kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,634
- 7,015
Pascal Mayalla ni kweli chadema inahitaji fresh blood ila sio Mwambe,CHADEMA inahitaji fresh blood kama Tundu Lisu ila walichokifanya sio kibaya ni maandalizi ya Tundu lisu kuongoza jahazi
Pascal alichofanya ni akili ya juu mno katika kujaribu kuasa wapiga kura.
Jee wapiga kura watakuwa hawajitambui na kuona kuwa katika mitikisiko ya kukiua chama hakikufa? Nani alipambana kisife wakati huo hadi sasa?
Na jee huyu mgeni ndani ya chama wa chini ya miaka 4 iweje aje na kufikiria kuwa yeye anauwezo wa kukamata nafasi ya juu kabisa ili kukiponya chama chake kipya dhidi ya chama chske cha zamani ambacho majuzi mwenyekiti wake amesema Mwambe anakipenda sana na alifanyiwa mizengwe tuu akaondoka?
Ni sawa na unataka kuoa mke aliyemuacha mumewe sio kwa vile hampendi bali gubu la mawifi ndio limemuondoa huko. Akikutana na mumewe wa zamani chocho basi ni mahaba "kama yote"
Andiko kuna walio lipokea tofauti kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Mmawia, kiukweli wengi humu tunajuana kupitia jf tuu lakini hatujuani in reality, mimi ni very real, sijawahi kuwa CCM, hata wakati nikimpigia debe EL, sikuwahi kuwa CCM wala sijawahi kuwa Team Lowassa, na hata Lowassa alipohamia Chadema, sikuwahi kuwa Chadema, na sasa ni kweli poti wangu ndio yuko kunako, bado sijawahi kuwa CCM, ila tunanokwenda...
P
Mkuu Mmawia kwanza nakubaliana na wewe kuwa kuna wana jf tunajuana in real names na tunajuana kuwa wote ni wana jf lakini hatujuani nani anatumia pen name gani, mimi mwenyewe my two kids are jf members and I don't know the names they use, hivyo inawezekana kabisa mimi na wewe tunajuana in reality, hivyo ningekuomba kuwa mkweli na muwazi kuhusu mimi, jee unavyo nijua in reality mimi nina chama chochote?.Pascal watu wazima hawadanganyani mimi nakujua na wewe unanijua ila sema tu sivizuri kuanza kutambulishana, wewe umeamua kuwa verified user sawa ila tukikutana tunafahamiana vizuri tu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu jamaa kwenye post yake kaweka tahadhalj ya watu kama nyie, na bado mnazidi kuprove yupo sahihi! Kukosoa chadema ni kutafuta ukuu wa wilaya?Mayalla nilikuwa nakuaminia Sana na kusoma makala zako, Ila kwa sasa unaangalia tumbo lako zaidi kuliko kusimamia haki. Endelea tu utaupata ukuu wa wilaya.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Kibaravumbi, naunga mkono hoja, kuna kitu kumhusu Lissu nami nilikisema hapaTundu Lisu ana ujuzi,uthubutu,na ujasiri,ila amepungukiwa na kitu kimoja kikubwa sana- Hana hekma!
Anafaa kuwa chini ya mtu au kupewa madaraka akiwa mzee wa miaka 60
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Mmawia kwanza nakubaliana na wewe kuwa kuna wana jf tunajuana in real names na tunajuana kuwa wote ni wana jf lakini hatujuani nani anatumia pen name gani, mimi mwenyewe my two kids are jf members and I don't know the names they use, hivyo inawezekana kabisa mimi na wewe tunajuana in reality, hivyo ningekuomba kuwa mkweli na muwazi kuhusu mimi, jee unavyo nijua in reality mimi nina chama chochote?.
