Nakukumbusha tena, "acha kubeti" mwisho wa betting sio mzuri

Nakukumbusha tena, "acha kubeti" mwisho wa betting sio mzuri

Betting inamadhara makubwa sana ya kisaikorojia.kifupi kubet kama bahati nasibu nijambo la hatari sana ambalo badae litakupa majonzi makubwa sana.
Kunakijana nimemshuhudia anashinda betting akiwa nanguo za shule nabeg lake mgongoni.
Ukweli hadi leo nimeshindwa kuelewa akila yayule kijana niyanamna gani!
Pia sio betting tuu jalibu kukosea kuoa mke hapo utaingia katika gereza kubwa sna lenye mateso mazito.
Tunayaona nakusikia vifo na mauwaji vitokanavyo na mapenzi nivingi kwatakwimu havina idadi kabisa.
Pombe ulevi kupindukia,madawa yakulevya hivi nivitu vinavyo tafuna sana kizazi kilicho pita,sasa hadi kinacho kuja.
 
Kijana acha kubeti, amua kuachana na utumwa huo bettingi haitakuacha salama

Katika betting sio tu unapoteza pesa bali unapoteza na uwezo wa kufikiri, ubunifu nk

Betting inaweza kuathiri sana akili ya mtu, na mara nyingi athari hizi hujikita taratibu, hivyo kuwa ngumu kugundulika mapema. Athari hizi zinaweza kubadilisha jinsi unavyofikiria, kufanya maamuzi, na hata jinsi unavyothamini mambo muhimu katika maisha yako. Hapa ni jinsi betting inavyoweza kuathiri akili yako:

1. Kuwepo kwa Msongo Mkubwa wa Mawazo

Watu wengi wanaojihusisha na betting huingia katika hali ya wasiwasi kutokana na mawazo ya kushinda au kupoteza. Uzoefu wa kushindwa mara kwa mara unaweza kuathiri sana hali ya kisaikolojia, kuleta msongo ambao hukufanya kuwa na mawazo hasi na mara kwa mara kujihisi huna thamani. Kila unapoendelea kupoteza fedha zaidi, msongo unaongezeka, hali inayoweza kupelekea mawazo ya kujihisi umefeli.

2. Kukosa Dira na Maono katika Maisha

Uraibu wa betting unaweza kufanya mtu kupoteza dira na kutoona fursa nyingine za kujikuza kimaisha. Mtu hujikuta akizingatia sana namna ya kushinda kwenye betting kuliko kuona njia nyingine za kujiongezea kipato. Kwa mfano, unaweza usione fursa za biashara ambazo zingeweza kukuingizia kipato halisi na endelevu. Mtu anaweza hata kuacha kazi au masomo kwa matumaini ya kupata "pesa" kwa kupitia betting.

3. Kujihisi Kukata Tamaa na Huzuni Kali

Kushindwa kwa mara kwa mara kunaleta huzuni na kukata tamaa. Watu wengi wanaopoteza fedha kwenye betting hujilaumu kwa maamuzi yao. Wanaweza kujiona kama watu wasio na bahati, wasio na uwezo wa kufanya maamuzi mazuri, na hii inaweza kuwa na athari kubwa kwa kujithamini kwao. Kwa kuwa betting hujenga matumaini yasiyo na msingi wa uhakika, mtu anaweza kuwa na hali mbaya zaidi ya kukata tamaa kila mara anapopoteza.

4. Kupoteza Udhibiti na Maamuzi Sahihi (Impulsivity)

Betting huchochea hali ya kuamua mambo haraka na mara nyingi bila kufikiria matokeo yake. Hii hufanya mtu kushindwa kuweka mipaka ya kifedha. Mtu anaweza kutumia fedha nyingi ambazo hazikuwa kwenye bajeti, au hata kuingia madeni kwa sababu ya tamaa ya kutaka "kupata mara moja" kupitia betting. Hii ni hatari, kwa sababu hujenga tabia ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi hata nje ya betting.

5. Kuvurugika kwa Mahusiano ya Kijamii na Watu wa Karibu

Betting inaweza kusababisha matatizo ya mahusiano, hasa na familia na marafiki wa karibu. Uraibu wa betting huleta hasira, msongo, na wakati mwingine mtu anakuwa na hatia kwa kutumia fedha ambazo zingeweza kusaidia familia au kutimiza mahitaji mengine muhimu. Mahusiano ya kijamii yanapoanza kuvurugika, unajikuta ukiwa mpweke na kuhisi watu wamekuepuka kwa sababu ya maamuzi yako.

