Nampongeza Rais Samia kwa kusimama na wakulima kwa kuwaruhusu kuuza mahali popote palipo na Bei nzuri

Nampongeza Rais Samia kwa kusimama na wakulima kwa kuwaruhusu kuuza mahali popote palipo na Bei nzuri

Pm nikupe namba za wakubwa uache kujiabisha
Kazi yangu nikuyasema mazuri yote nayoyaona katika uongozi huu wa mh Rais Samia na serikali yake, Kama kuusema ukweli na mafanikio ya serikali hii Ni kujiaibisha Basi niache Niendelee kuaibika kwa kusema ukweli wa mafanikio ya serikali ,
 
Ndugu zangu Sote tunafahamu kuwa secta ya kilimo katika nchi hii imeajiri na kubeba kundi kubwa Sana la watanzania, Ni secta ambayo ndio pumzi ya familia na Kaya nyingi, Ni secta inayotegemewa na watanzania wengi Kama shughuli kuu ya kiuchumi, Ni kimbilio la wengi, Ni ngazi ya wengi, Ni njia ipitayo na kupitisha watu wengi Sana kuinuka kiuchumi, kilimo Ni mgongo uliowabeba watu wengi Sana katika nchi hii, Ni ziwa ambalo kila mtanzania ananyonya , kilimo ni Mbeleko iliyowabeba wengi Sana,Kilimo Ni MAMA Mlezi wa Taifa hili,

Hivyo ukikipuuza kilimo Ni sawa na kuwa umewapuuza watanzania, ukikiacha kilimo Ni sawa na kuwa umewaacha watanzania wanyonge nyuma, ukikinyonya kilimo kibajeti Ni sawa na kuwa umewanyonya watanzania na ukikibana kilimo Koo Ni sawa na kuwa umewabana watanzania Koo na kuwanyima puumzi.

Sote Ni mashahidi namna ambavyo wakulima wa nchi hii kwa miaka mingi tu ambavyo wamekuwa wakipata hasara kubwa licha ya kuwa wamekuwa wakihenyeka na kuvuja jasho mwaka Hadi mwaka, lakini maisha ya mkulima yamekuwa yakibaki na kuwa duni tu kila siku, hii nikutokana na Bei mbaya ambayo mkulima amekuwa akiuza na kuipata, mkulima licha ya kutumia gharama kubwa katika uzalishaji lakini amekuwa akipangiwa Bei ya kuuza na mahali pa kuuza, amekuwa akipewa mashariti ya kwamba hutakiwi kuuza kule na kule na utauza hapa nchini pekee na mipaka ikawa inafungwa,

Hivyo mkulima amekuwa kwa miaka mingi akibeba misalaba ya watanzania wote, licha ya kulilisha Taifa hili lakini mkulima huyu amekuwa akibaki fukara Sana kwa kuwa Hana uamuzi katika kujitafutia na kuuza mahali ambapo soko Ni zuri na Bei ni ya uhakika,

Rais Samia alipoingia na kuapishwa kuwa Mkuu Wa nchi na Amiri Jeshi mkuu amekuja na mtizamo tofauti wa kukifanya kilimo Ni biashara ,hivyo biashara yoyote lazima itoe faida na itafutiwe soko zuri lakini pia kuwe na mipango mizuri yakuifanya biashara inawiri na kushamiri, mh Rais Samia amekataa kufunga mipaka kuzuia mahindi yasiuzwe nje ya nchi, Jambo lililopelekea mkulima kuuza Bei nzuri Sana mwaka huu tangia wakati wa mavuno,, huku mh Rais akihakikisha kuwa chakula kinakuwepo nchini Cha kutosha kwa usalama wetu

Sasa wakulima wanafaidi jasho lao, wanafaidika na juhudi zao, Sasa vijana wanahamasika kujiingiza katika kilimo, Sasa uzalishaji wa kilimo unaongezeka kwa kila mtu , Sasa watu wanaitafuta Aridhi ili walime maana Sasa kilimo kinalipa na hakimtupu mtu, Sasa kilimo kinakwenda kuwa kimbilio lenye matumaini kwetu vijana, Sasa kilimo kinatoa nuru ya kuinuka kiuchumi, Sasa kilimo kinarudi katika mioyo ya watanzania waliokuwa wameanza kukata tamaaa baada ya kuwa wahanga wakupata hasara kila mwaka,

