Taarifa inasema makarani wote wamepatiwa mafunzo,hii nchi ngumu sana.
NBS toeni ufafanuzi hapa #SOURCE AZAMTV[emoji116]
SENSA YA 2022 KUFANYIKA KIDIGITALI ZAIDI
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema kwa mara ya kwanza tangu #Tanzania ipate uhuru, sughuli ya sensa ya watu na makazi mwaka huu itaingiza maeneo ya vitongoji vyote nchini katika mfumo wa kidigitali na hivyo kurahisisha kazi ya kukusanya takwimu husika kwa njia rahisi na ya haraka zaidi.
Akizungumza na Jukwaa la Wahariri mkoani Morogoro, Mkuu wa Mifumo ya Ukusanyaji wa Taarifa za Kijiografia (GIS) na Kaimu Meneja wa shughuli za Kitakwimu, Benedict Mgambi amesema, sensa ya mwaka huu inayotarajiwa kufanyika Agosti 23-29 itakuwa ya kidigitali na ufanisi zaidi katika ukusanyaji wa taarifa tofauti na miaka iliyopita.
Alifafanua kuwa hilo litawezekana kwasababu makarani wote wamepatiwa mafunzo ya kutosha ya kutumia vishikwambi vyenye mifumo ya kidigitali kwa lengo la kupeleka taarifa moja kwa moja kwenye kanzidata ya NBS makao makuu pamoja na uwepo wa mfumo wa kuwafuatilia makarani wote popote walipo.
Tangu kuanza kwa shughuli ya sensa mwaka 1967 hadi 2012, sensa ya mwaka huu itakuwa ya kipekee na itahusisha idadi ndogo ya makarani kwasababu ya uboreshwaji wa miundombinu ya ufanyaji kazi.
Sensa mwaka ya mwaka hu, Tanzania inatarajiwa kuwa na watu milioni 61.3, wakati sensa ya kwanza mwaka 1967, Tanzania ilikuwa na watu milioni 12.3, mwaka 1978 ilikuwa na watu milioni 17.5, mwaka 1988 ilikuwa na watu milioni 23.1 na mwaka 2012 ilikuwa na watu milioni 44.9.
#AzamTVUpdates #AzamNews #Sesa2022
View attachment 2265675