Nahisi kama napoteza mahusiano na mzazi

Nahisi kama napoteza mahusiano na mzazi

Wazazi nao wanazinguaga basi tu ndio vile washakua wakubwa kwetu so tunajitahidi kuishi humo kwenye nidhamu

Kama sababu za ugomvi wenu ni kupishana mitazamo mfano mama anataka uende kanisani wewe hutaki,hataki utembee usiku basi jitahidi kumsikiliza anayotaka yeye...muhimu hayana madhara kwako
hii imekaa kihisia zaidi, au ni huu ujana ujana foolish age??😅
 
Nimekua nikipata changamoto kwenye mahusiano na mzazi, kuna kuwa hamna maelewano kati yetu, tunagombana sana, hatuwezi kukaa sehemu moja tukazungumza usitokee ugomvi kati yetu.... na kinachonishangaza zaidi, nikijaribu kuangalia sababu sielewi, hii hali imekua ikiendelea kwa mda mrefu sasa na inanipa mawazo kwa kweli.....

Sasa hii hali imenipelekea kukwepa kwenda nyumbani kwa miaka karibia mitatu sasa, nipo chuo, na nikiwa likizo najiweka mbali na mzazi.... mfano mwaka jana ilitokea mzozo kwelikweli, nilikua nimefunga chuo nikagoma kufikia kwa mama alipokua kikazi, kwasababu hakuweza kua nyumbani kwa muda huo, tuligombana sana mpaka ikafikia hatua ya yeye kunikaripia 'usipokuja kuniona wewe sio mwanangu' basi ikabidi niende kishingo upande ila sikua na amani....

Tumeendelea kuishi hivi hivi kwa kulumbana mpaka hivi sasa, bado ugomvi unatokea mara kwa mara, hivi sasa tumefunga chuo nimebaki huku huku chuo kufanyia field, imekua mzozo kweli kweli mara aniambie simpendi ndo maana sitaki kwenda kumuona, leo tumezozana anadhani naishi na binti huku nimempa mimba, anataka aje kuona nnapoishi....

Najua mtaona kama kuna maovu yangu naficha, ndio maana nagombana na mzazi, nakubali kuna makosa nimefanya nikagombana na mzazi lakini tuliyamaliza, ila hii hali ni tofauti, nikiwa karibu na mzazi nahisi vibaya, sijui kwanini, natamani tu nijiweke mbali nae.... hii hali inanitesa sana, na nikifikiria huyu ndo mzazi pekee niliyebaki nae, naumia zaidi, natamani kuithibiti hii hali, ila inajirudia....

Najua humu kuna watu wazima mmeshapita ujana na changamoto zake, hebu nishaurini kwa mtazamo wenu nifanyeje ili kurudisha mahusiano na mzazi....

Mwanaume, matured au Mwanamke hulipa gharama ya kujenga mahusiano na wazazi wake, You pay that cos, and not em, You do that. Utakuwa tu mjuani, hakuna lingine, kumbuka kama sio malezi yao na kujibisha kukusomesha usingekuwa na chuoni pa kukimbilia.
 
FB_IMG_1687252634251.jpg


Hii ni meme lakini ina ujumbe mzuri sana sijamaanisha kumtukana mzazi wako no, mchukulie hayo ndio madhaifu yake usibishane nae analosema usitumie nguvu nyingi kumpinga aking'ang'ania kitu mkubalie kama hakina madhara kwako mheshimu.

note; acha kujibizana nae wewe msikilize yanayofaa chukua yasiyofaa acha , ila usimdharau ukiona mnaelekea siko katisha maongezi usimkere
 
Acha Kiburi kijana mheshimu mzazi wako msikilize muelewane.
Unasema Kuwa hutaman kuishi naye hilo ni hisia za Upendo kwa mzazi wako na chanzo chake n ugomvi wa mara kwa mara ndo maana humtaki, solution yake acha Kiburi mpende mzazi wako.
Mzazi ni ndo Mungu wako wa Pili Kuwa makini
 
Akienda kwenye nyumba ya milele utajua umuhimu wake. Kwa Sasa utoto unao mwingi Sana. Maana hata maelezo yako usemi tatizo unazungumzia hisia tu. Kwanini unagombana na mama. Nataka kuongea jambo baya. Mungu anisamehe bure. Acha kuishi na mzazi yako Kama mpenzi unae lala naye kitandani. Na ndiyo maana unakosa heshima kwa mama yako. Tatizo lipo kwako na Ni kweli hauna upendo wa mama yako.
 
hii imekaa kihisia zaidi, au ni huu ujana ujana foolish age??😅
Kihisia zaidi kwasababu mmekuwa mkirumbana mara kwa mara...kwa hiyo hapo source/mzizi ya unavyojisikia kuhusu mzazi wako ni ugomvi wa mara kwa mara...kukosa amani

Kwenye mahusiano ya kimapenzi ukigombana na mpenzi kila wakati mapenzi huwa yanapungua hadi kuisha,sasa kwa case yako ni ngumu wewe kuacha kumpenda mama yako hata mkigombana mara ngapi...zaidi ya kujihisi hivyo unavyojihisi

Anza kujitibu kwa kuanza na source(ambayo naamini ni marumbano mnayokutana nayo)...ukianza kwa kumsikiliza anachotaka ufanye utakuwa poa sana
 
Mkuu mlivyosuluhisha hayakuisha,,,

Mzee wako bado ana doubt mienendo yako...

Hujaprove kwake umebadilika...

Au,

Anaona uelekeo wa wewe kurudia yale yale uliyokua unayafanya...

Hakuna mzazi asiye na best interests za mtoto wake..

Akiwa mkali,ni sababu hataki uwe failure..

Ni wewe kuwa submissive kwake...akikuambia jambo usimletee ujuaji..

Na usimuonyeshe unarudi kwenye ile michezo michafu uliyokua unafanya...

Trick ni kujifanya umekua mtu mzima, responsible..

Fanya yale vijana wa age yako ambao wako responsible wanafanya...

Akiwa na reassurance kuwa uko responsible atakua na amani,na conflicts zitaisha.
 
hayo yote kawaida tushayasuluhisha,

hii imekaa kihisia zaidi sielewi sababu
Hapo kwenye hisia. Nadhani kuna kitu hujakiweka wazi kwenye maelezo yako na ndicho kinafanya uhisi hivyo ndiyo maana wachangiaji wengine wamekuuliza kama unavuta bangi kwasababu haiwezi tu kuwa eti hujiskii kukaa karibu nae. Kama na wewe hujui tatizo ni nini basi mwenye tatizo ni wewe na sio mzazi wako. Jitafakari
 
Hapo kwenye hisia. Nadhani kuna kitu hujakiweka wazi kwenye maelezo yako na ndicho kinafanya uhisi hivyo ndiyo maana wachangiaji wengine wamekuuliza kama unavuta bangi kwasababu haiwezi tu kuwa eti hujiskii kukaa karibu nae. Kama na wewe hujui tatizo ni nini basi mwenye tatizo ni wewe na sio mzazi wako. Jitafakari
ndio mkuu ndo najaribu kupeleleza
 
Hapo kwenye hisia. Nadhani kuna kitu hujakiweka wazi kwenye maelezo yako na ndicho kinafanya uhisi hivyo ndiyo maana wachangiaji wengine wamekuuliza kama unavuta bangi kwasababu haiwezi tu kuwa eti hujiskii kukaa karibu nae. Kama na wewe hujui tatizo ni nini basi mwenye tatizo ni wewe na sio mzazi wako. Jitafakari
Kwani bangi ina shida gani?
 
Back
Top Bottom