Nataka niwaulize mnaolalamika uamuzi wa mh Rais wetu mpendwa kutofunga mipaka, Hivi mnajuwa adha za kilimo? Hivi mnajuwa gharama za kilimo nyie? Hivi mnajuwa misukosuko ya kilimo nyie? Hivi mnajuwa ugumu wa jembe nyie? Mmewahi kulima? Mmewahi kushika jembe nyie? Mnajuwa hata namna ya kushika mpini wa jembe au jembe la kukokota na ng'ombe? Mnajuwa mkulima anaamka saa ngapi na kulala muda upi? Mnajuwa mwili wa mkulima unapata maumivu kiasi gani? Au kwa kuwa mnaona vitu vikija sokoni tu? Jembe Ni Vita inayohitaji kujitoa kujitolea na kuwa mvumilivu Kama Asikari Jeshi aliye vitani kupigania nchi yake, mkulima amechoka kupata hasara kila mwaka

Muwe na huruma na mkulima jamani, jaribuni kuvaa viatu vya mkulima muone Kama vitawatosha, vitawashinda kwa uzito na ukubwa wake, lazima vitawapwaya na mtavivua tu, Kama mnaona mkulima hastahili kufaidika na jasho lake Basi nendeni nanyi mkalime, nendeni mkashike jembe, msikae tu kunyonya jasho la mkulima huku mkiwa kimvulini

Kazi iendeleee Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu
Ameruhusu Rais au sheria?

Tuanze hapo ili wenye akili tuelewe
 
Unfortunately uhakika mkulima anapata hiyo bei? Au ndo nyie madalali mnatajirika hamjui hata shamba likoje.wafanyabiashara wa nje wasiruhusiwe kwenda vijijini wanununue katika masoko yetu mjini au wilayani na tuhakikishe tunaondoa madalali
 
Unfortunately uhakika mkulima anapata hiyo bei? Au ndo nyie madalali mnatajirika hamjui hata shamba likoje.wafanyabiashara wa nje wasiruhusiwe kwenda vijijini wanununue katika masoko yetu mjini au wilayani na tuhakikishe tunaondoa madalali
Wakulima wengi kwa mwaka huu uliopita waliuza mazao yao kupitia madalali , hata kama bei zilichangamka wengi hawakupata kilichostahili.
Kwa miaka inayokuja sidhani kama kuna mkulima atauza mazao kupitia madalali maana masoko yote wanakouzia hao madalali yanajulikana na bei pia zinajulikana.
 
Hayo ni mapungufu endelevu.
Lazima ujuwe pia kupata soko na kupenya katika soko la mwenzio yaana nchi jirani au ya kigeni inahitaji maelewano mazuri ushirikiano mzuri na ushawishi wa kidiplomasia, kwa hiyo lazima mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani apongezwe Sana kwa namna alivyojenga na kuimarisha ujirani mwema kupitia diplomasia yetu na ushirikiano wetu ambapo Sasa tunaishi Kama ndugu wa karibu, hii ndio sababu inayotusaidia kupata fursa mbalimbali zikiwemo hizi za masoko ya mazao nje ya nchi
 
Lazima ujuwe pia kupata soko na kupenya katika soko la mwenzio yaana nchi jirani au ya kigeni inahitaji maelewano mazuri ushirikiano mzuri na ushawishi wa kidiplomasia, kwa hiyo lazima mh Rais wetu mpendwa mama Samia suluhu Hassani apongezwe Sana kwa namna alivyojenga na kuimarisha ujirani mwema kupitia diplomasia yetu na ushirikiano wetu ambapo Sasa tunaishi Kama ndugu wa karibu, hii ndio sababu inayotusaidia kupata fursa mbalimbali zikiwemo hizi za masoko ya mazao nje ya nchi
Mkuu
Ninaongelea utaratibu unaoruhusiwa. Ni fungate au sheria imepitishwa?
 
Back
Top Bottom