6. Kutoweza Kupanga na Kutimiza Malengo ya Maisha

Betting inachukua muda na rasilimali nyingi, hali inayosababisha kutokuweza kuweka malengo ya muda mrefu na kuyafanyia kazi. Kwa kuwa unapata changamoto ya kujipangia bajeti, inaweza kukufanya kushindwa kuwekeza katika mambo yenye faida ya muda mrefu. Mtu anaweza kushindwa kujiwekea akiba au kufanya maamuzi mazuri ya kifedha ambayo yangemsaidia kuwa na uhuru wa kifedha.

7. Kuathiriwa na Matamanio ya Pesa Za Haraka

Betting hujenga dhana potofu ya kwamba mtu anaweza kupata pesa nyingi haraka. Hii huathiri sana mtazamo wa mtu kuhusu kazi ngumu na bidii ya muda mrefu. Unapojikuta ukitafuta njia za mkato kupitia betting, unakosa fursa za kweli ambazo zinaweza kuleta matokeo bora kwa muda mrefu.

Namna ya Kujinasua na Betting na Kurudisha Hali ya Utulivu wa Kiakili


*Kujihusisha na Shughuli za Kimaendeleo - Tumia muda wako kujifunza stadi mpya, kama biashara au ujasiriamali.


*Kuweka Malengo Madogo na Kufuata Mpangilio wa Bajeti - Kuwa na malengo yanayoweza kutekelezeka na kuwa na nidhamu ya kifedha ni hatua kubwa ya kutoka kwenye betting.
Mwisho kabisa ni kuichukia betting yenyewe
Na wewe umeona umeandika kitu cha maana sana enh!!!acha kupangia watu maisha yao,wanatumia pesa zao hivyo acha kuwashwawashwa kwa andiko la kijinga
 
Betting inamadhara makubwa sana ya kisaikorojia.kifupi kubet kama bahati nasibu nijambo la hatari sana ambalo badae litakupa majonzi makubwa sana.
Kunakijana nimemshuhudia anashinda betting akiwa nanguo za shule nabeg lake mgongoni.
Ukweli hadi leo nimeshindwa kuelewa akila yayule kijana niyanamna gani!
Pia sio betting tuu jalibu kukosea kuoa mke hapo utaingia katika gereza kubwa sna lenye mateso mazito.
Tunayaona nakusikia vifo na mauwaji vitokanavyo na mapenzi nivingi kwatakwimu havina idadi kabisa.
Pombe ulevi kupindukia,madawa yakulevya hivi nivitu vinavyo tafuna sana kizazi kilicho pita,sasa hadi kinacho kuja.
Rubbish
 
Wewe inaonekana ulishawahi kuwa kwenye betting na ukawa master kabisa, ila umeona balaa lake, Kuna kipindi Fulani nilikuwa nafanya tafiti kuhusu hayo mambo lakini sikumaliza utafiti, nilichogundua aisee acha kabisa, vijana kazi hawafanyi zaidi ya kubeti tu, vijiwe vingi TZ wanaongelea hzi ishues si mjini Hadi vijijini ndani ndani hukooo, wanabeti halafu hawana kazi za kufanya au akifanya basi nusu ya pesa inaenda kwenye betting.
 
Uko sawa kabisa mkuu, hayo madhara unaweza ukaona kama hayahusiani na kamari hivi lakini ndio uhalisia ulivyo... Kisaikolojia zaidi

Kamari ina uraibu na uraibu unaathiri mfumo wa ufahamu katika ubongo na kusababisha matatizo ya kisaikolojia, ambayo sio rahisi kuyatambua/kuyashitukia, mapema.

Kitu chochote chenye uraibu kikishafikia hatua hiyo ya uraibu/chronic, iwe ngono madawa pombe kamari inaondoa utimamu wako wakuweza kuamua mambo mwenyewe (self control) badala yake chenyewe ndio kinakuendesha utake usitake, jiulize kwanini walevi, wavuta sigara, unga hawaachi licha ya mateso wanayopata.


Ni moja ya vitu ambayo watu wengi wanakujaga kujifunza muda/umri ukiwa umeshawatupa mkono/ yaani wakiwa wameshachelewa, na hapo ndipo neno ningejua huja mwisho wa safari.
 
amini amin nakuambia.
Umeandika kinyume.
Ieweke tu kwamba betting inaua nguvu za kiume.
Betting ni aina ya ulevi unaokumiliki viungo vyako vyote na hisia.
Ila betting tunapenda kuijadiri kijuu juu mno bila kuelewa aina za betting na uwezekano wa kukosa na kupata na kwa kias gani!
Wanaojua betting na aina zake hawafikirii kuacha bali chaguzi bora za kubet.
Kuanzia aina ya betting, machaguo na kiasi.
Betting inaweza kukupa hadi shinikizo la damu, ugonjwa wa moyo. Unaona timu 15 zimeshinda kwenye mkeka wako bado mbili tayari unajua una milioni kumi, Ile ya mwisho sasa. Moyo unakimbia, tumbo linacheza, kichwa kinauma, kukaa huwezi, kutembea huwezi unapoona unapigwa.

