JW Kama unatokea mtaani aisee ni hatari sana kwa afya kama hauna nguvu nyuma yako vinginevyo siku yako tu iwe imefika ila hivi hivi sio poa.
Ili kupenya katika ule usahili nyuma yako inatakiwa nguvu kubwa.
Wakati nipo JKT kuna jamaa nilikua nimezoeana naye maana tulikua tupo Coy moja na Platoon moja.
Kumbe mshikaji mzee wake alikua kitengo JW.
Sasa ikawa bado kama mwezi hivi kozi yetu ya kwa mujibu iwe imetamatika ghafla jamaa akapigiwa simu na mzee wake kua anatakiwa aende kambi ya Itaka kwa maana itakua ni moja ya kambi ambazo watachukua watu wa kwenda kupiga cadeth.
Kitu kilichonichosha ni kua maelekezo ya mshikaji kupelekwa Itaka,Mkuu wa kambi kashapewa maelekezo kila kitu na anatakiwa ahakikishe kua mshikaji anaenda itaka haraka iwezekanavyo.
Usiku wa ile siku ambayo mchizi alioongeana mshua wake.
Tukiwa tumefoleni kama kawaida kwa ajili ya madoso akaja mkuu wa kambi akamuulizia mshikaji kwa kutaja majina yake then akaniambia nifuate.
Baada ya hapo sikumuona tena jamaa mpaka kozi inaisha.[emoji28].
Hapo ndio nikaamini bongo Nyosso.
Sent using
Jamii Forums mobile app