Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

Najutia tukio hili: Sikuweza kumsaidia rafiki yangu akajinyonga

Majuto ya kinafiki tu asilimia kubwa wa Tanzania wagumu sana kutoa msaada kwa wanaohitaji msaada hila ukisikia amekufa ndio mnajifanya mnahuzuni na unatoa hela ya kusafirisha msiba wakati marehemu alishakuomba msaada Mara kibao ukakataa wakati uwezo ulikuwa nao na inawezakuwa ungemsaidia ungekua umeokoa maisha yake.
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Kazi yake mola haina makosa
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema,
Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
Pole sana! Inanikumbusha mimi miaka ya 90 mwanzoni. Nilikuwa nisafiri kwenda Dar bahati mbaya siku hiyo ndege ikaahirisha hai kesho yake. Basi ikanibidi nirudi zangu nyumbani. Ilipofika mida ya saa kumi na mja hivi, nikaamua kwenda sehemu kupata kiburudisha koo. Wakati naenda huko nilikutana na rafiki yangu, alikuwa akifanya kazi TRA, akataka niambatane naye, lakini akaghairi baadae kwani alidai ngoja aende kutazama sinema. Nilienda huko nilikokuwa nikienda na majira ya saa mbili usiku nilirudi zangu home. Nikiwa nimelala majira ya saa tano usiku niligongewa mlango, nikambiwa rafiki yako kachomwa kisu yuko hoi hospitali. Alichomwa kisu akiwa kabisa kakaribia nyumbani kwake mida ya saa nne akitoka kutazama sinema. Niliamka nikaongozana na majirani tukaelekea hospitali. Nakumbuka tulimkuta chumba cha daktari juu ya kitanda akiwa anakata roho. Na mimi nikamfunga macho!!!

Hadi leo huwa najilauma na kujiambia endapo ningeongozana naye labda mauti yasingemkuta. Rest in eternal peace my friend T.
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Hembuuuu...?! sasa hii inahusiana nini na kujinyonga kwani JPM alisema anajinyonga na hatukufanya jambo kuepusha?
 
Pole sana! Inanikumbusha mimi miaka ya 90 mwanzoni. Nilikuwa nisafiri kwenda Dar bahati mbaya siku hiyo ndege ikaahirisha hai kesho yake. Basi ikanibidi nirudi zangu nyumbani. Ilipofika mida ya saa kumi na mja hivi, nikaamua kwenda sehemu kupata kiburudisha koo. Wakati naenda huko nilikutana na rafiki yangu, alikuwa akifanya kazi TRA, akataka niambatane naye, lakini akaghairi baadae kwani alidai ngoja aende kutazama sinema. Nilienda huko nilikokuwa nikienda na majira ya saa mbili usiku nilirudi zangu home. Nikiwa nimelala majira ya saa tano usiku niligongewa mlango, nikambiwa rafiki yako kachomwa kisu yuko hoi hospitali. Alichomwa kisu akiwa kabisa kakaribia nyumbani kwake mida ya saa nne akitoka kutazama sinema. Niliamka nikaongozana na majirani tukaelekea hospitali. Nakumbuka tulimkuta chumba cha daktari juu ya kitanda akiwa anakata roho. Na mimi nikamfunga macho!!!

Hadi leo huwa najilauma na kujiambia endapo ningeongozana naye labda mauti yasingemkuta. Rest in eternal peace my friend T.
Mkuu,mambo haya yanaumiza sana moyo,unahisi ungerudisha muda nyuma anagalau ufanye jambo la kumsaidia.Pole sana mkuu!
 
mkuu pole kwa kubeba matatizo yasiyo kuhusu na unatembea nayo na yanakutesa haswaaaa
Kikubwa chukulia ushauri ulompatia ulikuwa sahihi sana ila jua kuwa kuna aina ya waomba ushauri wa aina hii;
1 kuna wale wanaomba ushauri na wako tayari kufanyia kazi ushauri wowote watakaopatiwa, maana huwa hawajui wafanye nini kwa wakati huo
2. kuna wale wanaomba ushauri ilihali wanamitizamo yao na huwa wanataka mtu wa kusarport kwa kile walichokifikiria yani, mtu anaomba ushauri ila anataka mtu ampe ushauri kulingana na jibu(mtizamo) alilo nalo kichwani mwake. mfano mtu anaomba ushauri ila ndani ya nafsi yake anaamini kujiua ndo ufumbuzi wa yotee, kwahiyo ukimshauri tofauti na kujiuo anaona ushauri wako hauna maana na ni ushauri usio na maana

Elewa hilo na chukulia alishakuwa na jibu lake ndani ya nafsi hata ka ungefanya jitihada gani
Asante mkuu kwa maneno yako ya faraja na ya kunizidisha nisonge.Nimejifunza mengi kutokana na kuondoka kwake,nimejifunza nichukue hatua kwa mtu mwingine akinishirikisha jambo kama hili tena.Kusahau ndio imeshindikana mkuu.Namuona hadi leo,nahisi kuna wajib sikuuitimiza katika kumshauri kwangu.
Siku ya tukio nilienda kwenye harusi ya mfanyakazi mwenzangu alikuwa anaoa.Rafiki yangu huyo aliwapigia simu baadhi ya rafiki zake wengine kuwaaga,simu yangu niliisahau nyumbani siku hiyo sikwenda nayo kwenye harusini.Niliporudi alfajiri nilikuta missed calls nyingi sana,lakini kwa vile ni alfajiri ilikuwa nikasema nilale nitapiga kesho yake asubui.12 asubui nikagongewa mlango ya taarifa ya msiba.
Nililia sana,kwenye msiba wake nilmkumbatia mama yake nikalia sana na kumuomba nsamaha.Majibu ya mama yake aliniambia sina cha kuombea msanaha nilikuwa mtu mzuri sana kwa rafiki yangu.Laiti ningepokea ile simu nikaongea naye,laiti angeongea na mimi,labda yasingetokea hayo yote!
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.

Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
Kama alikwisha kufa msamaha unaoumba unapoteza muda wako,mgeukie Mungu wako akuondolee hiyo roho ya kujuta kwani mpaka hapo sioni kosa lako ni nini,wakati aliejiua ndio mwenye kosa mbele za Mungu.Wewe hata ungemshauri asijiue tayari mwenzako alikuwa na roho ya mauti inamfuatilia na kwakuwa hakusimama vizuri kiimani usingeweza kuzuia kujiua kwake...
 
Wakuu Salaam,

Kama kichwa cha habari kinavyosema.

Niliwahi kuwa na rafiki yangu wa karibu sana,alikuwa sio mgonjwa au sikujua anaumwa. Tulikuwa tukikutana ana tabasamu zaidi ya mimi na muda wote alikuwa anafuraha mpaka mimi alikuwa ananishauri akiniona sina furaha.

Siku moja aliniambia anafikiria kujiua sikushtuka nikamshauri kidogo kama vile ushauri wa vijana, wiki mbili baadaye akajinyonga. Nimekaa na hili jambo muda mrefu sana lakini limegomakutoka kwenye nafsi yangu, sina furaha, najilaumu, ninahisi sikutimiza wajibu wangu sehemu fulani ambayo ukiniuliza ni sehemu ipi siijui lakini ninahisi kama rafiki yake nilifeli kumsaidia.

Huu ni mwaka wa 12 sasa naishi kwa maumivu makali sana na sijui nitajitoaje. Je, kuna mtu alishawahi kuwa katika mazingira kama yangu na alisahau vipi akawa na furaha na amani kama zamani?,Mimi nimeshindwa kutojilaumu! popote ulipo Suleiman Nisamehe!

Kama uliwahi kujutia kitu ambacho unahisi ungekifanya na hukukifanya hebu tirirka hapa tuone msaada unaoweza kupatikana.
pole sana, binafsi hakuna kitu huwa kinaniuma kama picha ya Patrick Lumumba mpambanaji wa Zaire, ile aliyopigwa wazungu wakiwa wamemkamata wamemfunga kamba na walikuwa wanaenda kumuua, hakuonekana hadi leo. it really pains, sijui waafrica tulikuwa wapi kipindi hicho. kuna watu wamezipigania sana hizi nchi, kwa damu, na wazungu walitufanyia unyama mkubwa sana.
lumumba one.jpg
lumumba two.jpg
 
pole sana, binafsi hakuna kitu huwa kinaniuma kama picha ya Patrick Lumumba mpambanaji wa Zaire, ile aliyopigwa wazungu wakiwa wamemkamata wamemfunga kamba na walikuwa wanaenda kumuua, hakuonekana hadi leo. it really pains, sijui waafrica tulikuwa wapi kipindi hicho. kuna watu wamezipigania sana hizi nchi, kwa damu, na wazungu walitufanyia unyama mkubwa sana.View attachment 1803578View attachment 1803579
Huyu lumumba alifanya nini mpaka akafa?

Kifo chake kilikuaje?

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Kafungue uzi wa malamiko huko tumechoka wamekufa wangapi hamkusema haya?
 
Ni miaka mingi sasa imepita, mambo mengine hayafutiki akilini ila hakuna namna kubali tu alishaondoka na hatarudi tena.

Hata mfalme Daudi alimlilia mwanaye yule aliyezaa na mke wa huria wakati mtoto anaugua, alipofariki aliacha kulia na akasema it's ok hawezi kurudi tena.

So achana na hilo. Maisha yaendelee.
 
pole sana, binafsi hakuna kitu huwa kinaniuma kama picha ya Patrick Lumumba mpambanaji wa Zaire, ile aliyopigwa wazungu wakiwa wamemkamata wamemfunga kamba na walikuwa wanaenda kumuua, hakuonekana hadi leo. it really pains, sijui waafrica tulikuwa wapi kipindi hicho. kuna watu wamezipigania sana hizi nchi, kwa damu, na wazungu walitufanyia unyama mkubwa sana.View attachment 1803578View attachment 1803579
Inaniuma sana hii na mimi?Huu ni usaliti wa waafrika mkuu!
 
hii kitu usipokuwa makini inaweza kukukuta kama yule mpiga picha kule darfur sudan yaliyompataga
Aliyempiga picha mtoto wakati anahitaji msaada,akamuacha akaliwa na Tai.Picha ile ilimpa umaarufu sana yule bwana.Alikuwa anaitwa Kevin Carter,aliulizwa baada ya kumpiga ile picha mtoto ilikuwaje kilichoendelea?Cha ajabu hakuwa na jibu na ikajulikana jibu ni alimuacha afe,watu wakaunganisha kwamba aliliwa na tai baada ya yeye kuondoka bila kumsaidia!Wazungu Bhana!
 
" Guilty Consciousness "
hali hio watakuwa nayo wanamatusi wa humu na kwengineko dhidi ya ushujaa wa kamanda JPM.

Ina nguvu sana hio kitu itawaandama daima kwa matusi walio na wanayo toa kwa Baba yetu JPM ,its hard to escape from it

watajiona wanahusika moja kwa moja na kifo chake kama ilivyo kwako hapo sasa ( Mtakuja kujionea wenyewe )
Marehemu alikuwa hana utimamu hata umteteeje
 
Back
Top Bottom