Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

Nakaribisha maswali kuhusu Tiba / Dawa

Vipi kuhusu polycystic ovary?
Naweza kushika Mumbai?
Polycystic ovary inatokana kwenye ugonjwa unaoitwa POLYCYSTIC OVARY SYNDROME(PCOS).

Polycystic ovary inaweza kujulikana kupitia kwenye ultrasound na dalili nyingine ambazo nimeziorodhesha chini.Wanawake wote wana follicles kwenye mayai na kila mwezi kundi la follicles linatengenezwa ambalo lina follicle mmoja inayotawala na kupevusha yai.

Wanawake wenye PCOS wanakuwa na follicles nyingi ndogo ambayo hazina uwezo wa kupevusha yai kila mwezi.Na hizi follicles zinashindwa kukua kawaida kutokana na hormonal imbalance.

Na kwasababu yai halipevuki kama linavyotakiwa inasababisha wanawake wenye ugonjwa huu kupata shida kubeba ujauzito.

Ovary(Jinsi follicle inavyopevusha yai)
Utajuaje kama una PCOS
  1. Irregular periods:Siku za hedhi zisizo na mpangilio.Mara nyingi wanawake hawa hupata jumla ya menstruation period 6-8 kwa mwaka.Wanaweza kupata hedhi ya kawaida kwa miezi kadhaa kisha kuruka mwezi au miwili au kuenda miezi kadhaa bila ya kuona siku za hedhi.Watu wenye tatizo hili wanashida kupata mimba kutokana na siku za hedhi kuwa irregular na hata wakishika mimba kuna risk ya hio mimba kutoka.
  2. Kuongezeka kwa andorgens/testosterone(homoni za kiume) mwilini,hii inaweza kuonekana kwenye damu kwa vipimo tofauti au kwa dalili kama kutokwa na chunusi nyingi(ngozi kuwa na mafuta mengi),vinyoleo kukua kwa wingi mf wanawake wanaoota vinyoleo usoni au kifuani.
  3. Polycystic ovaries:hii inaonekana kwenye ultrasound

Cc babuukikolo
uterus.gif
ovary.jpg
 
Natanguliza shukrani kwa msaada unaotoa kwa jamii. Nina tatizo la kutoka vipele sehemu za mikono na miguu, vikipasuka vinakauka na hiyo sehemu inatoa alama kama ya mapunye (mduara), Je mapunye hutokea sehemu yoyote ya mwili ukiacha kichwani? Na dawa gani inaweza kunisaidia?
Hello FORWARD,
Una tatizo linaloitwa POMPHOLYX/DYSHIDROTIC ECZEMA/VESICULAR ECZEMA ni jamii ya upele inayosababisha kutokwa kama malengelenge/vipele vidogodogo kwenye maji vinavyowasha na kuwaka moto kwenye mikono na miguu.Wakati mwengine hivo vipele vidogodogo vinaunganika na kutengeza kama mapachu makubwa ambayo yakianza kupona ngozi inakuwa kavu na kupasukapasuka hatimae kutengeneza kama mapunye.Wakati mwengine hayo malengelenge makubwa yanaweza kupasuka na kusababisha infection au kutokwa kwa usaha.
Mechanism hasa ya ugonjwa huu haijulikani ila kuna vitu vinasababisha au kuchochea hali hio kutokea kama
  • Madini ya cobalt/nikel aidha kupitia kwenye chakula au kwenye ngozi
  • Antibiotic inayoitwa neomycin
  • Makemikali kama perfumes
  • Infection ya fungus kwenye ngozi
  • HIV infection kama opportunistic infection
  • Emotional stress
Tiba ziko za aina tofauti
  1. Siki:Chujua siki kwenye maji utengeneze weak solution,iroweke mikono/miguu kwa dakika 15 kwenye maji hayo,fanya hivo mara nne kwa siku.
  2. Aluminium acetate kwenye maji.Ni unga unachujua kwenye maji kwa ratio ya 1:40,kisha roweka mikono/miguu kwa dakika 15,fanya hivo mara nne kwa siku
  3. Potassium permanganate solution.Inapatikana kama kimimnika au kama crystals/vidonge.Lazima uchujue na rudia kama point 1 and 2
  4. Unaweza kutumia pia topical steroid mfano bethamethasone au clobetasol ili kupunguza inflammation au vidonge(prednisolon) kwa serious case.
  5. Antibiotic inaweza kutumika kama una infection
  6. PUVA THERAPY:ni tiba kwa njia ya mionzi ya UV kwenye ngozi.
  7. Dawa zinazoweza kuaffect immune system ili kupunguza inflammation mfano tacrolimus/pimecrolimus ointment.Vidonge pia vinaweza kutumika mfano alitretionin,methothrexate,azathioprine,cyclosporine ONYO😀awa hizi zina athari nyingi.
 
