Najiuliza hivi kwanini CEO wengi wa kampuni kubwa duniani ni wahindi au kuna kundi kubwa la wafanyakazi wahindi?

Je mpaka lini? Lakini sisi waAfrika tuna shida mahali ukitaka ukijua sie tuna shida waangalie tunao ishi je wapo tayari kujifunza na sie tuwe top top CEOs?
 
Je mpaka lini? Lakini sisi waAfrika tuna shida mahali ukitaka ukijua sie tuna shida waangalie tunao ishi je wapo tayari kujifunza na sie tuwe top top CEOs?
Kuna stage itabidi tupitie.
Umewaona wahindi wavaa misuli wana vyounda injini, piki piki, transformer nk. Ukiwaona ni watu flan very local ila wanatoa engineering product kubwa. India sio mda mrefu inaenda kuwa industrialized. Sasa sisi waafrika hata hatua ile ya wahindi wavaa misuli hatujafika unategemea tutakuwa CEO kule silicon value.
Mtu hujawahi unda hata kisu, utasimamia nini ? Labda vijana wahamasishane waanzishe vituo vya solution kwa kila kitu. Baadae hivyo vituo vitageuka kuwa hub na kuzaliha kampuni.
Umeona trend ya BYD EV car camp ? Eisee hawaa waishaipita BMW kwa ubora na cost
Gari yao inakupa kila kitu kwa gharama nusu ya BMW, sasa mauzo ya BMW yameanza kushuka.
Unajua nini , BYD ilianza kama kampuni ya kuzalisha battery leo wanashindana na Mjerimani. Ujue jinsi tulivyo na safari ndefu.
But we have to start.
 

"Luka 16: 10-12
Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa. Kama basi, nyinyi si waaminifu kuhusu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli? Na kama nyinyi si waaminifu kuhusu mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?"



Sisi hatuaminiki. Tunapenda kuiba na kupiga deals. Mwanzoni nilifikiri ni hapa nyumbani tu. Kumbe hata nje, kuna watu waliosoma na kuelimika na wanafanya deals.
Kuna siku nilikutana na mate wangu wa A Level amerudi toka ughaibuni. Amefungua restaurant na hakuwa anaonekana kama anataka kurudi alikotoka. Ingawa familia yake yote iko huko nje. Ile restaurant ilikuwa uswekeni sana na haikulingana na status yake kabisa.
Kufuatilia kumbe alikuwa mfanyakazi wa shirika moja. Akawa anawaibia wateja kwa namna nyingi tofauti. Akakamatwa na baadae kufungwa. Haajiriki tena. Alipotoka aliamua kuja kutuliza boli uko ughaibuni wamsahau kidogo. Mwingine aliiba vifaa vya electronics US akaja na mbwembwe za kampuni lakini sasa hivi kalala chali.
In principle
 
Wahindi wanajua kufanya management hasa hawatanii hiyo ni nature yao.. ni kama tunavyowasifia wachaga wakikuyu au wakika kwenye biashara.

We kama ulishasoma management chuo lazima ulisoma vitabu vya Gupta a father of management.

they have built that. We also can build. East Africa, Kenya imeanza kuwa labor supplier wa powerful economies sababu wanaaminika na wanaonekana wamesoma.
Sisi tumelundikana pamoja kama mchele. Deal zetu ni kuiba kwenye tender na kudhulumu watu. Tunasubiria nani afe ili tupande vyeo.
Tumeishiwa maarifa kiasi cha kwamba tumesahau dunia nzima kuna skills hazina watu wa kutosha. Tunaweza kuzifanya.
Philipines iliweza. Tukiamua kuamka kutoka kwenye huu usingizi na kuacha ujinga pia tutaweza. Sisi wote hatuwezi kuwa waajiriwa wa serikali. Tuko wengi sana kuliko nafasi zilizopo.
Tubadilike tena haraka sana
 
Sababu ni moja tu. India ina population kubwa over 1 billion people na wengi wamesoma na kuhitimu vizuri bila ajira sababu taifa lao ni masikini, hivyo competition ni kubwa sana kitu kinachofanya wawe simultaneously cheap na over qualified kwenye field nyingi sana, hasa Technology.

Simple as that.
 
Wahindi wenyewe wa India wanalalamika sana kwa nini China inawaacha wakati hatua za ukuaji wote walianza sawa hata ukiangalia Global fortune 500 China anaongoza akifuatia na U.S India mbali huko.

Wahindi wanalalamika kwa nini wao wakienda nje wanabaki huko huko Canada,U.K hawarudi kwao kuikuza India ni tofauti kabisa na wachina wakienda nje ni lazima mzungu au muafrika alien siku moja.
 
Katika kitu CCM imewakosea sana Watanzania ni kuwapa elimu ya kuombea maji ya kunywa. Hao wahindi na waasia mifumo Yao ya elimu inawaandaa strategically
Naaaaahhh. India ni masikini wa kutupwa, na sehemu kubwa ya nchi yao ina mazingira hovyo kuliko Tanzania.

Strategically gani unaongelea hapa? How to shit in an open field at daytime anonymously?
 

Na wayahudi wako wangapi mpaka watutengenezee miundombinu ya kutuajiri sisi wote?
 
Except wahindi wengi ni smart.
 
Duniani kuna classes:
1. Wazungu - sayansi, ugunduzi
3. Wahindi - Biashara
Waarabu, waafrika Botha na Trump wameshasema sitii neno,
Wahindi biashara? Ushawahi sikia mtu anaitwa Steve Jobs? Bill Gates? Elon Musk? Au unadhani sio wafanya biashara hao?
 
Wahindi biashara? Ushawahi sikia mtu anaitwa Steve Jobs? Bill Gates? Elon Musk? Au unadhani sio wafanya biashara hao?
Hao matajiri sababu ya u genius wao kwenye mambo ya computer na internet siyo wafanya biashara. Unamjua mgunduzi wa Microsoft?
 
Except wahindi wengi ni smart.
Kuwa Manager not necessarily uwe smart, ukiwa chuo masomo ya biashara hili swali huulizwa sana tofauti baina ya Leader na manager.

Manager kazi yake yeye ni ku Execute, streamline operation, kuhakikisha wanapunguza gharama, hawatake risk sana etc.

Unamuweka mhindi Mhasibu ama HR anafanya kazi ile ile ambayo hata mbongo anaweza kufanya sio kazi ngumu, ila atachokupa mhindi cha ziada ni hatokosa kuja kazini, kila siku atakuja, yupo motivated kufanya kazi hatategea sana, productivity inakua ile ile siku ya kwanza ama after few years.

Mtu anaweza kuwa smart balaa, Genious kabisa ila sio motivated, siku ya kwanza anakupa Output nzuri tu ila after some time yupo bored output inashuka etc.

Hapa ndio unaona makampuni mengi yanataka managers.
 
Tanzania tuna successfull entrepreneur kushinda Kenya, tunaishi maisha mazuri kuliko wao. kuajiriwa nje ya nchi sio sifa bali ni kufeli kwa Serikali, unafikiri Nchi kubwa zinajisifia raia wake kuajiriwa Nchi nyengine?

Kuwa na watu kama Bakhresa ni mara 100 bora zaidi kuliko kuzalisha madaktari na wasomi wengine wanao kwenda kutumikia nchi za watu wakati Nchi yako ina taabika.
 
Nikifanikiwa kuianzisha kampuni ya maana, lazima hawa watu wawepo kwenye menejimenti ya kampuni zangu:
1. Wahindi
2. Wakenya

KWA NINI?
1. Wana exposure kubwa
2. Wabunifu
3. Wachapa kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…