P
Mkuu Ndumbayeye, binadamu tunatofautiana uwezo na uwezo, mwingine ni mzuri katika kupanga mikakati, mwingine ni mzuri kwa kusema sana, mwingine kwa kuhutubia, mwingine kwa ushawishi etc, na ili kufanikiwa lazima hawa watu wenye uwezo tofauti to work as a team. Chadema ilikuwa na team nzuri, mfano Zitto ana very big convincing power, JJ.Mnyika ni researcher mzuri kujimba data, Lissu ni very powerful speaker, Prof. Kitila Mkumbo ni good strategist, team ya Chadema ilikuwa ikikiwasha kinawaka kama ile list ya mafisadi ya Mwembe Yanga au Moto wa Buzwagi Bungeni. Baada ya kumtimua Zitto, JJ.Mnyika now is nothing, baada ya kumtimua Prof. Kitila Mkumbo, kwa upande wa strategies Chadema is zero kwasababu hamna mtu kama Zitto wala Kitila na Zitto kule kwake pia he is nothing kwasababu kuna viungo hana.ulipoanza kumsiktikia kitla mkumbo kuondoka huu uzi nimeupunguza uzito, hivi pandikizi litafanya kazi kwa bidii?
Sent using Jamii Forums mobile app
@PascalMayalla Rudi kusoma hii comment ya jamaa ina ukweli mtupuPascal Mayalla,
We Paskali acha unafiki, wakati CDM inahujumiwa waziwazi huwa upo kimya, CHADEMA na wapinzani wamefungiwa kufanya siasa karibu mwaka wa 4 sasa wakati Katiba na Sheria ya nchi inaruhusu mbona kalamu yako hatujawahi kuisoma ikiandika uonevu huo.
Unajua kwamba CHADEMA ni taasisi inayojitambua, Kiongozi mkuu wa taasisi ndiyo mboni ya taasisi husika, kuna vetting lazima ifanyike before na pre-agreement nzito na bodi nzima ijiridhishe kwamba huyo anayetaka kuongoza taasisi kashiba nondo, viatu vinatosha na anaendana na philosophy ya taasisi husika.
Sasa huwezi kulala ukaibuka ati unataka kuongoza CRDB benki kisa una Masters ya Uchumi na CPA, hapana mambo huwa hayaendi hivyo.. unajua kila kitu ila kwa sababu unapenda kuandika kuhusu CHADEMA in negative well and good.
Decling stage inaelekezwa kwa mbowe tu mbona haielekezwi kwa ccm 58 yrs in abject poverty? Acheni unafikiMkuu Kaka Mkubwa Wakudadavua, kiukweli sisi wazee hatuupendi kweli uzee due declining stage. Hata mimi mimi baada ya kukata 50+, nywele inapoanza kupiga bati wengi wetu ama wananyoa vipara au wanapiga black, wajukuu walipoanza kutokekelezea na kuitwa babu nikaanza kuona noma, nawambia bora mniite grandpa ni afadhali kidogo kuliko babu!. Rounds zilipoanza kupungua kutoka doze ya 3 kwa siku, daily siku zikaanza kupungua zikianzia 3 times a week, 2 times a week sasa only once a week tena round yenyewe moja, kiukweli unaanza kukosa amani na kuhusi kusaidiwa.
Uzee usikie hivyo hivyo, wakati wazee kwa wenzetu wanajipumzikia, huku kwetu wazee ndio they want more!.
Wazee wawapishe vijana.
P
Wakati huo hukuwa na price tagMkuu Ceftriaxon karibu mitaa hii
Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli
Hakika nimefurahishwa sana na Mwandishi huyu Pascal Mayalla wa kipekee aliyemuuliza swali Rais lenye msingi na hata rais kajibu kwa ubabaishaji. Natafuta clip au mwenye nayo aiweke. Kwanza kaanza kwa kuitaja JamiiForums kwa kusema ni mwanachama mwandamizi wa JamiiForums. Hayo yameelezwa na...www.jamiiforums.com
P
Mkuu Mmawia, wewe usicheke bali funguka tuu kama Paskali humu jf anajifanya hana chama huku in reality huwa akionekana ku randa randa viunga vya Lumumba wewe sema tuu.
CCM wanataka nini?CDM wanachotaka ni ruzuku tu ndo maana wapo tayari kushirikiana na yeyote anayewahakikishia hilo refer alichowaahidi Mamvi.