Polycystic ovarie inatokana kwenye ugonjwa unaoitwa POLYCYSTIC OVARY SYNDROME(PCOS).Polycystic ovary inaweza kujulikana kupitia kwenye ultrasound na dalili nyingine ambazo nimeziorodhesha chini.Wanawake wote wana follicles kwenye mayai na kila mwezi kundi la follicles linatengenezwa ambalo lina follicle mmoja inayotawala na kupevusha yai.Wanawake wenye PCOS wanakuwa na follicles nyingi ndogo ambayo hazina uwezo wa kupevusha yai kila mwezi.Na hizi follicles zinashindwa kukua kawaida kutokana na hormonal imbalance.Na kwasababu yai halipevuki kama linavyotakiwa inasababisha wanawake wenye ugonjwa huu kupata shida kubeba ujauzito.
View attachment 239703
View attachment 239704
Ovary(Jinsi follicle inavyopevusha yai)
Utajuaje kama una PCOS
  1. Irregular periods:Siku za hedhi zisizo na mpangilio.Mara nyingi wanawake hawa hupata jumla ya menstruation period 6-8 kwa mwaka.Wanaweza kupata hedhi ya kawaida kwa miezi kadhaa kisha kuruka mwezi au miwili au kuenda miezi kadhaa bila ya kuona siku za hedhi.Watu wenye tatizo hili wanashida kupata mimba kutokana na siku za hedhi kuwa irregular na hata wakishika mimba kuna risk ya hio mimba kutoka.
  2. Kuongezeka kwa andorgens/testosterone(homoni za kiume) mwilini,hii inaweza kuonekana kwenye damu kwa vipimo tofauti au kwa dalili kama kutokwa na chunusi nyingi(ngozi kuwa na mafuta mengi),vinyoleo kukua kwa wingi mf wanawake wanaoota vinyoleo usoni au kifuani.
  3. Polycystic ovaries:hii inaonekana kwenye ultrasound

Cc babuukikolo

Mimi cjawahi kuvusha mp ingawaje imekuwa irregular..naweza kutumia tiba gani?
 
Last edited by a moderator:
Habari yako.

1. Naomba unisaidie njia ya kitaalamu na safe ya kuondoa tatizo la kusweat sana.

2. Pia tatizo la kuondoa mafuta mengi kwenye ngozi.

3. Nywele zangu nyepesi sana halafu si nyeusi sana. Naomba msaada wa kitaalamu wa kuzifanya ziwe nzito na nyeusi.
Hello Bulldog,

  1. Kwenye hio quote uloniquote nimeweka link ya jinsi ya kuondokana na tatizo la jasho naomba ukaisome.
  2. Umegusia ngozi kuwa na mafuta mengi unamaanisha ngozi ya wapi usoni?Kama husumbuliwi na chunusi unapaswa utumie cleansers tu zinazoendana na aina ya ngozi yako kumaanisha ngozi ya mafuta.Facial cleansers zinasaidia kuondoa dead cells,mafuta na uchafu mwengine kwenye ngozi,zinasaidia pia kufungua pores za kwenye ngozi.Ukishasafisha ngozi inashauriwa utumie Facial Tonic ili kufunga pores za ngozi baada ya kutumia cleanser na baada ya hapo Facial cream ambayo haina mafuta mengi mfano Water based facial cream ni nzuri ili kuipa ngozi unyevyunyevu ili uso usiwe mkavu.Facial mask mara moja kwa wiki wont hurt nilishaona mtu akitangaza mask ya udongo nadhani itakuwa nzuri inasaidia kusafisha ngozi.
  3. Nywele ukitaka ziwe imara unapaswa uzitunze tumia hair mask mfano changanya yai + parachichi na uziloweke au ziloweke na mafuta.Mara nyingi nywele zinabadilika rangi kwasababu ya jua au sababu nyingine ni kwamba si watu wote wana nywele nyeusi sana wengine rangi ya nywele zao ni brown.Nakushauri Vitamin B supplement itakusaidia nywele kuwa imara zaidi.
 
