Nakubaliana na ndugu Bashe kuruhusu wakulima kuuza mazao popote wanapotaka

Nakubaliana na ndugu Bashe kuruhusu wakulima kuuza mazao popote wanapotaka

Ebu tukumbushe kipindi cha Mwinyi na Kikwete walipofunga mipaka,maana mi sikumbuki kabisa kama ilitokea.

Unamaanisha nini unaposema kufunga mipaka? Tangia lini mipaka ya Tanzania ikawa wazi na wapi ambapo iko wazi?
 
Na kwa akili zenu mnadhani wakulima wanafaidika?

Wanaofaidika ni madalali. Mteja (tajiri) anatoka Dar au nje ya nchi anaenda kijijini kutafuta mazao, madalali wanamdaka wanamwambia we tulia usihangaike sisi tutakutaftia kwa bei nzuri, wao ndo wanawajua wakulima, wanaenda wanawalangua kwa bei wanayo taka wao madalali, wakipeleka bidhaa kwa mteja wanapandisha cha kwao.

Sasa hiyo nimeongelea wale wakulima wa chini kabisa. Hamna faida ya tofauti wanayopata ila middle men ndo wanafaidika. Mkulima ukigoma kutoa mazao kwa bei wanayotaka wanaenda kusambaza mtaani kwamba bidhaa yako haina ubora. So ili visidode mkulima anaamua tu akubali.

Na kumbuka sio wakulima wote wenye uwezo wa kusafirisha mazao yao wenyewe kwenda nje. Wanawategemea madalali. Things are absurd kwa ground
Nakuhurumia Kwa jinsi usivyojua biashara zote duniani zina middle man kuwepo kwa middle man hakuathiri mwenendo wa bei hata hao middle man katika soko huria nao hushindana mwenye bei nzuri kumzidi mwenzie ndie hufanya biashara sana.

Tatizo ni kwamba mkulima akikosa soko middle man anageuka mwokozi kwa kumtafutia soko ila pia soko likiwa zuri middle man asilaumiwe.

Ule ni mnyororo wa thamani. Yaani haiwezekani mkulima akafanya kazi zoote yeye mwenyewe Iko hivyo nyakati zote kwenye biashara ya kilimo.

Hata leo chukua lory la mananasi peleka stereo ni ngumu sana kutana na mlaji wa mwisho lazima ukutane na mtu kati ndiye akuunge Kwa mlaji wa mwisho.
 
Wakulima mnaiwasema hamuwajui.

Sasa hivi wanao uza ni wafanya biashara. Wakulima wananunua vyakula pia.

Nahisi mnaishi nje ya hii nchi.

Waliuza Sasa hivi Wana Lia njaa. Serikali haiwezi kukwepa hii aibu.
Ikiwa Kuna mkulima wa aina hiyo basi ni wale wakulima waliokata tamaa ya maisha na Hana lengo lolote la maisha. Mkulima halisi huuza mazao ili kufidia gharama alizotumia Kwa maana ya kununua pembejeo kuhifadhi akiba na ziada hutumika Kwa matumizi mengine.

Hivyo unapomlazimisha auze Kwa bei ndogo kitakachotokea ni kwamba atakosa hela za kufidia gharama ya kuzalisha itabidi apunguze shamba au aache kulima ageuke machinga na utaratibu huu ukiendelea Kuna mwaka taifa litaagiza chakula chote Toka nje baada ya wakulima kuachana na kilimo na kuhamia kwenye kazi za kijinga tu zinazotabirika.
 
Nakuhurumia Kwa jinsi usivyojua biashara zote duniani zina middle man kuwepo kwa middle man hakuathiri mwenendo wa bei hata hao middle man katika soko huria nao hushindana mwenye bei nzuri kumzidi mwenzie ndie hufanya biashara sana.

Tatizo ni kwamba mkulima akikosa soko middle man anageuka mwokozi kwa kumtafutia soko ila pia soko likiwa zuri middle man asilaumiwe.

Ule ni mnyororo wa thamani. Yaani haiwezekani mkulima akafanya kazi zoote yeye mwenyewe Iko hivyo nyakati zote kwenye biashara ya kilimo.

