Elvis Legacy
JF-Expert Member
- Aug 10, 2017
- 3,984
- 5,820
Habari wakuu.Miaka ya nyuma kidogo tulisoma magazeti, tena kila habari kuanzia za siasa michezo hadi vibonzo bila kusahau matangazo.
Nakumbuka miaka ile, mzee alikuwa akija na magazeti ya Nipashe, Majira na Mwananchi kila alipotoka kwenye mihangaiko. Hii ilitujengea hamasa ya kupenda kusoma tukiwa nyumbani, maana, Magazeti ndio yalikuwa na mambo mapya tofauti na vitabu vya hadithi ambavyo tulivosoma na kuvirudia mpaka tukavichoka.
Siku hizi watoto wa familia nyingi hawana tena desturi ya kusoma magazeti maana wazazi hawana utamaduni wa kununua na kuyapeleka nyumbani, hata vijana wa leo wengi hatusomi magazeti wala hatuna source yoyote ya hard news ambazo tunasoma kila siku. Badala yake tumejikita zaidi na taarifa za kwenye social media ambazo hazijahaririwa wala hazina hata chanzo makini cha habari husika. Baada ya hapo tunapitia 'comments' na kujadili kila mtu kulingana na alivyoielewa au anavyotafsiri kama apendavyo.
Je hili jambo lina afya kwa kizazi kijacho? Sijaangazia kusikiliza taarifa ya habari ambapo zamani kulipewa umuhimu kwenye runinga za majumbani. Ndio kusema magazeti, redio na runinga zimepitwa na wakati. Cha kushangaza bado miswada ya sheria na matangazo muhimu ya serikali yanapatikana kwenye magazeti. Nini kifanyike?
Nakumbuka miaka ile, mzee alikuwa akija na magazeti ya Nipashe, Majira na Mwananchi kila alipotoka kwenye mihangaiko. Hii ilitujengea hamasa ya kupenda kusoma tukiwa nyumbani, maana, Magazeti ndio yalikuwa na mambo mapya tofauti na vitabu vya hadithi ambavyo tulivosoma na kuvirudia mpaka tukavichoka.
Siku hizi watoto wa familia nyingi hawana tena desturi ya kusoma magazeti maana wazazi hawana utamaduni wa kununua na kuyapeleka nyumbani, hata vijana wa leo wengi hatusomi magazeti wala hatuna source yoyote ya hard news ambazo tunasoma kila siku. Badala yake tumejikita zaidi na taarifa za kwenye social media ambazo hazijahaririwa wala hazina hata chanzo makini cha habari husika. Baada ya hapo tunapitia 'comments' na kujadili kila mtu kulingana na alivyoielewa au anavyotafsiri kama apendavyo.
Je hili jambo lina afya kwa kizazi kijacho? Sijaangazia kusikiliza taarifa ya habari ambapo zamani kulipewa umuhimu kwenye runinga za majumbani. Ndio kusema magazeti, redio na runinga zimepitwa na wakati. Cha kushangaza bado miswada ya sheria na matangazo muhimu ya serikali yanapatikana kwenye magazeti. Nini kifanyike?