Nguvu sasa ni kupambana kubaki chama kikuu Cha upinzani kuelekea 2020 na Mbowe ana uzoefu na hilo he deserves.
Do or dieWanabodi,
Kichwa cha habari cha bandiko hili kinajieleza wazi, hili likiwa ni bandiko la swali, kuwa Siku Zote Huwa Nailaumu Chadema Kuwa Hawajitambui na Hawajui Wanataka Nini!. Sasa Kesho Chadema Wanafanya Uchaguzi wa Mwenyekiti, Swali ni Jee Sasa Chadema Wanajitambua?, Jee Wanajua Wanataka Nini?...
Katika Uchaguzi wa Kesho wa Mwenyekiti wa Chadema, Kama Chadema Wanajitambua, Watachagua Kuishi, Lakini Kama Bado Hawajitambui Kama Kawaida Yao, Watachagua Kifo!.
Swali ni Jee Chadema Kuchagua Kifo au Kuishi?. Tusubiri Hiyo Kesho Tuone...
Naanza Bandiko Hili na Declaration, Kisha Naleta Justification
Naomba kuanza kwa declaration of interest, mimi Paskali wa Jeiefu, sio mshabiki, mfuasi, au mwanachama wa chama chochote cha siasa, lengo la declaration hii ni kwa ajili ya manazi wa Chadema waliotamalaki humu JF, ambao ukichangia jambo lolote ambalo hawalipendi, watakushukia kwa kukubeza, kwa vile wewe sio Chadema, mambo ya Chadema, yanakuhusu nini?!, hivyo maneno kama "pilipili usioila inakuwashia nini?" hayawezi kukosekana. Naamini kuna Watanzania wengi kama mimi ambao sio wanachama wa chama chochote cha siasa, na kuna wanachama wa vyama vya siasa ambao wako very objective kwa maslahi ya taifa wakiwemo wana CCM ambao wangependa kuona, nchi yetu inapata credible opposition, kwa huku Bara, Chadema ndicho chama pekee kilichoonyesha angalau kinaweza, ila baada ya kutokea huyu game changer aliyabadili the political game, Chadema imeporomoka na baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kama Chadema hawatafanya the right thing now, they are going to be reduced to nothing. Chadema ikifa, sio hasara kwa Chadema na wanachama wa Chadema tuu, ni hasara kwa Taifa na Watanzania kwa ujumla kwa nchi kurejea chini ya mfumo wa chama kimoja which is not good at all kwa majaaliwa ya mustakabali wa taifa letu.
Justification
Kuna justification kubwa moja kwa mtu ambaye sio Chadema kujadili mambo ya Chadema. Chadema kwa vile ni chama cha siasa na kina wanachama, kuna watu wanadhani Chadema ni private party, interms of usajili na kujiunga hivyo ni mali ya wanachama na viongozi wao pekee, no!, Chadema is a public party, nichama cha umma wa Watanzania, na kinaendeshwa kwa kugharimiwa na tax payers money, hivyo ni public party, kwenye kitu kinachoitwa "private property no right to trespass", hii maana yaye ni mali ya mtu binafsi ina kinga ya kisheria ya kutoingiliwa, na hata katika mienendo na maisha binafsi ya watu wakiwemo viongozi, kuna kinga ya kifaragha, "the right to privacy" ambayo haipaswi kuingiliwa, lakini mtu yoyote, au taasisi yoyote inayolipwa with tax payers money, inapoteza hizo kinga zote mbili za private propery na the right to privacy, the tax payers have all the rights to know the public as well as the private conduct of such entity maana nikodi zao!. Kwa vile Chadema kinaendeshwa kwa ruzuku, hiyo ruzuku ni fedha yako, fedha yangu na fedha yetu as public, hivyo we have all the rights, kujua kila kitu kuhusu Chadema na kutoa maoni yoyote kuhusu Chadema, na ndio maana hesabu za Chadema, zinakaguliwa na CAG.
