Nakusudia kuandika kitabu kuelezea UDIKTETA wa Magufuli

Vitabu kama hivyo huandikwa na watu kama mkuu wa majeshi au usalama wa taifa wa ngazi za juu au mkuu wa polisi wa kipindi husika cha Raisi mhusika sio kaukuta wa barabarani anayeokoteza vitaarifa majalalani
🚮🚮🚮
UONGO mtupu 🙄
Walamba soli za viatu vya dikteta mnateseka sana..
Tulieni kwanza aandike ndo muwe na cha kujadili
 
..by the time jpm anaaga dunia miradi ya sgr na stieglers ilikuwa imekamilika kwa kiasi gani?

..jpm alikuwa na makelele na propaganda nyingi, kwa mtu ambaye hayuko hapa nchini angeweza kufikiria miradi hiyo imekamilika.
Hata wasiotumia akili yao vizuri walitekwa na propaganda zake.
 
Kwa hiyo Biography ya rais inatakiwa kuandikwa na mfalme, au?
Credibility ya kitabu inatokana na weledi & integrity ya mwandishi, siyo cheo..

Siyo kila mwenye ' rank ya juu' ana taaluma ya uandishi!
Sio kweli kitabu chochote cha high profile person cha kwanza unaangalia aliyeandika ni nani? Pili kuna recommendation kule ndani wana recommend hicho kitabu kisomeke ni akina nani wa level ipi?

Mfano kitabu kinaandika kuhusu ujasusi
Kuwa na credibility lazima kiandikwe na jasusi .Kuna kitabu cha ujasusi kinaitwa The economic hitman .Mwandishi alikuwa jasusi wa cheo cha juu sana wa kiuchumi. Na kimeuzika mamilioni ya ma kopi

Huwezi andika kitabu kuhusu Raisi wakati wewe ni mkulima tu wa Namtumbo kisa eti una press card
 
Unasema?
 
Kwani mkulima akiandika maandishi yanafutika?
 
Hata ukiandika hicho kitabu hakitakuwa na maudhui ya kuridhisha kwa sababu mwandishi aliforge cheti cha Form IV.
 
Vinginevyo hakiwi na credibility sababu kitajaa umbeya tu usio na ushahidi
Acha uwongo wako. Zikitumika kumbukumbu za magazeti, mitandao na kuwahoji waathirika kama akina askofu Mwingira, Mo , Roma, Zitto, Kinana, mzee Makamba, Nape, mzee Diallo, Lisu, Membe, askofu Niwemugizi, askofu Kakobe, credibility itakuwa bado tu?
 
Wacha longolongo bhana!
Mbona unarukaruka tu kama maharagwe yanayochemshwa jikoni?!!

Nilidhani ungekuja na biographies za marais kadhaa na waandishi husika. Najua hutafanya hivyo kwa sabb unafahamu unachosimamia hapa ni propaganda tuu.
Kwani ww unafahamu profile ya kila mmoja humu?

Mkuu Sexless, usisikilize kelele za hawa CHAWA wa dikteta akina YEHODAYA, kanyaga mafuta twende😊
 
Acha uwongo wako. Zikitumika kumbukumbu za madaeti, mitandao na kuwahoji wahanga kama akina askofu Mwingira, Mo , Roma, Zitto, Kinana, nzeee Makamba, Nape, Lisu, Membe, credibility itakuwa bado tu?
Hao walikuwa karibu na Raisi? Kumjua kwa undani?
 
Naomba fursa ya kuandika dibaji tu ya kitabu chako. Ili nionyeshe kwa watanzania kuwa CC ya CCM na Jakaya Kikwette kama Mwenyekiti ni watu wa kushtakiwa kwa kutuletea Mrundi mwenye historia ya ugonjwa wa kichaa kuwa mgombea na Kisha Rais wa Tanzania.

Wagombea nafasi ya Urais wawe wanapimwa Afya zao, na TISS wafanye kazi yao kukagua uraia.
 
Yapo mengi sana ya awamu ya nne wanajisahaulisha
 
kwani serikalini si wamejaa vijana sasa hivi mbona hamuwaulizi nn wanafanya kuwasaidia vijana wenzao.Aweso,bashungwa,mazunde,patrobas,nape,makamba,mwanafa,mhagama joseph,hao wote ni vijana na sitaki kutaja wote.je mummewauliza kwa nn hawawapiganii vijana?
 
Je unatafuta ruhusa au unatafuta nini kwa wanajamwi? Kumbuka nchi hii inaruhusu mtu kutoa mawazo yake hadharani kwa njia ya sauti au uandishi na huhitaji uungwaji mkono na mtu yeyote. Fuata sheria za nchi katika uandishi wako upo huru.
 
Titel au Title?
 
Mkuu labda ukakichapa na ukiuze nje ya nchi, hapa Tanzania itakuwa ngumu.
 
Mbona huyo mtu alikuwa ni mchafu tangu akiwa Ujenzi!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…