Uchungu, huzuni yake ni kama umefiwa vile.
 
Hiyo bahati ni ya muda tu utashinda ila amini hata hicho ulichojipatia kitarudi huko
Hata mkeo anaweza kurudia huko ulikomtoa kuliwa kimasihara ukaachwa ukapata msongo wa mawazo ukafwaaaa..... Kila mtu ana. Maisha yake usiwapangie Nini Cha kufanya ....Mungu kawaacha HURU wewe nani uwapangie .... Fanya yako
 
Mimi nachokifikilia huu ujumbe umetufikia sisi tu tusio jihusisha na betting lakini wahusika wenyewe wako tayari kumaliza dakika 15 kwenye kusuka mkeka ambao hana uwakika kama ata pata ama kuliwa...kusoma makala kama hizi kiufipi nikwamba hawana mda huo wakupoteza.........😂😂tuombeane uzima tu amna namna
 
kamali ya shambani (kulima) haiwezi kukuathiri kama kama ya mtandaoni
Habari ya shamba n tofauti na izi betting wakubwa......shambani kama uliandaa ili upate gunia 30 za mahindi.....ikitokea wakati wa mavuno hujata gunia 30 bas lazima utapata 10-15. Utasonga mbele kimaisha unajianda n msimu ujao. Ila betting utaweka laki 5 kwenye betting ukiliwa safari ata nusu upati kwanini usiwe kichaaa
 
Wewe inaonekana ulishawahi kuwa kwenye betting na ukawa master kabisa, ila umeona balaa lake, Kuna kipindi Fulani nilikuwa nafanya tafiti kuhusu hayo mambo lakini sikumaliza utafiti, nilichogundua aisee acha kabisa, vijana kazi hawafanyi zaidi ya kubeti tu, vijiwe vingi TZ wanaongelea hzi ishues si mjini Hadi vijijini ndani ndani hukooo, wanabeti halafu hawana kazi za kufanya au akifanya basi nusu ya pesa inaenda kwenye betting.
Yeah, mimi nina uzoefu wa takribani miaka 10 kwenye betting siongei hapa kama motivational speaker tu bali kwa uzoefu wa hali ya juu kabisa
 
Yeah, mimi nina uzoefu wa takribani miaka 10 kwenye betting siongei hapa kama motivational speaker tu bali kwa uzoefu wa hali ya juu kabisa
Kuacha kwako pombe kusikifanye utake wote tuache pombe...ndio hivyohivyo kuacha kwako kubeti usowatake wengine waache wataacha Kwa wakati wao ukifika.
 
Nimeshaacha
 

Attachments

  • Screenshot_20241027-205659.png
    Screenshot_20241027-205659.png
    108.6 KB · Views: 10
Betting inaweza kukupa hadi shinikizo la damu, ugonjwa wa moyo. Unaona timu 15 zimeshinda kwenye mkeka wako bado mbili tayari unajua una milioni kumi, Ile ya mwisho sasa. Moyo unakimbia, tumbo linacheza, kichwa kinauma, kukaa huwezi, kutembea huwezi unapoona unapigwa.

Uchungu, huzuni yake ni kama umefiwa vile.
Uko sahihi.
Lakin kuna kubet kibiashara na kubet kiburudan.
Tofaut yake ni kubet kibiashara ni unastake high kwa odd ndogo sana kama 1.2 kwa 100k or +
Unajikuta kila siku una 30k ya mafuta na lunch nje ya kipato halali.
Kwa wenye na baby walkers
 
Kijana acha kubeti, amua kuachana na utumwa huo bettingi haitakuacha salama

Katika betting sio tu unapoteza pesa bali unapoteza na uwezo wa kufikiri, ubunifu nk

Betting inaweza kuathiri sana akili ya mtu, na mara nyingi athari hizi hujikita taratibu, hivyo kuwa ngumu kugundulika mapema. Athari hizi zinaweza kubadilisha jinsi unavyofikiria, kufanya maamuzi, na hata jinsi unavyothamini mambo muhimu katika maisha yako. Hapa ni jinsi betting inavyoweza kuathiri akili yako:

1. Kuwepo kwa Msongo Mkubwa wa Mawazo

Watu wengi wanaojihusisha na betting huingia katika hali ya wasiwasi kutokana na mawazo ya kushinda au kupoteza. Uzoefu wa kushindwa mara kwa mara unaweza kuathiri sana hali ya kisaikolojia, kuleta msongo ambao hukufanya kuwa na mawazo hasi na mara kwa mara kujihisi huna thamani. Kila unapoendelea kupoteza fedha zaidi, msongo unaongezeka, hali inayoweza kupelekea mawazo ya kujihisi umefeli.

