Nampongeza Askofu Rugambwa wa Nyaishozi kwa Kuteuliwa kuwa Kardinali Mpya

Nampongeza Askofu Rugambwa wa Nyaishozi kwa Kuteuliwa kuwa Kardinali Mpya

Attachments

  • IMG_2742.jpeg
    IMG_2742.jpeg
    41.2 KB · Views: 1
... wachaga wamekosea wapi? Ndio wanaongoza kwa idadi ya maaskofu, mapadre, masista, mashemasi, n.k. Anyway, uamuzi wa Papa ni alfa na omega; wanavyosema wao signature yake ni mwisho.
wachaga hata awe askofu elements za ukabila ziko palepale, nilitegemea yule askofu mkuu jimbo kuu la Dar Es Salaam Thadeus Ruwaichi angeukwa ukadinali inaonekana ana makandokando. Km wakati akiwa askofu wa jombo katoliki la Mbulu aliondoka na chuo cha ualimu na kuipeleka kwao Kibosho mtu km huyo ana usafi gani.
 
wachaga hata awe askofu elements za ukabila ziko palepale, nilitegemea yule askofu mkuu jimbo kuu la Dar Es Salaam Thadeus Ruwaichi angeukwa ukadinali inaonekana ana makandokando. Km wakati akiwa askofu wa jombo katoliki la Mbulu aliondoka na chuo cha ualimu na kuipeleka kwao Kibosho mtu km huyo ana usafi gani.

Thibitisha maneno yako kwa kuweka ushahidi hapa
 
Hii comment inahuzunisha sana

Kweli Inahuzunisha na inatoa wito kwa wanauoni kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu maswali yafuatayo;

-- KABILA (TRIBE) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?
-- UKOO (CLAN) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?
-- MBARI (RACE) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?

Nahimiza usomaji wa makala ifuatayo; Adrian Southall (1970), "The Illusion of Tribe," Journal of African and Asian Studies, 5.1:28–50. Naweka hapa chini Makala hii.....
 

Attachments

Nilimuuliza yeye mwenyewe swali hilo miaka mitano iliyopita. Akajibu kwamba hana undugu na Kardinali Laureano Rugambwa. Isipokuwa baba yake walikuwa marafiki wa karibu sana na marehemu Kardinali Laureano Rugambwa. Wakati marehemu anatawazwa kuwa Kardinali mjini Dar es Salaam mwaka 1960, baba wa Protase Rugambwa alisafiri kutoka Kagera kuja Dar kuhudhuria sherehe hiyo, akimwacha mama yake Protase hospitali akingojea kujifungua. Akaahidi kwamba kama mtoto atakuwa mwanaume atamwita Rugambwa na atafanya juu chini mpaka naye awe Kardinali kama Laureano. Hayo ndiyo yametimia.

Leta ushahidi wa kuwa Rugambwa kazaliwa Karagwe kwanza ndo mengine yafuate.
Kweli Inahuzunisha na inatoa wito kwa wanauoni kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu maswali yafuatayo;

-- KABILA (TRIBE) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?
-- UKOO (CLAN) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?
-- MBARI (RACE) NI KITU GANI NA SIO KITU GANI?
Kwa tunaomfahamu fika, inahuzunisha na kusikitisha. By the way ile sredi yako kumhusu aliisoma

 
Nilimuuliza yeye mwenyewe swali hilo miaka mitano iliyopita. Akajibu kwamba hana undugu na Kardinali Laureano Rugambwa. Isipokuwa baba yake walikuwa marafiki wa karibu sana na marehemu Kardinali Laureano Rugambwa. Wakati marehemu anatawazwa kuwa Kardinali mjini Dar es Salaam mwaka 1960, baba wa Protase Rugambwa alisafiri kutoka Kagera kuja Dar kuhudhuria sherehe hiyo, akimwacha mama yake Protase hospitali akingojea kujifungua. Akaahidi kwamba kama mtoto atakuwa mwanaume atamwita Rugambwa na atafanya juu chini mpaka naye awe Kardinali kama Laureano. Hayo ndiyo yametimia.
Ndugu yangu, upo sahihi kwa kuongezea:

Mashemeji wangu wanyambo wana kawaida ya kuwapa Watoto wao majina kutokana na events. Hivyo kama ulivyosema, alipewa jina hilo kutokana na tulio la wakati huo lilikuwa ni kusimikwa kwa Cardinal Rugambwa I; yeye jina lake halisi ni Protase Rugambwa Iholana.

