Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?

Kuna mawinga ya kule kariakoo. Yakapewe tin yote yale yalipe kodi.
 
Ni kama amesema large tax payers ndio only tax payers, hawa wengine wanaigiza tu.
Nilidhani alitakiwa ku appreciate na kuwa encourage wengine kulipa kodi sasa yy anatoa maneno ya dharau...haya!!
 
Raisi anaongelea direct tax, Indirect tax kila mtu analipa.
Mleta mada hajaelewa.

Hao 2 mil ni direct tax payers yaani wale TRA akifungua vitabu vyake anawaona.

Indirect tax almost everyone pays.
 
Reactions: Tsh
Wapigaji wanapunguza namba Ili takwimu zisishutukiwe
 
Duh! Ni mhimu kutafuta TIN namba. Imsaidie nini mtanzania wa hali ya chini? Umetumwa na TRA kupiga promo?
We endelea kununua vitu ambavyo receipt inayotolewa inatoa amount tu bila jina siku ukiambiwa hiyo Tv ni ya wizi ndo utajua? Maana ukiambiwa lete ushahidi unaleta Receipt bubu ina jina la bidhaa na amount tu haina jina la mnunuzi hapo ndo utaona umuhimu wake,we endelea kulala
 
Mleta mada hajaelewa.

Hao 2 mil ni direct tax payers yaani wale TRA akifungua vitabu vyake anawaona.

Indirect tax almost everyone pays.
Sio indirect kodi yao haipokelewi na haipo kwenye makusanyo ya serikali

USSR
 
Kuna mawinga ya kule kariakoo. Yakapewe tin yote yale yalipe kodi.
Hkinunua bidhaa au Huduma Kwa machinga utasema umelipa Kodi? Yule hana risiti Wala hatuko registered na VAT na hana TIN namba.

Walau akiwa na TIN ila hayuko kwenye VAT anatakiwa alipe Kodi ya kukadiriwa withholding tax.

Ndio maana sio Kila unaponunia bidhaa au Huduma useme umelipa Kodi,hapana hujalipa.
 
Reactions: Tsh
Mleta mada hajaelewa.

Hao 2 mil ni direct tax payers yaani wale TRA akifungua vitabu vyake anawaona.

Indirect tax almost everyone pays.
Si ndio, hili jambo kamishina alishaliongea likaleta mjadala ila still naona bado halieleweki.

Hizi kodi za manunuzi kila mtu analipa, kila mtu si anafanya manunuzi? Mkurugenzi wa benki akinunua mkate si analipa kodi? Akiweka mafuta si analipa kodi? Ila akipokea mshahara anakatwa kodi ya mshahara. Sasa kodi inayoongelewa ni hii kodi ya mshahara.

Kwa ufupi anasema ajira ziongezeke, ujasiriamali uongezeke na ule usio rasmi urasimishwe.
 
Nilidhani alitakiwa ku appreciate na kuwa encourage wengine kulipa kodi sasa yy anatoa maneno ya dharau...haya!!
Actually yeye kama kiongozi ni kosa lake nchi kuwa na walipa kodi wakubwa wachache.

Ameshindwa kazi ya kupandisha uchumi na kuongeza walipa kodi wakubwa.
 
Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza kinene...

hata hivyo,
nadhani somo na darasa la kodi, tozo na ushuru vinahitajika sana miongoni mwa familia hii pana sana ya JF, lakini pia kwa waTanzania wote kwa ujumla. Vinginevyo kupotoshana kunaweza kuongeza kuchanganya mambo na kuleta migawanyiko isiyo na tija katika uelewa wa jambo hili muhimu sana kwa usitawi wa Taifa letu.

Lipa kodi kwa ujenzi wa Taifa 🐒
 
Mh Rais Samia anasema kodi hazifiki hata tukilipa hizo direct bado kuna shida


USSR
 
Ishu ni kiwa tin au kulipa kodi je anayelipa bila TIN namba kodi yake haipokelewi na haijumuishwi kwenye pato la serikali

USSR
Kuna bidhaa chache sana ambazo unaweza lipa Kodi bila kusajiliwa mfano kama umeenda kununua bidhaa dukani Kwa yule ambae ni VAT registered na akakupa risiti hapo umelipa ila hiyo itasomeka.kwa.muuzaji yaani atapeleka return Kila robo.

Asipokupa risiti hujalipa Kodi hapo ila jmemnufaisha yeye.

Pia Kuna wale ambao ni producers kabisa walistahili.kulipa Kodi na hawalipi mfano mafundi wanapewa kazi mtaani,wakulima,wafugaji wanauza mifugo minadani au majumbani nk.

Kiufupi Kila mwenye idadi Fulani ya mifugo awe analipa Kodi au kuwe na utaratibu utakaoratibu mauziano kuanzia Vijijini huko Ili ukiuza tuu ulipe kodi ya withholding tax.
 
Mkuu, Bidhaa zina kodi zile zilizo silent zinazoanzia viwandani au bandarini na kuhamishwa mpaka kwa mtumiaji . Hivyo kwenye manunuzi kuna kodi ila sio kodi rasmi ya kujivunia kuwa unalipa kodi sababu Hii ni ya woote mpaka wazee walizozeeka wakinunua tumbaku za kiko wanalipa, hutakiwi kutoka mbele ukajivunia nayo wakati wenzako wanakatwa mishahara yao na wanalipa hizo kodi pia.
 
Fundi akilipwa kwa mpesa anakuwa amelipa akinunua Luku na maji analipa kiufupi lazima anachangia tu

USSR
 
Kwa hapo anaehesabika ni mlipakodi ni producer sio wewe maana yeye ndio anauza Kwa whole sellers.

Whole sellers anaweza kukuuzia wewe na ukanunua ukijua umelipa.kodi.kumbe hapana.Bila risiti hakuna Kodi umelipa Mzee labda zile ambazo unaona directly kama Huduma za simu,Mafuta nk..

Dai risiti ndio umelipa Kodi , otherwise Kuna producers wengi tuu kwenye informal sector hawalipi Kodi.
 
Reactions: Tsh
Fundi akilipwa kwa mpesa anakuwa amelipa akinunua Luku na maji analipa kiufupi lazima anachangia tu

USSR
Nani anaekubali alipwe kwenye m pesa au Benki Ili akatwe? Hapo ni kama mtoa pesa Yuko mbali ,harafu kama hela ni nyingi hawamkubali ukazitoa chap Kwa mara Moja Benki ndio maana watu wanafanya miamala Kwa Fedha mbichi.
 
Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?
Je Zanzibar wako wangapi kati ya hao 2 million?
 
Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?
Je Zanzibar wako wangapi kati ya hao 2 million?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…