2. Kukosa Dira na Maono katika Maisha

Uraibu wa betting unaweza kufanya mtu kupoteza dira na kutoona fursa nyingine za kujikuza kimaisha. Mtu hujikuta akizingatia sana namna ya kushinda kwenye betting kuliko kuona njia nyingine za kujiongezea kipato. Kwa mfano, unaweza usione fursa za biashara ambazo zingeweza kukuingizia kipato halisi na endelevu. Mtu anaweza hata kuacha kazi au masomo kwa matumaini ya kupata "pesa" kwa kupitia betting.

3. Kujihisi Kukata Tamaa na Huzuni Kali

Kushindwa kwa mara kwa mara kunaleta huzuni na kukata tamaa. Watu wengi wanaopoteza fedha kwenye betting hujilaumu kwa maamuzi yao. Wanaweza kujiona kama watu wasio na bahati, wasio na uwezo wa kufanya maamuzi mazuri, na hii inaweza kuwa na athari kubwa kwa kujithamini kwao. Kwa kuwa betting hujenga matumaini yasiyo na msingi wa uhakika, mtu anaweza kuwa na hali mbaya zaidi ya kukata tamaa kila mara anapopoteza.

4. Kupoteza Udhibiti na Maamuzi Sahihi (Impulsivity)

Betting huchochea hali ya kuamua mambo haraka na mara nyingi bila kufikiria matokeo yake. Hii hufanya mtu kushindwa kuweka mipaka ya kifedha. Mtu anaweza kutumia fedha nyingi ambazo hazikuwa kwenye bajeti, au hata kuingia madeni kwa sababu ya tamaa ya kutaka "kupata mara moja" kupitia betting. Hii ni hatari, kwa sababu hujenga tabia ya kufanya maamuzi yasiyo sahihi hata nje ya betting.

5. Kuvurugika kwa Mahusiano ya Kijamii na Watu wa Karibu

Betting inaweza kusababisha matatizo ya mahusiano, hasa na familia na marafiki wa karibu. Uraibu wa betting huleta hasira, msongo, na wakati mwingine mtu anakuwa na hatia kwa kutumia fedha ambazo zingeweza kusaidia familia au kutimiza mahitaji mengine muhimu. Mahusiano ya kijamii yanapoanza kuvurugika, unajikuta ukiwa mpweke na kuhisi watu wamekuepuka kwa sababu ya maamuzi yako.

6. Kutoweza Kupanga na Kutimiza Malengo ya Maisha

Betting inachukua muda na rasilimali nyingi, hali inayosababisha kutokuweza kuweka malengo ya muda mrefu na kuyafanyia kazi. Kwa kuwa unapata changamoto ya kujipangia bajeti, inaweza kukufanya kushindwa kuwekeza katika mambo yenye faida ya muda mrefu. Mtu anaweza kushindwa kujiwekea akiba au kufanya maamuzi mazuri ya kifedha ambayo yangemsaidia kuwa na uhuru wa kifedha.

7. Kuathiriwa na Matamanio ya Pesa Za Haraka

Betting hujenga dhana potofu ya kwamba mtu anaweza kupata pesa nyingi haraka. Hii huathiri sana mtazamo wa mtu kuhusu kazi ngumu na bidii ya muda mrefu. Unapojikuta ukitafuta njia za mkato kupitia betting, unakosa fursa za kweli ambazo zinaweza kuleta matokeo bora kwa muda mrefu.

Namna ya Kujinasua na Betting na Kurudisha Hali ya Utulivu wa Kiakili


*Kujihusisha na Shughuli za Kimaendeleo - Tumia muda wako kujifunza stadi mpya, kama biashara au ujasiriamali.


*Kuweka Malengo Madogo na Kufuata Mpangilio wa Bajeti - Kuwa na malengo yanayoweza kutekelezeka na kuwa na nidhamu ya kifedha ni hatua kubwa ya kutoka kwenye betting.
Mwisho kabisa ni kuichukia betting yenyewe

Acha wewe haha
Wenzako wanabetia ela ambayo angeenda kunywea pombe

Sio ela ambayo angenunua chakula

Sasa mtu anabet odds kumi Kwa elf 3 ili apate elf 30 atafilisika na nini?

Au hiyo elf tatu angefanyia kitu gani?

Hata Kadi ya mwendokasi hawez kununua Kwa elf 3
 
Back
Top Bottom