Ikumbukwe kawaida ya mapadre huchukua majina mawili ya kwanza. Ndo maana anaitwa Protase Rugambwa mtoto wa Marehemu Prosper Iholana.
 
... wachaga wamekosea wapi? Ndio wanaongoza kwa idadi ya maaskofu, mapadre, masista, mashemasi, n.k. Anyway, uamuzi wa Papa ni alfa na omega; wanavyosema wao signature yake ni mwisho.
Kanisa linaunganishwa kwa damu ye Yesu na sio damu ya kabila.
 
From above quote,
1. Rais wa TEC
2. Askofu mkuu

So hakunaga more seniors huko? You dont answer to nobody since you are a sovereign? Mimi nilifikiri those guys they report to Ruwaichi

Therefore that guy kuwa Cardinal basi Ruwaichi do surrender to the cardinal.
Hakuna Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Tanzania…

Kuna Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania - TEC (Askofu Mkuu Gervas J. M. Nyaisonga) ambaye husaidiwa na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (Askofu Flavian Kasala Matindi)…..Na kuna Mtendaji wa TEC ambaye ni Katibu Mkuu wa TEC (Padre Dr. Charles Kitima)…

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania ni muunganiko/mkusanyiko wa Maaskofu wote Katoliki Tanzania….

Askofu Yuda Thadei Ru’Waichi yeye ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salaam (Metropolitani ya Dar es salaam)…..

Kanisa Katoliki Tanzania lina jumla ya Majimbo Makuu Saba na majimbo 27 (7 ecclesiastical provinces/metropolitan dioceses and 27 suffragan dioceses)

Majimbo makuu saba ni Dar es salaam (Askofu wake Mkuu ni Yuda Thadei Ru’waichi O.F.M.Cap), Mwanza (Askofu wake Mkuu ni Renatus Leonard Nkwande), Arusha (Askofu wake Mkuu ni Isack Amani Massawe), Tabora (Askofu wake Mwandamizi - Coadjuctur Protace Rugambwa ambaye amekuwa elevated kuwa Kadinali), Dodoma (Askofu wake Mkuu ni Beatus Kinyaiya O.F.M.Cap), Songea (Askofu wake Mkuu ni Damian Dennis Dallu) na Mbeya (Askofu wake Mkuu ni Gervas John Mwasikwabhila Nyaisonga).

Kila Askofu ni Kiongozi katika Jimbo lake (hii ni kwa Maaskofu Wakuu Jimbo Kuu-Archbishops na Maaskofu wa Majimbo-Bishops).

Kuhusu cheo/hadhi ya Mwadhama Kadinali ndani ya Kanisa…Kadinali huteuliwa na Papa na huwa ni Cheo cha Maisha yote…Polycarp Kadinali Pengo haitwi Kadinali Mstaafu, Kikanuni Askofu akitimiza miaka 75 hustaafu majukumu yake ya Kiaskofu (ingawa bado huwa na fursa ya kuendelea na majukumu yake ya Kichungaji).

Hivyo Pengo ataendelea kuwa Kadinali mpaka siku yake ya mwisho Duniani. Na kwa sasa yeye anaitwa Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salaam Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.

Hivyo Maaskofu Katoliki wote wakiwemo Makadinali (bila kujali hadhi zao) wanawajibika moja kwa moja kwa Baba Mtakatifu ambaye kwa sasa ni Papa Francis.

Mojawapo ya role ya Kadinali wa Kanisa Katoliki ni kushiriki katika Uchaguzi wa Papa.

NB: Kadinali huteuliwa miongoni mwa Maaskofu Wakuu, Maaskofu na Mapadri…Hivyo hata Padri wa kawaida anaweza kuwa elevated to Cardinal Priest.

Huu ndio ufahamu wangu kidogo…..Nipo tayari kusahihishwa pale nilipoteleza.
 
Back
Top Bottom