Hoja za Bandiko hili
Japo Chadema wenyewe hawajikubali na kuukubali ukweli kuwa Chadema hapa kilipofika kama chama kikuu cha upinzani kiko stagnant na graph yake imeanza kushuka kwa kasi ambapo viongozi na wanachama wake wanaojitambua, they are doing the right thing, wengine wanasubiri tuu Bunge livunjwe nao waamue, hivyo wana Chadema kindakindaki wenye misimamo thabiti, walioamua kuifia Chadema, itawabidi wajitambue "Kama Chadema Sasa Wanajitambua, na Wanajua Wanataka Nini, Watamchagua Mwambe, Lakini Kwa Vile Siku Zote Chadema Huwa Hawajitambui, Sijui Sasa Kama Wanajitambua, Hebu na Tusubiri Tuone!".
Hitimisho
Kwanini Mwambe na Sio Mbowe?.
Nanalizia kwa kusisitiza, Mhe. Mbowe hana tatizo lolote bali amefikia point of his optimum, mwisho wa uwezo wake, he can not do anything more than what he can or what he did due to over staying na kuwa over saturated to the point of saturated solution that can take no more that it can, ila pia naelewa mapenzi ya Watanzania kwa viongozi wao, hata Nyerere asingengatuka mwenyewe ile 1985 hakuna mtu angethubutu kumwambia mzee pumzika, hivyo inawezekana wana Chadema bado wana mapenzi makubwa sana na Mhe. Mbowe, kwenye mustakabali wa uhai, survival na sustainability ya chama, wasiangalie mapenzi, waangalie uwezo, ability na capabilities.
Politics is science, inafuata principles of political science, Mbowe alipokea Chadema kikiwa ni chama cha kiharakati, alipaswa aki transform kugeuka chama tawala in waiting. Serikali Kivuli ni government in waiting, ilipaswa kila Waziri akifanya jambo fulani, waziri kivuli ana counters kwa kueleza how wrong the government is wangekuwa Chadema wangefanya nini tofauti but serikali kivuli ya Chadema utaisikia tuu Bungeni but its like it doesn't exist nje ya Bunge.
Namfahamu vizuri Mwambe, huyu sio mwanaharakati ni strategist, baada ya Chadema kumpoteza Prof. Kitila Mkumbo, na ZZK, kiukweli kabisa Chadema is totally empty in terms of strategists, hivyo Mwambe ata i transform Chadema kutoka chama cha kiharakati kukigeuza chama tawala in waiting. Japo umaarufu wa Chadema ni ule uanaharakati wake, chama cha kiharakati kazi yake ni harakati tuu, hakiwezi kwenda Ikulu unless na sisi tufanyie majaribio ikulu yetu!.
You can just imagine kama Chadema hii tunayoiona sasa ndio ingepewa nchi ile 2015, hali ingekuwaje?!, si ingekuwa disastrous, thanks God angalizo hili, limesaidia
Elections 2015 - CHADEMA ikipewa Nchi, Oktoba 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!
Wanabodi, Preamble: Chadema ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo jina tuu, ila uendeshaji wake ni wa kidikteta wa hali ya juu!. Katiba yake inavipengele vya kidikteta vinavyokwenda kinyume cha katiba ya nchi!, hii thread ni ya swali tuu, Hivi Chadema ilivyo, bado haijakabidhiwa nchi, inatoa...www.jamiiforums.com
Namalizia Kwa Lile Lile Swali la Msingi, Kama Chadema Sasa Wanajitambua, na Wanajua Wanataka Nini, Watamchagua Mwambe, Lakini Kwa Vile Siku Zote Chadema Huwa Hawajitambui!...Then Watamchagua Tena Mhe. Mbowe. Swali Jee Chadema Sasa Wanajitambua na Kujua Wanataka Nini?Au Bado Hawajimbui?,
Tusubiri Tuone!.
Nawatakia Wana Chadema, Uchaguzi Mwema wa Kuchagua Ama Kuendelea Kuishi Ama Kifo!.
Paskali