Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Naamini Mungu yupo ila nashindwa kuuelewa ukamilifu wake, labda muendelee kunifunza

Waarabu, wazungu, Wayahudi na wabantu wote Mungu wao ni mmoja ndio aliyewaumba

Shida ni kwamba Kuna watu miongoni mwa hao hawamjui Mungu wao aliyewaumba
Mungu yupi sasa ?????Mbona wana dini tofauti na kila dini ina mungi mwenye utaratibu wa tofauti na mwingine???
 
Tunarudi palepale wewe na adam ni mfano kwa nini unataka ukamilifu usio wako... hapo na utashi wako ndio ukamilifu wako... kutenda makosa na kulazishwa kukili na kuomba msamaha, kudhibiwa ukikaidi au kumiminiwa baraka ikimpendeza aliyekuumba ndio ukamilifu wako.. unadai ukamilifu upi ili iweje kwa manufaa ya nani?
Ukamilifu ambao mimi nilikuwa nauungumzia ni wa Mungu.

Mungu kaumba viumbe ambao badae walikuja kumuasi, that means kulikuwa na kasoeo
Sasa kwa nini hapendi wanaofanya mabaya?

Na uwezo wa kuyaondoa hayo mabaya alikua nao,

Utambuzi wa sisi kujua mema na mabaya ni dhahiri kwamba Mungu alipanga tufanye yote mema na mabaya.

Kama hapendi sisi tufanye mabaya asinge tupa utambuzi na ufahamu wa kutenda mabaya.

Labda useme kwamba anapenda mema na mabaya..
Kwa muktadha wa Biblia ni kana kwamba "Mungu alimuumba mwanadamu na kumpa ufahamu wa kujua mema tu" ila shetani ndiye akamwonesha mwanadamu ubaya mwa kumshawishi ale lile tunda
 
Ingawa Daudi alitimiza mambo mengi, alikuwa mnyenyekevu. Aliimba hivi kumhusu YEHOVA: “Ninapoziona mbingu zako, kazi za vidole vyako, mwezi na nyota ambazo umetayarisha, mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba umweke akilini, na mwana wa mtu wa udongo hivi kwamba umtunze?” (Zaburi 8:3, 4)
 
Hakuna imani bila dini na hakuna dini bila imani....Lazima ujue definition ya neno imani na definition ya neno dini
Imani ndo huanza.
Kwani Abrahamu alikuwa na dini?
Alikuwa na Imani Wala sio dini, mara ngapi Abraham aliwadanganya Abimeleki na Farao kuwa Sara ni dada yake Ili asiuwawe?
MBONA alimuingilia Hagai bila ya kumuoa?
 
