aliyewaumba

Shida ni kwamba Kuna watu miongoni mwa hao hawamjui Mungu wao aliyewaumba
 
Binafisi siamini katika habari za moto wa milele kwamba kuna sehemu roho za binadamu zitachomwa milele.

Hizi habari za mbinguni na motoni ni aina ya reward and punishment system iliyowekwa ili kuleta hofu na kuweza kutawala watu kwa njia nyepesi. Kwamba ukifanya kama tunavyotaka utazawadiwa na ukifanya kinyume basi utaadhibiwa.

Na ili kukamata watu zaidi wakamtengeneza mungu wa kufikirika na kusema yeye ndio mwazilishi wa hayo yote, na kulazisha watu wamuani huyo mungu na kumuacha Mungu wa kweli.

Kwa kifupi Mungu hayupo kama wanavyo muelezea kwenye vitabu vingi vya kiimani.

Kuna mtu aliwahi kuniambia njia nzuri ya kujifunza mambo ya kiimani ni through experience, achana na mambo ya kusoma rundo la vitabu ambavyo vimeyumbishwa na wanadamu kwa maslai binafsi.
Ni maoni yako
Kwasababu ni miungu tofauti, mmoja wapo ndo wa ukweli, .
Kila mwamba ngoma huvutia kwake
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
I bore down and worship my GOD - JEHOVA... kila sekunde na kila saa.. Matendo yake ni ya Ajaabu....
1. Kila mwenye Pumzi na Amsifu BWANA ( Zaburi 150:6)
 
Back
Top Bottom