Mimi cjawahi kuvusha mp ingawaje imekuwa irregular..naweza kutumia tiba gani?
Kwa maana hio huna tatizo mkuu!Mabadiliko ya mazingira na ya kimwili,ya kimaisha ,matumizi ya njia za uzazi wa mpango pia yanaweza kusababisha menstruation kuwa irregular.Na kama unashaka sana kuhusu hormonal imbalance nakushauri uende hospitali ukachukue vipimo ili kupata uhakika.
 
Maradhi yangu ni ngozi - ambayo maradhi haya huitwa kwa jina psoriasis - niko nayo
maradhi haya muda mrefu sefu na nimeisha tumia dawa nyingi bila faida.

So naomba muelekezo..
 
Maradhi yangu ni ngozi - ambayo maradhi haya huitwa kwa jina psoriasis - niko nayo
maradhi haya muda mrefu sefu na nimeisha tumia dawa nyingi bila faida.

So naomba muelekezo..
Umetumia dawa gani mpaka sasa?
 
#gorgeousness
reason for being prescribed of this medicine was I had a patch n still it is on skin a round one more darkish (like mtu alovilia dam) compared to my skin It started as a lil one as it is on the one side of my back the time I noticed it thought it would disappear... a time passed likely months if nat a yr ahead I noticed it has increased in size hapaumi wala hapa washi papo tuu.. what could possibly be the problem.
Thank you.
Inaonekana una hyperpigmentation kwenye ngozi na inasababishwa na jua, inflammation au majeraha kwenye ngozi.

Hyperpigmentation inasababishwa na kuongezeka kwa production ya melanin kwenye ngozi.Melanin inatengenezwa kutoka kwenye melanocytes iliyopo kwenye ngozi(epidermis layer).

Utengenezaji wa melatonin unapungua jinsi umri unavyokuwa mkubwa kutokana na melanocytes distribution kupungua.
 
Aibu ni ugonjwa wa kibiolojia au ni tatizo la kurithi? Ni njia gani ya kuondokana na aibu?
Siwezi kusema aibu ni ugonjwa.Ila ikifikia hali inaathiri maisha yako ya kila siku na utendaji wako wa kazi na majukumu tofauti naweza kusema imedevelop kuwa fear au anxiety.Na ndio zipo tiba za fear au anxiety!
 
Nimetumia daivobet sana na canesten na benovate na eliscal creams na elocom na betnovate.
Samahani mkuu hio psoriasis ipo kwenye sehem gani ya mwili??Inaonekana una therapy resistent psoriasis.
Nakushauri ujaribu Acitretin(Neotigason) since umeshatumia glucocorticoids pekee bila mafanikio.Na naona umetumia daivobet pia ni combination ya calsipotriol (Vitamin D[SUB]3[/SUB] analogue)+ bethamethasone(glucocorticoid).
Acitretin(Neotigason) dosage ni 10-75mg per day.Unakula capsule mmoja pamoja na maziwa au chakula.Dawa hii unaweza kuandikiwa na daktari wa ngozi.
Kama psoriasis ni ya mikono then tiba ni Alitretionin(Toctino):30mg per day for 3-6 month.Kwa watu wenye kisukari,high cholesterol,matatizo ya moyo na obesity dosage inatakiwa iwe 10 mg per day.
Acitretin na alitretionin zina precautions zake ni muhimu kutambua hayo kabla ya matumizi hasa kwa fertile women.Zina teratogenic effect.
Kama una psoriasis ya kichwa nakushauri Ditranol.
 
Hellow wapendwa,

Nakaribisha maswali yoyote kuhusu dawa zozote zenye active ingredients (DRUGS). Kama una maswali kuhusu matumizi yake, matumizi yake pamoja na dawa nyingine, vyakula (interactions), athari zake (side effects) au hata kama unataka kujuzwa jinsi dawa inavyofanya kazi kutibu ugonjwa!!