Hata leo chukua lory la mananasi peleka stereo ni ngumu sana kutana na mlaji wa mwisho lazima ukutane na mtu kati ndiye akuunge Kwa mlaji wa mwisho.
Ungeelewa kwanza nilichomaanisha.

Sijasema middle men hawafai nimewajibu hao wanaokazana kusema bora bei ipande ili wakulima wafaidike ndo nikawajibu hata hao wakulima hawafaidiki kama inavyoonekana huku nje. Wanadhani mchele ukiuzwa 4,400 huku dar basi yule mkulima wa chini kabisa aliuza 2500 per kilo. Unakuta mkulima aliuza gunia la mpunga kwa laki, tajiri analiweka ghalani anakuja kuuza baadae. Sasa mkulima anafaidika vipi na laki? Hiyo 2500 unakuta ni bei ya alienunua kutoka kwa mkulima na sometime wanauza hata zaidi. Wanaofaidika ni middle men na wale wakulima wenye direct access na soko kuu. Sio wale wa chini. Na kwa utafiti wako, large scale Farmers Tanzania unajua wako wangapi? Kwamba umkute mkulima wa ifakara kule anaelima na tractor la kuazima atakua na hata tani tatu ghalani?
 
Ungeelewa kwanza nilichomaanisha.

Sijasema middle men hawafai nimewajibu hao wanaokazana kusema bora bei ipande ili wakulima wafaidike ndo nikawajibu hata hao wakulima hawafaidiki kama inavyoonekana huku nje. Wanadhani mchele ukiuzwa 4,400 huku dar basi yule mkulima wa chini kabisa aliuza 2500 per kilo. Unakuta mkulima aliuza gunia la mpunga kwa laki, tajiri analiweka ghalani anakuja kuuza baadae. Sasa mkulima anafaidika vipi na laki? Hiyo 2500 unakuta ni bei ya alienunua kutoka kwa mkulima na sometime wanauza hata zaidi. Wanaofaidika ni middle men na wale wakulima wenye direct access na soko kuu. Sio wale wa chini. Na kwa utafiti wako, large scale Farmers Tanzania unajua wako wangapi? Kwamba umkute mkulima wa ifakara kule anaelima na tractor la kuazima atakua na hata tani tatu ghalani?
Nimeelewa mantiki yako biashara ikiwa mbaya Kwa middle man hata huyo mkulima mdogo anaumia zaidi ingawa manufaa ya mkulima wa chini hapa ni uhakika wa soko la bidhaa zake
 
Wakati mwingine unaweza kufikiri kwamba Historia ya Tanzania ilianza na Magufuli na kuishia na kifo kwamba hakuna Historia ya Tanzania bila Magufuli kama ukiwasikiliza baadhi ya watu wanaongozwa na emotions badala ya logic, maraisi wote wote wa Tanzania waliopita walizuia uuzwaji wa mazao nje ilipobidi lkn imegeuka ni Magufuli ndiye aliyeanzisha na kuuwa kilimo kana kwamba kabla ya Magufuli kulikuwa na kilimo chochote cha maana ambacho kimeuliwa.

Wakati mwingine intelligence ya watu humu iko chini ya kiwango, kuzuia kuuza mazao nje ni mfumo wa CCM na siyo kwamba ulianzishwa na Magufuli, besides unatumika Dunia nzima hata capitalists kama USA, Europe au hata China hufanya pale inapobidi, huwezi kuexport chakula nje wakati wananchi wanakufa njaa!
Kumbe Marais waliopita walikuwa wanazuia mazao kuuzwa nje? ndio maana kilimo kipo ICU

Samia ndio atakipaisha kilimo cha Tanzania na kukifanya kiwe biashara na ajira nzuri, kwa kuwapa uhuru wakulima
 
Na kwa akili zenu mnadhani wakulima wanafaidika?

Wanaofaidika ni madalali. Mteja (tajiri) anatoka Dar au nje ya nchi anaenda kijijini kutafuta mazao, madalali wanamdaka wanamwambia we tulia usihangaike sisi tutakutaftia kwa bei nzuri, wao ndo wanawajua wakulima, wanaenda wanawalangua kwa bei wanayo taka wao madalali, wakipeleka bidhaa kwa mteja wanapandisha cha kwao.

