Nachukizwa na wanaomuita mwanangu Zuchu

Nachukizwa na wanaomuita mwanangu Zuchu

Utakaapochukia ndio watu watakufanyia inda, hivyo ndio wengi wa binaadam walivyo, mühimu wewe ni kumwambia mtoto wako asiitikie akiitwa jina Hilo Maana sio lake, na wala asiwaambie msiniite, akiwakataza ndio watakapozidi, yeye ajifanye kiziwi akisikia jina hilo na kumfahamisha kwanini unachukia asiitwe hivyo na ushahidi kumionyesha.
Uzuri ni kwamba hata yeye anajua Baba yake sipendi hilo jina, na kweli itabidi niwe namwambia awapuuze na kuto kukubali kuitikia hilo jina
 
Habari za wakati huu waungwana..

Mitaani kumekuwa na tabia ya kuwaita watoto wa kike jina la ZUCHU, hasa kwa wale ambao majina yao yanaanzia na herufi 'Zu'

Mwanangu anaitwa Zulfa, sasa wanamuita ZUCHU kitu ambacho mimi kama mzazi sipendi kwani sio jina nililompa mwanangu.

Wakati mwingine nawaza kubadili jina na kutafuta jingine lakini siwezi kwani Zulfa ni jina ninalo lipenda.

Ujumbe wangu ni kwamba, sio vizuri kutunga na kuwapa majina watoto wa watu ambao wana majina yao halisi, hasa kuwapa majina ambayo hayana picha nzuri upande wa maudhui na maadili.
Sasa hapa JF umeambiwa kuna hao wanaomwita hilo jina?? AU ndio matumizi ya bundle lako na keybord ya sim yako?
 
Back
Top Bottom