We ni shahidi ?
MAJINA YA MUNGU NA MAANA ZAKE
♢GOD'S NAMES WITH THEIR MEANING

1. ADONAI
=> Mungu Mwenye enzi yote,kimbilio imara Mwa 15:2‐8, Kut 6:2‐3
God of sovereign,strong refuge
2. EL-ELYON
=> Mungu Aliye juu zaidi ‐Mwa14:18, Dan 4:34
Most high God Psa 21:7
3. EL‐GIBBOR
=> Mungu Mwenye Nguvu Isa 9:6, Zab 147:5
(Mighty God )
4.El GMULOT -
=>Mungu alipaye/atoaye ujira
The God of recompense Jer 51:56
5. EL- HAI
-Mungu Aliye Hai/Anaishi ‐Josh 3:10, 1Sam17:26
Living God
6. EL-OHEENU
. =>Bwana Mungu wetu Zab 99:5,8,9
Lord our God Psa 99:5,89
7.EL-OHIM
=> Mungu Muumbaji /Muumbaji wa milele ‐ Mwa33:20, Kol 1:16‐17
8.ELOHIM YISRAEL
=> Mimi ni Bwana Mungu wako
. Iam the lord your God Lev 18:2
9. EL-OLAM
=> Mungu wa Milele ‐ Ufu4:8, Kut 3:14 Mwa 21:23
Everlasting God/Eternal God [ olam means age ]
10. EL-ROI
=> Mungu Aonaye kila kitu ‐Mith 15:3, Zab 32:8
=> BWANA Mchungaji wangu Zab 23:1
The God of sight, The God who keeps watch Gen 16:13
11. EL-SHADDAI
Mungu Mtoshelezi ‐Mdo 17:28, Kumb 8:4
12. JEHOVA EL-ASHIYB
The lord my restorer
Bwana ni mrejeshaji wangu
13.JEHOVAH EL-EMUMAH -
Mungu mwaminifu
Faithful God
14.JEHOVAH EL-GEMU 'AH -
Mungu alipaye/atoaye ujira
The God of recompense Jer 51:56
15.JEHOVAH EL-MAGOWR -
Bwana ni Chemchemi ya maji hair
The fountain of living water Jer 2:13
16. JEHOVAH JIREH/YIR 'EH = (YEHOVA YIRE )
=> Mungu Mtoaji wetu / Bwana atoaye, Mungu wa kweli ‐ Mwa 22: 8, 14
Yahweh provides,true God
17.JEHOVAH MAKEH
=>Bwana huadhibu dhambi Eze 7:9
The lord smites,punishes sin
18. JEHOVAH MEKADDISHEM
=> Bwana Nikutakasaye ‐ Kut 31:13
I the lord sanctity you Ex 31:13
19. JEHOVAH MISGAB
. =>Bwana ni Mwamba wangu na kinara cha wokovu wangu Zab 18:2
Lord is my rock and my tower deliverance Psa 18:2
20. JEHOVAH NISSI = (YEHOVA NISI )
=>Bwana ni Beramu ( Bendera) yetu
=>Mungu Ushindi wetu ‐ Kut 14:13‐14
=> Bwana ni Ishara yetu/ishara ya ushindi wetu
The lord is our banner /essign/sign
21. JEHOVAH RAPHA => (YEHOVA RAFA )
=>Mungu Atuponyaye ‐ Kut 15:26, Mwa 15:26
The lord who heals Ex15:26 Is 53:4
22. JEHOVAH ROHI
=> Bwana ni Mchungaji wangu ‐ Zab 23:1
The lord is my shepherd Psa 23;1
23.JEHOVAH SABAOTH
=> Bwana wa Majeshi (Majeshi ya Malaika )‐ Malaki 3:7 , 1Sam 1:3
The lord of hosts (Angelic armies)
24. JEHOVAH SHALOM =(YEHOVA SHALOM)
=> Mungu ni Amani yetu ‐ Amu 6:22‐24
The lord is our peace - Judges 6Vs22-24
25. JEHOVAH SHAMMA = (YEHOVA SHAMA )
=> Bwana Yupo/Bwana ni Aliyepo Kut 3:14 Eze 48:35
The lord is there/here Eze 48:35
26. JEHOVAH SHAPHAT
=>Bwana ni hukumu yangu Is 22:32
The lord is my judge
27. JEHOVAH TSIDKZEMU
=> Bwana ni Haki yetu ‐ Yer 23:6
The lord is our righteousness Jer 23:6
 
Ni maoni yako
Maoni yako wewe yakoje?

Hakuna imani bila dini na hakuna dini bila imani....Lazima ujue definition ya neno imani na definition ya neno dini
Kuna mambo bado huyaelewi.

Imani haitegemei dini. Dini ni mifumo tu iliyoanzishwa wala haina uhusiano wa moja kwa moja na imani. Kuna watu wapo kwenye dini moja lakini imani zao zimeegemea sehemu nyingine.
 