Karibuni sana..
Habari mkuu, mimi ni mwanamme miaka zaidi 30 npo kwenye mahusiano muda sasa paspo kuwa baba. Nilipo fanyiwa uchunguzi wa kimaabara nikaonekana kuwa na tatzo hasa azoospermia!, nikashauriwa kufanya vipimo zaidi hasa kuangalia hali ya vichocheo mwilini hasa FSH, LH na TESTOSTERONE. Na haya ni matokeo ya vipimo FSH 21.42miu/ml, LH 11.63miu/ml na TESTOSTERONE 6.36ng/ml kwa mujibu wa specialist ilionekana uwepo wa tatzo kwa viwango hivi wa vichocheo ( kuzidi kuliko kawaida) na kuonekana suala hili kutorekebishka hapa nchini na kufanya uchunguzi wa kina! kwa kweli sipo vizuri kutokana na majibu hayo na mara tu baada ya kugundulika na tatzo hili, ukizingatia wataalamu wetu hawapo tayari kuulizwa maswali mengi ya kidadisi. tafadhali naomba maelezo ya kina (mechanism) kwa vipi vichocheo vinavyoweza athiri uzalishaji wa mbegu, kama kuna namna yeyote ya kudeal na suala hili hapa nchini, ahsante. Nasubiri.
 
Habari mkuu, mimi ni mwanamme miaka zaidi 30 npo kwenye mahusiano muda sasa paspo kuwa baba. Nilipo fanyiwa uchunguzi wa kimaabara nikaonekana kuwa na tatzo hasa azoospermia!, nikashauriwa kufanya vipimo zaidi hasa kuangalia hali ya vichocheo mwilini hasa FSH, LH na TESTOSTERONE. Na haya ni matokeo ya vipimo FSH 21.42miu/ml, LH 11.63miu/ml na TESTOSTERONE 6.36ng/ml kwa mujibu wa specialist ilionekana uwepo wa tatzo kwa viwango hivi wa vichocheo ( kuzidi kuliko kawaida) na kuonekana suala hili kutorekebishka hapa nchini na kufanya uchunguzi wa kina! kwa kweli sipo vizuri kutokana na majibu hayo na mara tu baada ya kugundulika na tatzo hili, ukizingatia wataalamu wetu hawapo tayari kuulizwa maswali mengi ya kidadisi. tafadhali naomba maelezo ya kina (mechanism) kwa vipi vichocheo vinavyoweza athiri uzalishaji wa mbegu, kama kuna namna yeyote ya kudeal na suala hili hapa nchini, ahsante. Nasubiri.

Ukiona unapewa majibu kama hayo hospitalini ujue hawana cha kukusaidia, na madaktari wa hospitali za kisasa wakishindwa kukuondolea tatizo wataanza kukwambia unatakiwa uende india, marekani, au hata south africa ili mradi tu wamekujibu, hata siku moja hawawezi kukwambia ukatafute tiba kwenye clinic za tiba badala.

Mimi nakushauri nenda kwenye hospital/clinic za tiba mbadala na nina amini utapona tatizo lako, tiba ya kisayansi huku kwetu bado sana.
 
