Elections 2015 Nani hatari zaidi kati ya malaika aliyegeuka shetani, Au shetani aliyegeuka malaika?!

Elections 2015 Nani hatari zaidi kati ya malaika aliyegeuka shetani, Au shetani aliyegeuka malaika?!

Dudus?Kwa uelewa wako Shetani ni kitu/kidudu au kiumbe gani?

Habari za Shetani hizi hapa:

"... Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka mkubwa, naye joka mkubwa na malaika zake wakapigana 8 lakini hakushinda, wala mahali hapakupatikana mbinguni kwa ajili yao tena. 9 Kwa hiyo yule joka mkubwa akatupwa chini, yule nyoka wa zamani, yeye anayeitwa Ibilisi na Shetani, anayeipotosha dunia nzima inayokaliwa; akatupwa chini duniani, na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye."; Ufu 12

Kwa ufupi, Shetani ni nafsi iliyo hai, inayojitegemea, yenye utashi, na maamuzi yake yenyewe. Umenisoma?
 
Hadithi yako haina mashiko yakutosha,kwasababu hakuna jambo ambalo mtu anaweza kujifunza juu ya hadithi hiyo, kwa upeo wangu wakuelewa, nimeelewa hivi "unataka kuaminisha umma ya kuwa mtu akifanya makosa baadae anaweza kubadilika na kuwa mtu safi" NI KWELIi, lakini msamaha wa mungu mpaka uwe malaika ni lazima ukiri juu ya hayo mabaya uliyofanya, kuwafuata na kuwaomba radhi wote ambao umewakosea, na kuwarudishia wote ambao ume wadhulumu. Je huyo ambae wewe unae taka kuaminisha umma amekua malaika ameyafanya hayo yote au ana zuga zuga tuh kwa alio wafanyia makosa na kuwadanganya na hadithi za juma na uledi. Tubadilike Watanzania tuwe makini juu ya mambo ambayo yanaweza kuleta madhara makubwa sana katika Taifa letu..Tafadhali fanya maamuzi sahihi huyo shetani ni SHETANI TUh NA SIO MALAIKA kwa sababu bado ana endelea na tabia zaki shetani,
 
Pasco,hata Mtakatifu Paulo alikuwa muuaji wa wakristu akiitwa SAULI,hivyo vyote vya wezekana kwa Mungu.Ila badala ya hii ya Shetani na Malaika.bora ungeiweka hii ya SAULI kuwa PAULI.

Pole Mungu ndiye ahukumuye kwa HAKI.

Kwa sasa nikipiga akili MASWALI ni mengi kuliko majibu.

Sawa kabisa!
 
bora shetani kugeuka kuwa malaika si unaona mwenyewe shetani anavyotutenda si alikuwa malaika tena kipenzi cha MUNGU
 
Eti umesema kuna mashetani wanatubu kwa Mungu alafu wanakua malaika tena???? Heheheh haitakaa ikatokea milele
 
Wanabodi,

Leo tena naendelea na zile nakaa zang za malaika na shetani.

Kwa wasomaji wapya katika kukumbushaba tuu, hapo hapo mwanzo, shetani alikuwa malaika kabla hajawa shetani, tena ndio alijua malaika Mkuu! .

Kwenye himaya ya mashetani shetani hayuko peke yake, yuko na wale malaika wengine waliojiunga nae ambao sasa wote ni mashetani wengine walioamua kujiunga nae.

Katika la jeshi la malaika wa mbinguni from time to kuna baadhi ya malaika huwa wana defect na kumfuata shetani na huo hugeuka mashetani.

Vivyo hivyo kwenye jeshi la shetani kuna mashetani huwa wanatubu na kumrudia Mungu hivyo hurejea na kuwa malaika. Hawa sasa ni harmless kwa sababu ushetani wao wote wana kuwa wameuacha kyle ushetanini!.

Lakini inapotokea malaika akaamua kufanya kazi ya shetani huku amepose kama malaika!, huyu ni Hatari kuliko hata shetani mwenyewe maana you can't tell!. Watu wa Mungu watamsikiliza wakidhani ni malaika kumbe nje na ngozi tuu ndio ya malaika lakini ndani ni ibilisi mwovu shetani waged! .

Swali ni je ni nani ni Hatari zaidi Kati ya shetani aliyetubu na kugeuka malaika na malaika Aliyegeuka shetani kwa kufanya kazi ya shetani huku akiendelea kupose as malaika?!.

Tafakari na chukua hatua.

Nawatakia Jumatano njema.

Pasco

Nje ya mada Pasco

Kuna timu za maripota kwenye misafara ya Lowassa na Duni?

Naona kama reporting kwenye social networks sio mujarabu sana!
 
Kuhusu malaika aleyegeuka shetani sijui, ila hakuna shetani aliyegeuka malaika.

Kuhama chama sio kugeuka malaika.

Shetani akitaka kugeuka malaika lazima kwanza akubali kuwa yeye ni shetani.

Shetani anayejifanya kuwa hajawahi kuwa shetani hawezi kubadilika maana ule ushetani wake anaona unamfaa kabisa...

Shetani anakataa kuwahi kuwa shetani lakini hawa mashabiki wanakiri alikuwa shetani lakini sasa ni malaika .....kumbe tunakubaliana alikuwa shetani .....sasa tusemezane katakaswaje kuwa malaika leo ....
 
Shetani akigeuka Malaika hakuwahi kuwa shetani huyo na malaika akigeuka kuwa shetani naye hakuwahi kuwa malaika! Malaika hawezi kuwa shetani na kinyume chake ni kweli vile vile. MMM
 
Shetani akigeuka Malaika hakuwahi kuwa shetani huyo na malaika akigeuka kuwa shetani naye hakuwahi kuwa malaika! Malaika hawezi kuwa shetani na kinyume chake ni kweli vile vile. MMM

Lucifer ama Satan alikuwa nani hapo mwanzo?
 
Shetani akigeuka Malaika hakuwahi kuwa shetani huyo na malaika akigeuka kuwa shetani naye hakuwahi kuwa malaika! Malaika hawezi kuwa shetani na kinyume chake ni kweli vile vile. MMM
Hapo mwanzo, shetani alikuwa malaika!, ni baada ya uasi ndipo akawa shetani, na jeshi lake lote la mashetani, wote pia walikua malaika!.

Malaika watiifu waliendelea kuwa malaika but from time to time, baadhi ya malaika watiifu huamua kumfuta shetani, hivyo nao hugeuka mashetani, yaaani the 'fallen angeles!.

Vivyo hivyo baadhi ya watumihi wa shetani na wafuai wa shetani, wakitubu, humrudia Mungu, na huwa ni furaha kubwa mbinguni, mwenye dhambi mmoja akitubu!, hivyo ndivyo alivyokusa Mtume Paulo!.

Tatizo ni wale malika ambao waanajiita malaika na kujidai wako kwenye kundi la malaika lakini wanafanya kazi ya shetani!.

Nakutakia kazi njema!.
P.
 
kuna watu ufisadi aka uwizi aka ushetani uko kwenye damu. ukiutoa atakufa
 
Back
Top Bottom