Wanajmii forum. Kwa uhuru tuliopewA na Mwenyezi Mungu... Allah/ JehovA... naomba tumkemee Mwanzisha Uzi.. kwa kujaribu Kumkashifu.. Mwenyezi Mungu anaetupA Uhai..
1. Dr. Janabi.. Director of MUHAS ( cardiologist) kuna kipindi alihojiwa ITV... alisema sisi Wataalam kuna kipindi tunautoa Moyo wote na kuufanyiA operation.... ila tunakua tunamba Mungu Moyo uendelee kudundA.... GOD miracles...
2. Ben Carson- Katika kitabu chake cha Gifted hands..." If we acknowledge our need for God, he will help us.”
ni mtu aliemwamini Sana Mwenyezi MUNGU... ALLAH/ JEHOVA
 
download.jpeg

Soma hiki kitabu.. utaelewa Ukuu wa Mungu.
 
Wanajmii forum. Kwa uhuru tuliopewA na Mwenyezi Mungu... Allah/ JehovA... naomba tumkemee Mwanzisha Uzi.. kwa kujaribu Kumkashifu.. Mwenyezi Mungu anaetupA Uhai..
1. Dr. Janabi.. Director of MUHAS ( cardiologist) kuna kipindi alihojiwa ITV... alisema sisi Wataalam kuna kipindi tunautoa Moyo wote na kuufanyiA operation.... ila tunakua tunamba Mungu Moyo uendelee kudundA.... GOD miracles...
2. Ben Carson- Katika kitabu chake cha Gifted hands..." If we acknowledge our need for God, he will help us.”
ni mtu aliemwamini Sana Mwenyezi MUNGU... ALLAH/ JEHOVA
Hapana, lengo langu ni kujifunza siyo kum-kashfu Mungu
 
Kwanza unajuaje kwamba uliumbwa?

Kwa nini unadhani uliumbwa na kitu usicho kifahamu na hukijui?

Ukisema designer aliye kuumba wewe yupo ina maana unamjua ulishawahi kumuona.

Lakini hujui kama kweli yupo ila ni imani za watu tu, kwamba yupo.Pia hata kusema hayupo ni sahihi kwa vile ukitaka kudhibitisha ali kuumba huwezi unabaki kukisia.
Hujajibu swali langu Mkuu,. Mimi nimeuliza hivi⤵️
Mtu pamoja na designed systems zote zilizopo kwenye mwili wake kwa ufahamu wako, zina Designer au hazina?
 
Hujajibu swali langu Mkuu,. Mimi nimeuliza hivi⤵️
Mtu pamoja na designed systems zote zilizopo kwenye mwili wake kwa ufahamu wako, zina Designer au hazina?
Akikujibu mo
MAJINA YA MUNGU NA MAANA ZAKE
♢GOD'S NAMES WITH THEIR MEANING