Sasa hiyo nimeongelea wale wakulima wa chini kabisa. Hamna faida ya tofauti wanayopata ila middle men ndo wanafaidika. Mkulima ukigoma kutoa mazao kwa bei wanayotaka wanaenda kusambaza mtaani kwamba bidhaa yako haina ubora. So ili visidode mkulima anaamua tu akubali.

Na kumbuka sio wakulima wote wenye uwezo wa kusafirisha mazao yao wenyewe kwenda nje. Wanawategemea madalali. Things are absurd kwa ground
Hii hoja mfu inapigiwa bango na watu wasio wakulima na wasiojua hata biashara ya kilimo ipo vipi

Hakuna kuzuia mazao ya mkulima
 
Serikali ikishikilia msimamo huo, na Mimi mwaka huu nalima.

Yaani Kuna majitu yanacheza karata asubuhi mpaka jioni, mkulima anamenyeka shambani, halafu baadae yanataka yake chakula Cha Bure.

Serikali ikikazia hapo, hata wimbi la vijana kuwa bodaboda na kukimbilia mijini litakwisha, utajiri utarudi vijijini.

La msingi ni kuondoa madalali tu
Hakuna soko lisilokuwa na madalali, kanunue hisa kwenye soko la hisa Dar, lazima kuna dalali, kanunue gari Japan lazima kuna dalali, nyumba n.k
 
Hapo wanaofaidika ni middlemen, wakulima wa chini wataendelea na hali zao zilezile kama hawauzi mazao yao kwenye vyama vyao vya ushirika
Wewe ni mkulima ? Usijitie kutetea wakulima kama wewe hulimi, maana unaongea usichokijua
 
Anachofanya bashe na ndio msimamo wa makamu mwenyekiti wa ccm bara kinana ni kuruhusu kuuzwa mazao kiholela ambapo wafanyabiashara kutoka nchi jiradi wanakuja kununua mazao. Nchi inategemea kulishwa chakula na wakulima wake kabla kutegemea nje.

Wakulima wauze chakula kwa yeyote ila inapokua chakula kinapelekwa nje lazima uwepo utaratibu kuhakikisha haitasababisha upungufu wa chakula nchini.

Ni sawa na tatizo lipo kwa viwanda nchini. Tunauza sukari nje na huku tunaagiza toka nje. Hapo ndio utaona ni mpango wa uwekezaji usiolenga mahitaji ya wananchi ila faida na matakwa ya muwekezaji kupata fedha ya kigeni. Hapo pia ndio anaepa kodi kirahisi.
Mkulima hana jukumu la kukulisha wewe, mkulima anatafuta faida kama wafanyabishara wengine wanavyotafuta faida kwa kutafuta masoko mazuri
 
Ungeelewa kwanza nilichomaanisha.

Sijasema middle men hawafai nimewajibu hao wanaokazana kusema bora bei ipande ili wakulima wafaidike ndo nikawajibu hata hao wakulima hawafaidiki kama inavyoonekana huku nje. Wanadhani mchele ukiuzwa 4,400 huku dar basi yule mkulima wa chini kabisa aliuza 2500 per kilo. Unakuta mkulima aliuza gunia la mpunga kwa laki, tajiri analiweka ghalani anakuja kuuza baadae. Sasa mkulima anafaidika vipi na laki? Hiyo 2500 unakuta ni bei ya alienunua kutoka kwa mkulima na sometime wanauza hata zaidi. Wanaofaidika ni middle men na wale wakulima wenye direct access na soko kuu. Sio wale wa chini. Na kwa utafiti wako, large scale Farmers Tanzania unajua wako wangapi? Kwamba umkute mkulima wa ifakara kule anaelima na tractor la kuazima atakua na hata tani tatu ghalani?
Bro Mimi nimeuza ton 30 za mshindi siku chache zilizopita
Dalali alinipigia simu nikampa Bei yangu ni elfu 98 kwa gunia
Yeye kamwambia mnunuzi elfu 99 mia 5
So hapo shida nini
Mimi nimefikia matarajio yangu
Nimeuza mahind
Nimenunua mbolea
Maisha yanaendelea
 
Mkulima hafaidiki, mnufaika ni Dalali
 
Na huuu ndio ukweli usiopingika! Ukweli mtupu yani ukweli ulio uchi!

