Namna wenzetu wanavyoona aibu kuiba mali za Umma

Namna wenzetu wanavyoona aibu kuiba mali za Umma

tang'ana

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2015
Posts
11,931
Reaction score
15,849
Kuna kipindi nilikwenda Japan kwa shughuli flani.

So nikawa nacheck news kwenye television, na uzuri Station niliyokua naangalia ilikua inatumia lugha ya Kiingereza katika kurusha matangazo yake so nilielewa vizuri tu kilichokua kinazungumzwa.

Mtangazaji alitangaza kwamba kuna maiti ya mwanaume mmoja imekutwa kwenye chumba cha hotel, police wakasema mwanaume huyo inasadikiwa aliamua kujiua kwa sababu ya aibu aliyoipata baada ya kugundulika kwamba alitumia fedha kutaka kuwahonga maofisa wa serikali ili aweze kupata tender flani kutoka serikalini.

So nikakumbuka huku kwetu Tanzania mtu anasifika na kuonekana mjanja kwa sababu ya kuiba mali za umma, kumbe huko kwenye nchi za wenzetu ni suala la aibu sana kuiba mali za umma.

Kwa kweli nilijifunza kitu kipya katika maisha yangu na ndio maana wenzetu wanapiga sana hatua za kimaendeleo.
 
Wale jamaa wanafundishwa tangu mwanzo adui mkubwa wa nchi yao ni Rushwa, madawa ya kulevya na uwizi wa Mali za umma. Haya ikija sababu ya umaskini ni izo points uwizi wa Mali za umma na Rushwa.

Hata hukumu zao dhidi ya hayo mambo ni hatar unapotezea soon, pia wale Wana taasisi imara sio mfumo maana mfumo unafavor mtu fulani
 
Wale jamaa wanafundishwa tangu mwanzo adui mkubwa wa nchi yao ni Rushwa ,madawa ya kulevya na uwizi wa Mali za umma ...Haya ikija sababu ya umaskini ni izo points uwizi wa Mali za umma na Rushwa...
Kwa kweli kule kuna tofauti kubwa sana ya maisha.
 
China mtu akiiba mali ya umma serikali itamuua. Japan mtu akiiba mali ya umma atajiua kwa kujiletea aibu yeye mwenyewe na ukoo wake mzima.

Bongo mtu akiiba mali ya umma atasifiwa na jamii na kuitwa mjanja mtoto wa mjini na hatafanywa cho chote kwa sababu amekula kulingana na urefu wa kamba yake!

Halafu tunalalamika kwa nini hatuendelei [emoji706][emoji706][emoji706]
 
So nikakumbuka huku kwetu Tanzania mtu anasifika na kuonekana mjanja kwa sababu ya kuiba mali za umma, kumbe huko kwenye nchi za wenzetu ni suala la aibu sana kuiba mali za umma.
Huku kwetu aibu labda ujambe au ujinyee mbele ya mkutano wa siasa napo utakomaa tu kudanganya wadanganyika
 
Kula kwa urefu wa kamba yako [emoji23] the slogan says watu weusi n changamoto sana
 
Huku kwetu tumefundishwa kuwa maadui wakubwa ni ujinga, umaskini na maradhi.
20230222_190948.jpg
 
Hao jamaa wana strategies zao toka utotoni raia wanafundishwa pia sheria zao ni kali kias kwamba mtu anaona bora ajiue kuliko fedheha ya kunyongwa au kifungo cha maisha!

Sheria zao zinafanya kazi effectively bila kujal ni kiongozi ama ni nan, tofauti na kwetu kwanza katiba haina makali wala kusimamiwa kikamilifu. NB; uzalendo huanzia ngaz za juu na raia watafuata!!
 
Kumbukeni Japan sio jamhuri ya muungano, ni republic! Nchi ambayo ni United republic huwa na matatizo ya rushwa, ufisadi na kutojali. Ili nchi ipate maendeleo ya haraka inatakiwa ihame kutoka United republic kuwa republic! Vinginevyo itabaki maskini milele.
 
Kuna kipindi nilikwenda Japan kwa shughuli flani.

So nikawa nacheck news kwenye television, na uzuri Station niliyokua naangalia ilikua inatumia lugha ya Kiingereza katika kurusha matangazo yake so nilielewa vizuri tu kilichokua kinazungumzwa.

Mtangazaji alitangaza kwamba kuna maiti ya mwanaume mmoja imekutwa kwenye chumba cha hotel, police wakasema mwanaume huyo inasadikiwa aliamua kujiua kwa sababu ya aibu aliyoipata baada ya kugundulika kwamba alitumia fedha kutaka kuwahonga maofisa wa serikali ili aweze kupata tender flani kutoka serikalini.

So nikakumbuka huku kwetu Tanzania mtu anasifika na kuonekana mjanja kwa sababu ya kuiba mali za umma, kumbe huko kwenye nchi za wenzetu ni suala la aibu sana kuiba mali za umma.

Kwa kweli nilijifunza kitu kipya katika maisha yangu na ndio maana wenzetu wanapiga sana hatua za kimaendeleo.
Hiyo hutaiona Afrika na zaidi Tanzania,🤔
 
Back
Top Bottom