1. ADONAI
=> Mungu Mwenye enzi yote,kimbilio imara Mwa 15:2‐8, Kut 6:2‐3
God of sovereign,strong refuge
2. EL-ELYON
=> Mungu Aliye juu zaidi ‐Mwa14:18, Dan 4:34
Most high God Psa 21:7
3. EL‐GIBBOR
=> Mungu Mwenye Nguvu Isa 9:6, Zab 147:5
(Mighty God )
4.El GMULOT -
=>Mungu alipaye/atoaye ujira
The God of recompense Jer 51:56
5. EL- HAI
-Mungu Aliye Hai/Anaishi ‐Josh 3:10, 1Sam17:26
Living God
6. EL-OHEENU
. =>Bwana Mungu wetu Zab 99:5,8,9
Lord our God Psa 99:5,89
7.EL-OHIM
=> Mungu Muumbaji /Muumbaji wa milele ‐ Mwa33:20, Kol 1:16‐17
8.ELOHIM YISRAEL
=> Mimi ni Bwana Mungu wako
. Iam the lord your God Lev 18:2
9. EL-OLAM
=> Mungu wa Milele ‐ Ufu4:8, Kut 3:14 Mwa 21:23
Everlasting God/Eternal God [ olam means age ]
10. EL-ROI
=> Mungu Aonaye kila kitu ‐Mith 15:3, Zab 32:8
=> BWANA Mchungaji wangu Zab 23:1
The God of sight, The God who keeps watch Gen 16:13
11. EL-SHADDAI
Mungu Mtoshelezi ‐Mdo 17:28, Kumb 8:4
12. JEHOVA EL-ASHIYB
The lord my restorer
Bwana ni mrejeshaji wangu
13.JEHOVAH EL-EMUMAH -
Mungu mwaminifu
Faithful God
14.JEHOVAH EL-GEMU 'AH -
Mungu alipaye/atoaye ujira
The God of recompense Jer 51:56
15.JEHOVAH EL-MAGOWR -
Bwana ni Chemchemi ya maji hair
The fountain of living water Jer 2:13
16. JEHOVAH JIREH/YIR 'EH = (YEHOVA YIRE )
=> Mungu Mtoaji wetu / Bwana atoaye, Mungu wa kweli ‐ Mwa 22: 8, 14
Yahweh provides,true God
17.JEHOVAH MAKEH
=>Bwana huadhibu dhambi Eze 7:9
The lord smites,punishes sin
18. JEHOVAH MEKADDISHEM
=> Bwana Nikutakasaye ‐ Kut 31:13
I the lord sanctity you Ex 31:13
19. JEHOVAH MISGAB
. =>Bwana ni Mwamba wangu na kinara cha wokovu wangu Zab 18:2
Lord is my rock and my tower deliverance Psa 18:2
20. JEHOVAH NISSI = (YEHOVA NISI )
=>Bwana ni Beramu ( Bendera) yetu
=>Mungu Ushindi wetu ‐ Kut 14:13‐14
=> Bwana ni Ishara yetu/ishara ya ushindi wetu
The lord is our banner /essign/sign
21. JEHOVAH RAPHA => (YEHOVA RAFA )
=>Mungu Atuponyaye ‐ Kut 15:26, Mwa 15:26
The lord who heals Ex15:26 Is 53:4
22. JEHOVAH ROHI
=> Bwana ni Mchungaji wangu ‐ Zab 23:1
The lord is my shepherd Psa 23;1
23.JEHOVAH SABAOTH
=> Bwana wa Majeshi (Majeshi ya Malaika )‐ Malaki 3:7 , 1Sam 1:3
The lord of hosts (Angelic armies)
24. JEHOVAH SHALOM =(YEHOVA SHALOM)
=> Mungu ni Amani yetu ‐ Amu 6:22‐24
The lord is our peace - Judges 6Vs22-24
25. JEHOVAH SHAMMA = (YEHOVA SHAMA )
=> Bwana Yupo/Bwana ni Aliyepo Kut 3:14 Eze 48:35
The lord is there/here Eze 48:35
26. JEHOVAH SHAPHAT
=>Bwana ni hukumu yangu Is 22:32
The lord is my judge
27. JEHOVAH TSIDKZEMU
=> Bwana ni Haki yetu ‐ Yer 23:6
The lord is our righteousness Jer 23:6
Jina la Mungu nalolifahamu ni YHWH, hapo umetaja sifa zake.
 
Mungu yupi sasa ?????Mbona wana dini tofauti na kila dini ina mungi mwenye utaratibu wa tofauti na mwingine???
Mungu ni mmoja na dini ni Moja na manabii wote walifunuliwa Mungu ni mmoja na dini ni Moja

Hi ni orodha ya manabii waliotajwa ndani ya Quran kuwa walifunuliwa Mungu ni mmoja na dini ya kweli ni Moja ( Uislam)

1)Adam
2)Idris
3)Nuh
4)Saleh
5)Shuayb
6)Hud
7)Ibrahim
8)Lut
9)Ismail
10)Is-haq
11)Yaqub
12)Yusuph
13)Yunus
14)Mussa
15)Harun
16)Ayyub
17)Daud
18)Sulayman
19)Ilyas
20)Alyasa
21)Dhul-kifl
22)Zakaria
23)Yahya
24)Issa
25)Muhammad
 
Wakuu poleni kwa upambanaji.

