Pre GE2025 Nabii Sanga: Mgawanyiko mkubwa utaikumba CCM mwaka 2024 na 2025, tuiombee

Pre GE2025 Nabii Sanga: Mgawanyiko mkubwa utaikumba CCM mwaka 2024 na 2025, tuiombee

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huyo ni nabii wa aina gani ambae hawaoni wapinzani bali aiona CCM tu katika miujiza yake?

Angefanya pia maombi kwa upinzani ili nao uweze kupata ushawishi ili wachaguliwe na wananchi.
Tumalizane na hili, Kisha tutamuuliza baadae.
 
Mi naamini CCM asili, yenye watu aina ya Butiku na WARIOBA ikirudi,

Tukaandika Katiba mpya,

Tutarudi kwenye mstari.

CCM ya akina Butiku, Warioba ikirudi, nami nitakuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kuchukua kadi. Lakini kwa CCM hii ya akina Makamba, Nape na akina Ridhiwani, hata kwa mijeledi, siwezi kuthubutu.
 
It is obvious kesho ni jumanne au siyo?Nabii kadandia gari kwa mbele🤣🤣
Mtu ameona na wote tumeona wingu zito na radi zinapiga halafu yeye anajifanya ana unabii wa mvua kunyesha?
 
What if Mungu anapenda chama hiki kuendelea kutuongoza?
Mkuu Rabboni "teacher" huwa nakuelewa sana mtumishi kutokana na ushuhuda wa Roho Mtakatifu ndani yangu. Lakini kwa swala la ccm kuparaganyika inaweza kuwa mwanzo wa Tanzania tuitakayo, ishara ya Mungu kuwakataa yaweza kuwa kuumana na kulana ccm wenyewe kwa wenyewe.
 
Mkuu Rabboni "teacher" huwa nakuelewa sana mtumishi kutokana na ushuhuda wa Roho Mtakatifu ndani yangu. Lakini kwa swala la ccm kuparaganyika inaweza kuwa mwanzo wa Tanzania tuitakayo, ishara ya Mungu kuwakataa yaweza kuwa kuumana na kulana ccm wenyewe kwa wenyewe.
Ndo tuombe,

Ili kuparaganyika kwao kusisababishe maumivu Kwa wasohusika, raia maskini.

Wavamizi, wapiga deal ndani ya chama, mfumo wao ukikomeshwa, tutapiga hatua kubwa sana kimaendeleo.
 
Salaam, Shalom.

Katika Unabii wa mwaka 2024, Nabii Sanga ametoa ujumbe Kwa Watanzania kuingia katika maombi kukiombea chama tawala CCM, amesema ameambiwa kuwa mwaka huu 2024 kutakuwa na mgawanyiko mkubwa utakaokikumba chama hiki.

Amesema pia kuwa, mgawanyiko na mtikisiko utakaokikumba chama Cha MAPINDUZI CCM, haitakuwa Siri, itakuwa ni mtikisiko wa wazi ambao hata raia wa kawaida watajua.

Amesema Mungu amemwambia awaase raia kukiombea Chama Cha MAPINDUZI CCM Kwakuwa mtikisiko wa chama tawala utaathiri pia Nchi Kwa ujumla, na ujumbe wa kukiombea CCM ni Ishara kuwa Mungu BADO anapenda CCM iendelee kuongoza Nchi na amesema kuwa, adui amepanga kutumia mgawanyiko huo kuivuruga Amani ya nchi.

Amesema pia, amepata ujumbe kuwapa Marais wote wa Africa kuwa Waaminifu Kwa Nchi zao na kuwatumikia wananchi Kwa HAKI, la sivyo, patakuwako maandamano katika Nchi nyingi Afrika ikiwa hawatakuwa Waaminifu.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni.🙏

Source: POG family Tv.
Haihitaji unabii

Kaibieni waumini pesa

Siasa acheni
 
Haihitaji unabii

Kaibieni waumini pesa

Siasa acheni
Kwamba Mungu akileta maonyo au maelekezo Kwa Taifa na viongozi wa Nchi wawe wananyamaza?

Mambo hayaendi hivyo, Nchi ni yetu sote.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hawa manabii [emoji119]
 
Mtikisiko ukitokea ndani ya CCM itakuwa ni jambo jema kwa Tanzania. Tukipata vyama viwili, kambi mbili, at least mojawapo inaweza kuanza kujali maslahi ya taifa na kuacha kuishi kwa mazoea.
Utabiri wa Mwalimu Nyerere ?!
Ngoja tuone 🙏
 
Kwamba Mungu akileta maonyo au maelekezo Kwa Taifa na viongozi wa Nchi wawe wananyamaza?

Mambo hayaendi hivyo, Nchi ni yetu sote.
Hapana

Yuko biased na siasa tangu tunafanya naye kazi mwanza

Hatujamjua leo

Ni shabiki wa kemera na populism
 
Hapana

Yuko biased na siasa tangu tunafanya naye kazi mwanza

Hatujamjua leo

Ni shabiki wa kemera na populism
Ndo nasema,

Wewe huoni haja ya CCM kutubu na kubadili uelekeo juu ya namna wanavyoongoza wananchi?
 
Salaam, Shalom.

Katika Unabii wa mwaka 2024, Nabii Sanga ametoa ujumbe Kwa Watanzania kuingia katika maombi kukiombea chama tawala CCM, amesema ameambiwa kuwa mwaka huu 2024 kutakuwa na mgawanyiko mkubwa utakaokikumba chama hiki.

Amesema pia kuwa, mgawanyiko na mtikisiko utakaokikumba chama Cha MAPINDUZI CCM, haitakuwa Siri, itakuwa ni mtikisiko wa wazi ambao hata raia wa kawaida watajua.

Amesema Mungu amemwambia awaase raia kukiombea Chama Cha MAPINDUZI CCM Kwakuwa mtikisiko wa chama tawala utaathiri pia Nchi Kwa ujumla, na ujumbe wa kukiombea CCM ni Ishara kuwa Mungu BADO anapenda CCM iendelee kuongoza Nchi na amesema kuwa, adui amepanga kutumia mgawanyiko huo kuivuruga Amani ya nchi.

Amesema pia, amepata ujumbe kuwapa Marais wote wa Africa kuwa Waaminifu Kwa Nchi zao na kuwatumikia wananchi Kwa HAKI, la sivyo, patakuwako maandamano katika Nchi nyingi Afrika ikiwa hawatakuwa Waaminifu.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni.🙏

Source: POG family Tv.
Upuuzi mtupu. Watu tunafanya kila liwezekanalo CCM ife ili kuinusuru nchi hii wewe unataka iombewe? Una akili sawacsawa kweli.
 
Back
Top Bottom