Habari mkuu, mimi ni mwanamme miaka zaidi 30 npo kwenye mahusiano muda sasa paspo kuwa baba. Nilipo fanyiwa uchunguzi wa kimaabara nikaonekana kuwa na tatzo hasa azoospermia!, nikashauriwa kufanya vipimo zaidi hasa kuangalia hali ya vichocheo mwilini hasa FSH, LH na TESTOSTERONE. Na haya ni matokeo ya vipimo FSH 21.42miu/ml, LH 11.63miu/ml na TESTOSTERONE 6.36ng/ml kwa mujibu wa specialist ilionekana uwepo wa tatzo kwa viwango hivi wa vichocheo ( kuzidi kuliko kawaida) na kuonekana suala hili kutorekebishka hapa nchini na kufanya uchunguzi wa kina! kwa kweli sipo vizuri kutokana na majibu hayo na mara tu baada ya kugundulika na tatzo hili, ukizingatia wataalamu wetu hawapo tayari kuulizwa maswali mengi ya kidadisi. tafadhali naomba maelezo ya kina (mechanism) kwa vipi vichocheo vinavyoweza athiri uzalishaji wa mbegu, kama kuna namna yeyote ya kudeal na suala hili hapa nchini, ahsante. Nasubiri.
Hello mkuu,
Gonadotropes(GONADOTROPIN-RELEASING HORMONE)GnRH ni hormone inayozalishwa kutoka kwenye anterior pitutiary iliyopo kwenye hypothalamas(ubongo).Gondotropes inatoa vichocheo vinavyofanya kazi kwenye mfumo wa uzazi wa kike(ova) na wa kiume(testes).FOLLICLE STIMULATING HORMONE(FSH) ni hormone mojawapo inahusika uzalishaji wa mbegu za kiume.LUTENIZING HORMONE (LH)ni hormone nyingeneyo inayochochea interstital cells of leyding zilizopo kwenye testes kusecrete testosterone(hormone ya kiume).
Azoospermia ni ugonjwa unaotokea pale mwanaume anapokuwa hana sperm count zinazohesabika kwenye semen.Huu ugonjwa umegawanyika kwenye makundi makubwa matatu
  1. Pretesticular azoospermia:Kundi hili wanakuwa na hypogondatrope hypogonadisme ambapo hawana release ya kutosha ya gonadotropin-releasing hormone kutoka kwenye ubongo.Wanakuwa na low levels ya FSH,LH na testosterone.Tiba ni kwa gonadotropinderivates/analogue.
  2. Testicular azoospermia:Kundi hili aidha kuna abnormality kwenye testes,mapungufu kwenye uzalishaji wa mbegu za kiume au hata kutokuwepo uzalishaji kabisa.Level za FSH/LH zinakuwa juu na kusababisha Hypergondatrop hypogonadism.Abnormality kwenye testicles inasababisha mbegu kutoweza kupevusha ipasavyo.Testicular retention ni sababu nyingeneyo ambayo watoto wa kiume wanazaliwa nayo.Geminal cells zipo sensitive na temperature na ndio maana mbegu zinakuwa defect na kuharibika kabla hazijafika kwenye korodani.
  3. Posttesticular azoospermia:Kundi hili wanatengeneza mbegu lakini hazitoki through ejaculation.Na wapo wanaozaliwa na mapungufu ya vas deferens(njia ya kutolea ejaculation)(Congenital bilateral absence of the vas deferens) au retrograd ejaculation ambapo mbegu za kiume baada ya kwenda kwenye urethra zinaenda kwenye urinary bladder na kusababisha mbegu kuwepo kwenye mkojo.Tiba ni dexbromfeniramin kwa wenye retrograd ejaculation.
Screenshot_2015-04-03-19-03-14.jpg
View attachment Azoospermia.docx
**Anejaculation:ni uwezo wa kutozalisha mbegu kwa wanaume
**Orichitis:Inflammation kwenye testes inayosababishwa na infection kama STD´s n.k
**Vasectomy:Njia ya kufunga kizazi kwa wanaume
**Epididimytis:inflammation kwenye eneo ambazo mbegu za kiume zinazalishwa na kuegeshwa.Inasababisha maumivu,kuvimba na korodani kuwaka moto.
epididymitis.jpeg

Pretesticular na posttesticular azoosermia vinarekebisihika lakini testicular ni irreversible and permanent.Tiba mojawapo ni kwa IVF(In vitro fertilization) + ICSI(Intro cytoplasmic sperm injection).Ambapo mbegu zinachukuliwa kutoka kwenye testicles na kutumika kuegesha ujauzito.
 