Binafsi mimi kuna mda huwa nikitulizaga kichwa changu huwa naanza kujiuliza maswali mengi sana kuhusu mimi (binadamu) na ulimwengu kiujumla (Universe).

Maswali kama sisi (binadamu) ni kina nani,tumetoka wapi asili yetu, kwanini tupo (dhumuni la kuishi), mwisho wetu ama hatima yetu ni nini, Ulimwengu wa vitu je kama sayari, nyota, galaxies zimekuwepo vipi na nini hasa mwisho wake.

Hapo juu ni baadhi tu ya maswali ambayo huwa naiuliza sana akili yangu ikiwaga katika hali ya utulivu.

Lakini cha kusikitisha ni kwamba, katika maswali yote hayo ambayo huwa najiuliza, sijawahi kupata jibu la uhakika kuniridhisha kuhusu hayo maswali yangu.

Nimekuwa nikifanya bidii kubwa sana kupata majibu ya maswali yangu kupitia usomaji wa majarida au vitabu vihusuvyo historia,sayansi, dini na Falsafa lakini kote bado sijapata majibu ya kuniridhisha tofauti na kuambulia majibu ya kinadharia tu ambayo yana strength kiasi chake lakini pia yana weakness sehemu nyingi tu.

Na nikiri wazi tu kuwa katika usomaji wangu wa nadharia hizo zote (historia, sayansi, dini, falsafa) sehemu ambayo nimeanza kuiamini kunipa majibu ya maswali yangu ni kwenye DINI.

Nikiwa na maana nimeanza kuamini kwamba uwepo na sisi tuliohai na visivyo hai hapa ulimwenguni ni matokea ya Uumbaji ya nguvu kubwa sana inayoitwa MUNGU/ALLAH kama ambavyo dini nyingi zinaelezea nguvu hiyo.

Na leo maswali yangu yanajikita huko kwenye hiyo nguvu (Mungu) maana nimeanza kuiamini lakini pia kila nisomapo BIBLIA (mimi mkristo) inanipa maswali chungu nzima.

Sasa leo swali langu limejikita kwenye UKAMILIFU wa MUNGU.

Naombeni wasomaji mnielewe kuwa sina maana ya kukufuru (maana mara nyingi niulizapo maswali kuhusu MUNGU huwa naambiwa nakufuru) bali mimi nataka kujifunza zaidi kumuhusu huyu Mungu.

Dini nyingi (hasa Ukristo na uislamu) zimekuwa zikimwelezea Mungu kuwa ni Mkamilifu sana,mwenye nguvu nyingi sana, uwezo na akili zake hazichunguziki, hashindwi na chochote n.k.

Je hilo lina ukweli ? kupitia Biblia mimi nimeanza kudhani kwamba huenda kweli Mungu ana nguvu nyingi sana ila siyo zote, ana uwezo mkubwa sana ila siyo uwezo wote,ana maarifa mengi sana ila siyo maarifa yote, ana ukamilifu mwingi sana ila siyo ukamilifu wote n.k

Nasema haya ni kutokana na maswali yafuatayo :

1. Kama Mungu ana ukamilifu wote, kwanini sasa alimuumba malaika (Lucifer/shetani) alafu badae akaja kumuasi?
Kama Shetani/Lucifer aliasi maana yake ni kwamba Mungu alimuumba huyu kiumbe akiwa na madhaifu kadhaa na ndiyo maana alishindwa kuitii amri/mamlaka ya muumbaji wake.

Kama Mungu angelikuwa na ukamilifu wote, basi malaika wote wangelikuwa wameumbwa katika namna ya utii pekee, uasi usingetokea na huo uasi unadhihirisha kwamba Mungu aliwaumba hawa malaika wakiwa na udhaifu flani, hawakuwa na uimara wote.

