Uchaguzi 2020 Namba 3: Lazaro Nyalandu achukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia CHADEMA, asema watahakikisha mechi wanaipeleka sawasawa

Raisi wa mashoga
 
Hata Mobutu alikua anasema hivi hivi pia
 
Kaongea vizuri Nyalandu yuko perfect kichwani.
Mr Nyalandu leo nimemuaminia. His ideas are very constructive,kiasi kwamba unasikia mwili kusisimka na kuitamani kuiona Tz ya hivo. Mungu ni mwema atatenda haki na umoja ni nguvu siku zote.
 
Kiukweli Nyalandu kaongea point nyingi sana leo
 
Ni makosa kukata tamaa mapema kabla ya mechi lakini sioni Tume hii ikimtangaza mtu mwingine yeyote zaidi ya Magufuli. Tume hii sio huru na inaongozwa na mwana CCM na matokeo ya urais hayapingwi popote hata kama kuna wizi wa wazi kabisa.

Chadema wanaweza kuendelea na michakato yao kama takwa la demokrasia lakini pia katika ile kuleta hamasa na kusaidia wabunge wa upinzani wengi zaidi wachaguliwe. Ili hili lifanikiwe, mgombea wao apatikane fairly and squarely na mtu yeyote asishinikize kupitishwa yeye/rafiki yake.
 
Sio vibaya kukata tamaa mapema tu ila ni kosa kubwa sana kukata tamaa wakati wowote. Unapokosa utakacho ni hatua moja mbele ya kukipata utakacho.
 
Sawa, tunamtakia Mnyampaa Nyalandu kila la heri kwenye uwendawazimu uliomuingia!!

huyu mnyampaa ni mtu hatari manake kuna stori kuwa wakati akiwa sisiem wale waliokuwa tishio kwake waliogombea nae kura za maoni kuchaguliwa kugombea ubunge kwa ticket ya sisiem kuna wengine walilamba udongo huko Singapore!!

hivi kama si ukichaa ninini? mtu mzima msomi kama Nyalandu unaacha cheo kizuri cha level yako yaani ubunge unavamia urais ambao ni oversaiz? pumbavu kabisa huyu! watu wanauana kutafuta ubunge ye anaacha! ni mtu mwenye dharau sana!!

hivi kwa kazi alizofanya Magufuli , Rais anaekubalika Dunia nzima kwasasa unaanzaje japo kufikiria kwa mbali kupambana nae? si ukichaa huo!! Yaani Francis Cheka akazipige na Tyson yule wa wakati ule hiyo ni akili au matope!!

Kwanza sijui kwanini Nyalandu yuko huru na twiga wetu aliuza Dubai wakiwa hai na hajui hadi sasa tumekosa watalii wangapi wa twiga??huyu ni kiongozi mwenye ubinafsi sana na mpumbavu, hana uchungu na nchi hii!!

Namuonea huruma sana Nyalandu sababu ameshashindwa na Magufuli kabla mbio hazijaanza!!na hajijui!!

Nimwambie ukweli tu Nyalandu na aweke kichwani kuwa unapodhani una akili na sifa za kuendesha mambo zaidi ya boss wako alie madarakani ambae hakwambii purukushani anazopambana nazo basi daima huwezi kuwa na cheo cha boss huyo!!!

he should know and accept that he will never be a president kwakuwa anajiona yeye ni mtu mwenye akili kuliko watu wote bongo kumbe hata ‘Slow times two’ kamzidi kiakili mbali kabisa kwenye siasa hizi za majitaka na kuchafuana!!

zama hizi chama kilianza kufa wakaja na mbinu za kisasa kwanza nunua, akikataa piga katafunua, akiendelea kubisha vunja miguu na mikono akiendelea kupinga juhudi piga risasi akipona mdake mpoteze huku miradi mikubwa ikikonga mioyo ya wapiga kura na bao la mkono at work, Nyalandu atapita njia gani?
 
Tusubiri tuone MTIFUANO ndani ya CHADEMA kuhusu uteuzi huo wa mgombea wao. Na hapo ni kuwa ACT - Wananchi hawajaja na mgombea wao na kutaka kufanya coalition huku Bara kwa nia na lengo la kupata wabunge ili kupata ruzuku for their survival kwani handouts kutoka kwa wafadhili zinaelekea MWISHONI.
 
Kilichonishangaza ni hotuba ndefu aliyoitoa kiasi cha waandishi wa habari kuchoka,
Lakini pamoja nahutuba yte ile hakuruhusu maswali ambayo waandishi walitaka kujua yafuatayo.

1.Alimlipia mbowe nauli yakwenda islaeli km alivyosema lakini waandishi walitaka ufafanuzi kuhusu kulala je walilala chumba kimoja?
Maana alisema usiku wa manane waliamua waende huko kwenye kanisa alilojenga suleimani
Naalitaja hotel waliyolala bila kufafanua je vyumba tofauti?
2.wakati wanaweka vikaratasi waliangaliana na kucheka, kivipi! Maana kwenye maombi kila mtu anakuwa serious na anachoomba
3. Walikuwa kwenye tax moja, wte walikaa nyuma? Au .

Maelezo ya nyarandu yalikuwa na maswali mengi ambayo hayakujibiwa maana ilikuwa ni hotuba hivyo alipaswa aulizwe maswali haya.

Basi atujibu kupitia hapa jf kwakuwa amejileta, bila majibu basi tutaandika chochote.
 
Wagombea wote wa kiti cha urais kupitia vyama vya upinzani wanajua wamepata fursa adimu ya ku-update CV zao kuwa walishiriki uchaguzi mkuu wa 2020.
 
Daah kama mgombea ni huyo ndio amewasilisha upupu wake hivi hafai hata nyumba kumi!
 
ni sawa ila Lissu kiboko ya pombe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…