Hello mkuu,
Gonadotropes(GONADOTROPIN-RELEASING HORMONE)GnRH ni hormone inayozalishwa kutoka kwenye anterior pitutiary iliyopo kwenye hypothalamas(ubongo).Gondotropes inatoa vichocheo vinavyofanya kazi kwenye mfumo wa uzazi wa kike(ova) na wa kiume(testes).FOLLICLE STIMULATING HORMONE(FSH) ni hormone mojawapo inahusika uzalishaji wa mbegu za kiume.LUTENIZING HORMONE (LH)ni hormone nyingeneyo inayochochea interstital cells of leyding zilizopo kwenye testes kusecrete testosterone(hormone ya kiume).
Azoospermia ni ugonjwa unaotokea pale mwanaume anapokuwa hana sperm count zinazohesabika kwenye semen.Huu ugonjwa umegawanyika kwenye makundi makubwa matatu
  1. Pretesticular azoospermia:Kundi hili wanakuwa na hypogondatrope hypogonadisme ambapo hawana release ya kutosha ya gonadotropin-releasing hormone kutoka kwenye ubongo.Wanakuwa na low levels ya FSH,LH na testosterone.Tiba ni kwa gonadotropinderivates/analogue.
  2. Testicular azoospermia:Kundi hili aidha kuna abnormality kwenye testes,mapungufu kwenye uzalishaji wa mbegu za kiume au hata kutokuwepo uzalishaji kabisa.Level za FSH/LH zinakuwa juu na kusababisha Hypergondatrop hypogonadism.Abnormality kwenye testicles inasababisha mbegu kutoweza kupevusha ipasavyo.Testicular retention ni sababu nyingeneyo ambayo watoto wa kiume wanazaliwa nayo.Geminal cells zipo sensitive na temperature na ndio maana mbegu zinakuwa defect na kuharibika kabla hazijafika kwenye korodani.
  3. Posttesticular azoospermia:Kundi hili wanatengeneza mbegu lakini hazitoki through ejaculation.Na wapo wanaozaliwa na mapungufu ya vas deferens(njia ya kutolea ejaculation)(Congenital bilateral absence of the vas deferens) au retrograd ejaculation ambapo mbegu za kiume baada ya kwenda kwenye urethra zinaenda kwenye urinary bladder na kusababisha mbegu kuwepo kwenye mkojo.Tiba ni dexbromfeniramin kwa wenye retrograd ejaculation.
View attachment 240208
View attachment 240194
**Anejaculation:ni uwezo wa kutozalisha mbegu kwa wanaume
**Orichitis:Inflammation kwenye testes inayosababishwa na infection kama STD´s n.k
**Vasectomy:Njia ya kufunga kizazi kwa wanaume
**Epididimytis:inflammation kwenye eneo ambazo mbegu za kiume zinazalishwa na kuegeshwa.Inasababisha maumivu,kuvimba na korodani kuwaka moto.
View attachment 240203

Pretesticular na posttesticular azoosermia vinarekebisihika lakini testicular ni irreversible and permanent.Tiba mojawapo ni kwa IVF(In vitro fertilization) + ICSI(Intro cytoplasmic sperm injection).Ambapo mbegu zinachukuliwa kutoka kwenye testicles na kutumika kuegesha ujauzito.

Please mkuu msaada wa haraka mke wangu anasumbuliwa na tosess koo linauma sana! Amechoma sindano hazimsaidii naomba kujua zinasabishwa na nini na tiba yake ni nini zinamsumbua kwa muda mrefu kama 10 yrs!

Huwa zibaibuka mara zinapotea nisaidie dawa ya kutibu kabisa.
 
samahani mkuu hio psoriasis ipo kwenye sehem gani ya mwili??inaonekana una therapy resistent psoriasis.
Nakushauri ujaribu acitretin(neotigason) since umeshatumia glucocorticoids pekee bila mafanikio.na naona umetumia daivobet pia ni combination ya calsipotriol (vitamin d[sub]3[/sub] analogue)+ bethamethasone(glucocorticoid).
acitretin(neotigason) dosage ni 10-75mg per day.unakula capsule mmoja pamoja na maziwa au chakula.dawa hii unaweza kuandikiwa na daktari wa ngozi.
Kama psoriasis ni ya mikono then tiba ni alitretionin(toctino):30mg per day for 3-6 month.kwa watu wenye kisukari,high cholesterol,matatizo ya moyo na obesity dosage inatakiwa iwe 10 mg per day.
acitretin na alitretionin zina precautions zake ni muhimu kutambua hayo kabla ya matumizi hasa kwa fertile women.zina teratogenic effect.
Kama una psoriasis ya kichwa nakushauri ditranol.

takriban nnayo mwili mzima.....na kama unavyosema ninayo na sukari na blood pressure from 2008 natumia dawa... Nakushuru sana mkuu kwa mweelekezo wako mzuri inshaalah mungu akubarik akupe
kheri yako duniani na akhera..

Regards
nasser almazrooei
 
Siwezi kusema aibu ni ugonjwa.Ila ikifikia hali inaathiri maisha yako ya kila siku na utendaji wako wa kazi na majukumu tofauti naweza kusema imedevelop kuwa fear au anxiety.Na ndio zipo tiba za fear au anxiety!

Asante sana kwa uchambuzi murua, endelea kubarikiwa, sasa nn tiba ya anxiety au fear?
 
Back
Top Bottom