2. Uumbaji wa Eva (Hawa) unaonesha kulikuwa na madhaifu pia.
Katika Biblia takatifu kwenye kitabu cha mwanzo, kuna mistari inaeleza kuwa "Mungu alimpa usingizi mzito Adam, alafu akabandua sehemu ya ubavu wake na kumfanya/kumuumba mwanamke (Hawa/Eva)".

Alafu Mungu akamwambia Adam kuwa huyu mwanamke atakuwa msaidizi wako

Lakini ni huyo huyo mwanamke ambae shetani (kwenye umbo la nyoka) alienda kumdanganya akachukua matunda ya mti walioambiwa asile yeye akala na akampelekea na mumewe (Adam) pia akala.

Lakini Mungu alivyomuuliza Adam kwanini umekula matunda ya mti ambao nilikwambia usile, Adam alijibu kuwa "Ni huyo mwanamke uliyenipa ndiye aliyeniletea nikala".

Tukio hili linadhihirisha kuwa Mungu alimpa Adam msaidizi (Hawa) ambae ni dhaifu sana na ndiyo maana alisababisha dhambi ikaenda hadi kwa Adam.

Na huenda kama Mungu angelikuwa amempa Adam msaidizi imara asiye na madhaifu basi ile dhambi ya kula tunda ingeepukika.

Uko wapi sasa ukamilifu wote wa Mungu ikiwa aliweza kuwaumba malaika dhaifu (ambao walikuja kumuasi) na pia bado akampa Adam msaidizi dhaifu kabisa ambaye alisababisha dhambi imwendee hadi Adam?

Kwa leo naombeni comment zenu zinifunze kuhusu hilo tu (La ukamilifu wa Mungu) alafu mengine nitauliza siku nyingine, na mengine nitakuwa nauliza humo humo kwenye comments zenu.

NB: Naamini Mungu yupo, kutokana na baadhi ya vitu ninavyoviona ulimwenguni (hasa uumbaji/creation) ambapo kuna baadhi ya vitu hasa sayansi inakosa majibu ya kuridhisha, ila shida yangu kubwa ni sifa za Mungu ambazo anapewa na wanadamu naona kama zinashindwa kujidhihirisha kwenye baadhi ya mambo.

Karibuni mnifunze.
Safi umeanza kupevuka kiakili niseme sio watu wengi hujiuliza kwa undani hivi. Mimi nami katika kujibu maswali ya watu huwajibu kulingana na level yao.

Usitetereke kiimani hata mimi naamini uwepo wa Mungu. Lakini yakupasa kujua kuwa Mungu tunayesoma habari zake vitabuni (Biblia, Quran) sio yule Mungu halisi kwani ameelezewa kulingana na jinsi mtu flani alivyoona, ndio kusema ni vigumu kumwelezea Mungu kwa utimilifu wake kwani kuna tatizo kubwa la kumwelewa Mungu (epistemological problem).

Ni kweli yeye ni mkamilifu na mweza wa vyote ameumba vyote na kuvipa uhuru ikiwa ni pamoja na shetani. Shetani au mwanadamu akitumia uhuru wake kufanya ubaya Mungu hawezi kulaumiwa.

Ubaya au uovu ni jinsi unavyoona wewe tu niseme in absolute terms hakuna kitu kama hicho! Kwani simba akila swala ni uovu? Je simba akila mtu ni uovu! Au mtu akila swala ni uovu? Mtu akila ndizi ni uovu? Na je mtu akila mtu ni uovu?

Ni “hatari “ kutaka kumjua sana Mungu na unatakiwa uwe na uelewa flani wa mambo la sivyo utaishia kuwa hovyo. Nitaachia hapo kwani kujua kunaambatana na majukumu makubwa.
 
Back
Top Bottom