Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,984
Mhe. Freeman Mbowe yupo mahabusu kwa miezi kadhaa sasa, siyo kwa sababu ametenda kosa ya jinai bali kwa sababu amekataa kutumika kuwakandamiza watanzania. Kukaa kwake ndani naamini ni Mpango wa Mungu kutufunulia aina ya watawala tukio pamoja na namna dola inavyoshughulika na wanachi wasio na hatia. Kuwekwa kwake mahabusu kunatuonyesha aina ya Majaji na Mahakimu tulionao pamoja na kutufumbua macho Kwanini wezi wa rasilimali za nchi Wapo uraia lakini maskini Wapo magerezani. Tunapata kufumbuliwa macho kwanini nchi inauza rasilimali zetu kwa wageni kila kukicha, tunatambua ni kwa nini tunaamini maendeleo ya Tanzania yataletwa na wageni na si Watanzania.
Mbowe amevunjiwa vitega uchumi vyake ambavyo naamini viliwanufaisha zaidi waajiriwa wake kuliko yeye mwajiri. Wakati akivunjiwa vitega uchumi nchi imeingia Mikataba na wageni wengi kuja kuwekeza nchini na yeyote atakayewasumbua wawekezaji hao atakiona cha moto. Chuki baina ya watawala na watawaliwa imepelekea leo miradi yote ya watu wenye mawazo tofauti na serikali imekufa kwa mgongo wa uhujumu uchumi lakini miradi ya wageni inalindwa kwa nguvu zote. Watawala wamejaa chuki.
Kama watawala wamejaa chuki dhidi ya watawaliwa ni dhahiri kwamba Mbowe ana amani sana kuliko watawala. Amani ya Mbowe inatokana na ukweli kwamba Hana hatia moyoni mwake na ateseki kwa ajili yake anateseka kwa ajili ya watawaliwa.
Tumeona kilichotoka jana ambapo bila kutumwa na Mbowe mkutano uligubikwa na agenda ya Mbowe kwa maneno na context mbalimbali. Mbowe yupo mahabusu ila wapo watu wanajiona wao wanamthamini sana kuliko anavyojithamini mwenyewe. Kuna watu unawaona wanaumia sana kwanini Mbowe yupo ndani na hari ya wafuasi wa chama chake ipo juu. Kumbuka watu wenye roho mbaya wakiona unafanikiwa wanaumia zaidi. Ndicho kinachotokea leo.
Ukiangalia mitandaoni na hata kwenye hii post utabaini Wana CCM wanampigania sana Mbowe kuliko hata wanavyompigania kiongozi wao, si kwamba wanamaanisha hivyo bali wamebaini Mungu wa Mbowe ni Mungu wa wanyonge.
Haingii akilini kuona watawala wanataka kumlaumu mahabusu kwanini ajawapigia magoti. Mbowe ameamua kwa dhati kufungwa ili watakaomfunga waende Mbinguni ,ajataka wamfanyie upendeleo waende kuzimu. Amewaruhusu watumie madaraka yao wapendavyo huku akijua siku za mwanadamu kuishi zinapangwa na Mungu
Mbowe amevunjiwa vitega uchumi vyake ambavyo naamini viliwanufaisha zaidi waajiriwa wake kuliko yeye mwajiri. Wakati akivunjiwa vitega uchumi nchi imeingia Mikataba na wageni wengi kuja kuwekeza nchini na yeyote atakayewasumbua wawekezaji hao atakiona cha moto. Chuki baina ya watawala na watawaliwa imepelekea leo miradi yote ya watu wenye mawazo tofauti na serikali imekufa kwa mgongo wa uhujumu uchumi lakini miradi ya wageni inalindwa kwa nguvu zote. Watawala wamejaa chuki.
Kama watawala wamejaa chuki dhidi ya watawaliwa ni dhahiri kwamba Mbowe ana amani sana kuliko watawala. Amani ya Mbowe inatokana na ukweli kwamba Hana hatia moyoni mwake na ateseki kwa ajili yake anateseka kwa ajili ya watawaliwa.
Tumeona kilichotoka jana ambapo bila kutumwa na Mbowe mkutano uligubikwa na agenda ya Mbowe kwa maneno na context mbalimbali. Mbowe yupo mahabusu ila wapo watu wanajiona wao wanamthamini sana kuliko anavyojithamini mwenyewe. Kuna watu unawaona wanaumia sana kwanini Mbowe yupo ndani na hari ya wafuasi wa chama chake ipo juu. Kumbuka watu wenye roho mbaya wakiona unafanikiwa wanaumia zaidi. Ndicho kinachotokea leo.
Ukiangalia mitandaoni na hata kwenye hii post utabaini Wana CCM wanampigania sana Mbowe kuliko hata wanavyompigania kiongozi wao, si kwamba wanamaanisha hivyo bali wamebaini Mungu wa Mbowe ni Mungu wa wanyonge.
Haingii akilini kuona watawala wanataka kumlaumu mahabusu kwanini ajawapigia magoti. Mbowe ameamua kwa dhati kufungwa ili watakaomfunga waende Mbinguni ,ajataka wamfanyie upendeleo waende kuzimu. Amewaruhusu watumie madaraka yao wapendavyo huku akijua siku za mwanadamu kuishi zinapangwa na Mungu