Mkulima havuni na kuweka ghalani anavuna na kuuza papo hapo kwa walanguzi, walanguzi wanaweka kwenye maghala wanasubiri msimu wa kupanda mazao wanaamua Bei wanayotaka!

Wamechukulia advantage zifuatazo:
1. Rais wa nchi kwa kinywa chake alitamka wazi wazi kuwa lazima bei za bidhaa zitapanda kwahiyo Kuna clear Goa ahead ya kupandisha Bei!

2. Serikali ilishaingiza fedha kwenye mafuta kustabilize Bei wakati gharama za ushafirishaji zilishapanda tayari kwahiyo hakuna kikichoshukq

3. Vita ya Ukraine na Uviko 19 imekua Chaka la kujificha kuanzia waziri wa fedha na wanasiasa wote wenye dhamana.
....
Ko ulitaka Kila kitu kipande ila mazao ya mkulima yashuke bei kwani yeye ana dunia yake?
 
Nimeona humu watu wengi sana wakiishambulia serikali Kwa kutozuia mazao kuuzwa nje ili kupunguza mfumuko wa bei. Ukweli ni kwamba serikali inaweza kuzuia mazao kuuzwa nje.

Jambo hilo ni hatari sana Kwa mustakabali wa kilimo na wakulima wa Tanzania. Gharama za uzalishaji zimepanda sana, kila nyanja ya maisha vitu vimepanda je hayo mazao ya kilimo yakiuzwa bei chini nani atafidia gharama za ziada?

Mwaka ambao nililaani kilimo ni ule mwaka Serikali ilizuia mazao kuuzwa nje eti kwa sababu ya kulinda bei tuliuza gunia shs 30 elfu hata hivyo hapakuwa nawanunuzi. Kuna kipindi serikali ikatutangazia kuwa itanunua mahindi yetu sijui tani ngapi lkn haikusaidia chochote wakulima tukiendelea kusota na mazao.

Likiwa hilo halijapoa serikali ikakosana na wanunuaji wa mbaazi badala yake nikamsika manyanya anasema mbaazi ni tamu sana wakulima kuleni.

Ndugu zangu soko la uhakika na lenye bei nzuri la mazao yote ya kilimo ni muhimu sana kwa uhai na ukuaji wa kilimo kuliko kushinikiza mazao yashuke bei.

Nakumbuka mama alipo apishwa alizinguka sana kwa majirani kuomba waruhusu mazao ya Tanzania yauzwe kwao. Kuna wakati Kenya walisema mahindi yetu yana sumu ilileta maafa Kwa wakulima
Jamaa zetu walisahau kabisa kuwa maridhiano si leseni ya kuwafurahisha CHADEMA wa mjini kwa kuwagandamiza Wakulima. Dhana yao ni kwamba bei ya vyakula itashushwa na tumehuru. Badala ya kuipongeza Serkali kwa kuruhusu wakulima wetu wafaidike kwa bei nono, wao wanatumia hili jambo kisiasa.
ZFZMWCCM
 
Bro Mimi nimeuza ton 30 za mshindi siku chache zilizopita
Dalali alinipigia simu nikampa Bei yangu ni elfu 98 kwa gunia
Yeye kamwambia mnunuzi elfu 99 mia 5
So hapo shida nini
Mimi nimefikia matarajio yangu
Nimeuza mahind
Nimenunua mbolea
Maisha yanaendelea
Dah sijui kwanini watu wanakua wagumu kuelewa. Sasa wewe una tani 30 ndugu yangu mimi naongelea wale small scale farmers mbona tangu mwanzo kabisa wa mada hiyo ndo ilikua point yangu?

Hivi unadhani nchi nzima wakulima wana simu, wana tani 30 ghalani. Sasa basi acha taifa liongelee shida za matajiri wenzao hawa wa chini atawasemea nani? Mimi siwaongelei nyinyi mnalima na mna mishe zinawaingizia hela.

Kuna kulima anategemea heka yake moja tu ndo isomeshe wanae. Hata mimi ni mkulima na muuzaji wa mpunga. Nielezeeje aisee? Au ulitaka tujue kuwa una tani 30 ndani?
 
Back
Top Bottom