Nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania ni ipi, Kwanini Rais wa Zanzibar awe Msaidizi wa Rais Samia?

Nafasi ya Makamu wa Rais wa Tanzania ni ipi, Kwanini Rais wa Zanzibar awe Msaidizi wa Rais Samia?

Kitendo hiki ni Cha Uvunjaji mkubwa zaidi wa Katiba ya nchi hii ya Tanzania.

Rais wa Zanzibar hana mamlaka ya ki-Urais ya kuweza kumwakilisha Rais wa Tanzania huko nje ya nchi kwani hana mamlaka ya kikatiba kwa upande wa Tanganyika. Aidha, Makamu wa Rais wa Tanzania anayo mamlaka ya kiutendaji u-Rais) hata kwa upande wa Zanzibar, lakini nashangaa ni kwa nini Makamu wa Rais mara nyingi sana amekuwa akienguliwa katika kupewa nafasi ya kumwakilisha Rais wa Tanzania katika ziara za kikazi huko nje ya Tanzania na badala yake nafasi yake imekuwa ikiwaklishwa na Rais wa Zanzibar, mtu ambaye mwenye Cheo kidogo ukilinganisha na cheo Cha Makamu wa Rais.

Nafikiri ndani ya Ikulu ya Rais wa Tanzania kuna tatizo kubwa Sana hususani kuhusiana na Mambo ya masuala ya Itifaki (Protocol). Kuna shuhuda nyingi sana za wazi kabisa ambazo zimedhihirisha kwamba Masuala haya ya Itifaki ndani ya Ikulu ya Rais wa Tanzania yamekuwa hayazingatiwi wala kutiliwa maanani. Mara nyingi Itifaki hii imekuwa ikivunjwa hadharani, na tatizo hili limekuwa likijirudia rudia.

Kwa kuzingatia Muundo wa Utendaji ndani ya Ikulu ya Rais wa Tanzania, Je, mtu mwenye Cheo gani hasa ndani ya Ikulu ambaye anahusika moja kwa moja na Usimamizi wa masuala ya Itifaki katika nchi hii???
Huu Muungano tugawane mbao tu
 
Sisi tumezaliwa Tanzania hatukuikuta Tanganyika. Tanganyika iliishakufa zamani na ikazikwa jumla. Sasa tuna Tanzania tuu.
P
Pascal, hivi huwa unakuwaje kwenye ubongo wako??? Huwa Unafikiri kwa kutumia vigezo gani hasa??

Hiyo Tanganyika unayodai kwamba "ilishakufa zamani na ikazikwa" ni Tanganyika ya wapi hiyo??????
Ilikufa lini?? Ilizikwa wapi na kaburi lake liko wapi?? Je, unaweza kwenda kutuonyesha hilo kaburi ambalo Tanganyika ilizikwa humo??
 
Wataalam wa Masuala ya Protokali na Katiba ya Nchi tunaomba Maelezo yenu ili tuelewe, Siku tutakuja kuambiwa Mkuu wa Wilaya ya Chakechake au Kizimkazi Kamwakilisha Rais Nchi Fulani.

Ikiwa Makamu wa Rais wa Tanzania yupo na ni mzima wa Afya, inakuwaje mtu asiye na cheo chochote Tanzania amwakilishe Rais wa Tanzania?

View attachment 3083085
Baba hizo deal za watu kumbuka Tanzania bara kuna mzanzibar na zanzibar kuna mzanzibar tukae kwa utulivu.
 
C
Watanzania wanahitaji sana kufundishwa katiba yao, Rais wa Tanzania ni executive president na sio ceremonial leader, amepewa mamlaka inayoitwa presidential appointment ya kumteua mtu yeyote kumsaidia au kumwakilisha popote as long as ni Mtanzania and sometimes sio lazima awe Mtanzania!. Je, wajua Rais aweza kuteua yeyote hata darasa la saba?. Teuzi hizi hazihojiwi popote na yeyote!

Kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania ambao Watanzania wote wa pande zote wana haki sawa za Utanzania hivyo kiuraia Wanzanzibari wote wana haki sawa za Utanzania kama wabara, hivyo wana haki ya kuteuliwa kushika nafasi yoyote ya uongozi popote ndani ya JMT na Rais wa JMT yuko huru kumteua mtu yoyote kumwakilisha popote katiba jambo lolote!.

Inapotokea Rais hayupo kabisa au hawezi kutekeleza majukumu yake ya urais kwa sababu yoyote ile ikiwemo kifo, then hierarchy ya Katiba ya JMT inafuatwa
No.1 ni Rais wa JMT
No.2 ni VP
No.3 ni PM
No.4 ni Spika
No. 5 ni CJ

Lakini inapotokea Rais yupo busy, anaweza kumteua mtu yoyote kumwakilisha popote.

Pia kuna hierarchy ya ki Protokali
No. 1. Rais
No. 2 VP
No. 3 ZnZ President
No. 4 PM
No. 5. DPM
No. 6 VP 1- ZnZ
No. 7 VP 2- ZnZ
No. 8 -Spika
No. 9- CJ
No. 10- CDF

P
Chenga
 
Watanzania wanahitaji sana kufundishwa katiba yao, Rais wa Tanzania ni executive president na sio ceremonial leader, amepewa mamlaka inayoitwa presidential appointment ya kumteua mtu yeyote kumsaidia au kumwakilisha popote as long as ni Mtanzania and sometimes sio lazima awe Mtanzania!. Je, wajua Rais aweza kuteua yeyote hata darasa la saba?. Teuzi hizi hazihojiwi popote na yeyote!

Kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu, uraia wa Tanzania ambao Watanzania wote wa pande zote wana haki sawa za Utanzania hivyo kiuraia Wanzanzibari wote wana haki sawa za Utanzania kama wabara, hivyo wana haki ya kuteuliwa kushika nafasi yoyote ya uongozi popote ndani ya JMT na Rais wa JMT yuko huru kumteua mtu yoyote kumwakilisha popote katiba jambo lolote!.

Inapotokea Rais hayupo kabisa au hawezi kutekeleza majukumu yake ya urais kwa sababu yoyote ile ikiwemo kifo, then hierarchy ya Katiba ya JMT inafuatwa
No.1 ni Rais wa JMT
No.2 ni VP
No.3 ni PM
No.4 ni Spika
No. 5 ni CJ

Lakini inapotokea Rais yupo busy, anaweza kumteua mtu yoyote kumwakilisha popote.

Pia kuna hierarchy ya ki Protokali
No. 1. Rais
No. 2 VP
No. 3 ZnZ President
No. 4 PM
No. 5. DPM
No. 6 VP 1- ZnZ
No. 7 VP 2- ZnZ
No. 8 -Spika
No. 9- CJ
No. 10- CDF

P
Raisi kwa maelezo yako anaweza hata darasa la saba awe jurge.? Mgambo awe mkuu wa majeshi Dr awe CAG
[emoji1787]
 
Raisi kwa maelezo yako anaweza hata darasa la saba awe jurge.? Mgambo awe mkuu wa majeshi Dr awe CAG
Tujifunze basi kusoma kitu ndipo unlike swali. Nimekuwekea ndiko limesema Je, wajua Rais aweza kuteua yeyote hata darasa la saba?. Teuzi hizi hazihojiwi popote na yeyote! ungelisoma hilo andiko, usingeuliza hili swali, ila kwa faida ya wengi nakuwekea
Wanabodi,

Teuzi za Sifa na Vigezo na Teuzi Ambazo Hazina Sifa wa Vigezo.
Teuzi zote za rais, hufanyika kwa mujibu wa katiba, ila katika teuzi hizo, kuna teuzi za aina mbili, kuna teuzi zinazohitaji sifa na vigezo, na kuna teuzi ambazo hazihitaji sifa wala vigezo. Nafasi za uteuzi zinazohitaji sifa na vigezo, zimeainishwa katika katiba na sifa hizo na vigezo pia zimeainishwa kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni, yaani prescribed kwa kumuelekeza rais atateua watu wenye sifa gani katika nafasi zipi, mfano Jaji Mkuu lazima awe mwanasheria, Mwenyekiti wa NEC lazima awe Jaji Mstaafu, CDF lazima awe ni mwanajeshi, IGP lazima awe polisi, Director wa TISS lazima awe ni "wale jamaa", Msajili wa vyama ni Jaji, CAG mtu wa mahesabu, au wakurugenzi wakuu wa taasisi za umma katika positions za utendaji, lazima wawe na sifa fulani za kielimu na kitaaluma. Baadhi ya teuzi hizi hazifanyiki at presidents pleasures bali rais huzifanya kwa kufuata maelekezo, mfano Jaji Mkuu, ni kwa maelekezo ya Tume ya Majaji, Katibu wa Bunge, tume ya Bunge, na pia zina kitu kinachoitwa " a security of tenure" kumaanisha rais anaweza kuteua tuu not at his pleasure bali kwa maelekezo na akiishamteua hawezi kumfukuza anavyojisikia, not at his pleasure bali kwa utaratibu maalum, hawa ni pamoja na Jaji Mkuu, Gavana wa BOT, CAG etc.
Paskali.

P
 
Kwa mujibu wa katiba ya JMT, nafasi ya VP ni just only if President hayupo, kama vile ile ya March 17, lakini president akiwepo, VP hana any executive powers zozote zaidi ya kusubiria just in case rais ata nanilii!, hivyo Rais anaweza kumpangia mtu yeyote kumwakilisha popote na hajakiuka katiba!.
Tujifunze katiba ya JMT.
Mimi nimejitolea kusaidia Kipindi cha TV, Kutoa Elimu ya Katiba, Sheria na Haki, Kuanza Jumapili Hii Kupita Channel Ten
P
Mara mambo ya Muungano na kero za Muungano ziko kwake kimajukumu lakini hana Mamlaka nazo,hawezi kuhamisha hata mkato(,) kwenye setup yake.Katiba nzuri itakayoainisha majukumu na Mamlaka ya Kila VIP na kuondokana na hii (dried vip).inahitajika Sasa kama si leo.
 
Mara mambo ya Muungano na kero za Muungano ziko kwake kimajukumu lakini hana Mamlaka nazo,hawezi kuhamisha hata mkato(,) kwenye setup yake.Katiba nzuri itakayoainisha majukumu na Mamlaka ya Kila VIP na kuondokana na hii (dried vip).inahitajika Sasa kama si leo.
Naunga mkono hoja
P
 
Back
Top Bottom