Zanzibar 2020 Namba 5: Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi achukua fomu kuwania Urais wa Zanzibar

Mkuu Bora huyu awe raisi, amekulia kwenye mazingira ya uongozi, hawa wengine akina kajambakoti wakipewa madaraka ni wasumbufu sana, nadhani mifano unaijua.
Kwani nyie chadema hamtarajiii kushinda urais kule?
 
Ifike wakati tabia ya kurithishana madaraka ya nchi ikomeshwe , Wazanzibar ambao baba zao hawakuwa viongozi hawana haki ya kuwania uongozi ?
Hivi Karume, Jumbe, Mwinyi, Abdulwakiil, Salmin nao baba zao walikuwa viongozi!? Punguzeni basi uchawi enyi kizazi cha ufipa!!
Inamaana mzazi wako akiwa kiongizi,basi na wewe ndio upoteze haki zako za kiraia?

Ushauri huo ungemwambia mzee Mtey aliyempa mkwe wake usultani. Na sultani akaimarisha himaya yake kwa kuruhusu viongozi kuwapa ubunge mahawara, wakwe na ndugu
 
Huyu ndio Rais Mtarajiwa. Yupo nyuma ya system na amekuwa waziri wa ulinzi kwa kipindi kirefu bila kubadilishwa. Tatizo lake ni mpole sana, sio mtu wa maamuzi magumu. Atakuwa kwenye wakati mgumu iwapo wazenji wakikinukisha kuhusu suala la Muungano.
Namtakia kila la kheri
 
Still waters run deep
 
Hatimaye romours za long time zimetokea kweli.

Anyway,wazenji wachague wanaye mtaka
 
Huyu nyumbu watoto wake watarithi chuki,roho mbaya na uchawi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…