Nampongeza Rais Samia kwa kusimama na wakulima kwa kuwaruhusu kuuza mahali popote palipo na Bei nzuri

Kwanza huo mfumuko wa Bei upo Tanzania pekee? Kwa hiyo mkulima ndio maalumu kwa kubeba gharama za mfumuko wa Bei ukitokea?

Kwani yeye Hana haki ya kuneemeka na kufaidi jasho lake? Kwani wewe huoni juhudi za mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani kukabiliana na mfumuko wa Bei hapa nchini? Acha mkulima afaidike na jasho lake
 
Njaa inakuja...
Ni wajibu wako pia kutunza chakula Cha kutosha badala ya kusubiri serikali ikutunzie, lakini pia msimu mpya huoo unaanza hivyo andaa mashamba ya kuja kulima na siyo usubili wakulima wavuje jasho halafu wewe utake kuja kuwapangia Bei zako za kinyonyaji,
 
Inflation inapimwa na bidhaa nyingi, huku bidhaa za chakula zikiangaliwa kwa ukaribu sana, maana ndizo zinazoliwa kwa wingi ukilinganisha na bidhaa zingine.
 
Unajidanganya mzee, wakulima masikini wote walishauza mazao yao pale tu walipovuna, anaefaidika ni yule mtu wa kati mwenye mtaji aliyenunua mazao kwa wakulima kwa bei ndogo
 
Unajidanganya mzee, wakulima masikini wote walishauza mazao yao pale tu walipovuna, anaefaidika ni yule mtu wa kati mwenye mtaji aliyenunua mazao kwa wakulima kwa bei ndogo
Bei ya mazao mwaka huu ilikuwa nzuri Tangia wakati wa mavuno Jambo lililo kuwa tofauti na miaka mingine ambapo Bei ilikuwa chini Sana wakati wa mavuno, lakini siyo wakulima wote huuza mazao yao wakati wa kuvuna, wengi tu hutunza mazao yao nakuyauza wakati wanajiandaa kuaza msimu mpya
 
Kwa hiyo ulitaka kusemaje, unataka mkulima auze kwa hasara , unajuwa Bei ya mbolea mwaka Jana ilivyokuwa?
Inflation inapimwa na bidhaa nyingi, huku bidhaa za chakula zikiangaliwa kwa ukaribu sana, maana ndizo zinazoliwa kwa wingi ukilinganisha na bidhaa zingine.
 
Mkulima hauzi na kufaidika yeye. Kuna watu hapo katikati ndiyo manufaa yote yanaenda kwao.
Hao wapo lakini pia soko lililo la wazi msimu huu lilikuwepo na Bei nzuri ambapo mkulima alipata nafasi ya kuuza mazao yake bila kumtumia au kupitia kwa mtu yeyote yule
 
Nyie ndo mnafanya tununue unga kg 2000tsh....
 
Nyie ndo mnafanya tununue unga kg 2000tsh....
Tanzania imebarikiwa kuwa na ardhi kubwa Sana yenye rutuba , hivyo hujachelewa chukua hatua nenda ushike ujembe utavuna na kupata chakula Cha kutosha mwaka mzima
 
Anayelalamika aende akalime, aende akashike jembe alone, kilimo Ni biashara hivyo haiwezekani kila siku wakulima wawe wakupata hasara
Kweli kabisa wasilalamike. Mimi napendekeza kilo ya unga ifike hadi 10,000/= ili kila mmoja akalime huko!
 
Mkuu, anayefaidika na mazao yake kuuzwa nje ni wale wanaojiita madalali. Mkulima hana chake katika biashara hiyo.
Na ili mkulima afaidike 100% zoezi linatakiwa kuwa endelevu. Bashe anatakiwa kutorudi nyuma kwenye hili. Akisikiliza kelele tu ameharibu. Bora ajiuzulu kuliko kuachana na huu msimamo.
 
Mkulima hauzi na kufaidika yeye. Kuna watu hapo katikati ndiyo manufaa yote yanaenda kwao.
Amekubaliana nao kwa hiyari yake. Na zoezi la kuacha mipaka wazi likiwa endelevu mkulima atafaidika kwa asilimia. Leo funga kesho fungua ni kukaribisha njaa na kuharibu kilimo.
 
Mkuu kwa taarifa nilizo nazo toka kwa mfanyabiashara ni kwamba serikali imezuia kuuza chakula nje ya nchi baada ya bei za chakuka kuwa juu nchini.
Mleta mada anasifia kitu asichojua huku anaponda kitu inachofanya serikali bila kujua.
Katazo ni la kimya kimya.
CC: Lucas mwashambwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…