Nani mkweli kati ya Rais Samia na Waziri Bashungwa?

Nani mkweli kati ya Rais Samia na Waziri Bashungwa?

Wakati anaapisha baadhi ya viongozi Mh. Rais Samia alimshushia sifa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Joan Kataraiya. Ikumbukwe huyu ni miongoni mwa mabinti wadogo kabisa kutoka CCM walioteuliwa katika nafasi hiyo.

Mh. Rais alisema Mkurugenzi huyo amefanya vizuri sana katika utendaji kazi wake kwa ujumla na sifa nyingine kibao.

Leo Mh. Bashungwa (Waziri wa TAMISEMI) ametoa taarifa ya utendaji kazi wa Halmashauri zote nchini ambapo Halmashauri hiyo ya Malinyi haina sifa yoyote iliyostahili kupewa na Rais. Taarifa ya Bashingwa inaonesha kuwa;

Katika asilimia za ukusanyaji wa mapato kwa ujumla Malinyi ni ya 142. Katika wingi wa mapato ni 119. Katika kutoa mikopo ya wanawake, vijana na wenye ulemavu ni ya 96 na wala haijatoa 10% kama sheria inavyotaka.

Katika kujibu hoja za CAG ni ya 45 na tathmini ya jumla ya utendaji kazi Malinyi ni ya 103.

Sasa najiuliza Rais Samia alitumia kigezo gani kuimwagia sifa Malinyi na kuziacha Halmashauri nyingine zilizofanya vizuri zaidi. Au alidanganywa na vyanzo vyake?

Rais haoni kama anatengeneza mazingira ya sisi kutokuamini maneno yake mengine maana tutahisi yamejaa uongo?

Kauli ya Rais ni nzito yenye mamlaka na ya kuaminika, so asivunje sifa hiyo kwa sababu zozote zile.
Wote fix tu hakuna mkweli

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Wakati anaapisha baadhi ya viongozi Mh. Rais Samia alimshushia sifa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi Joan Kataraiya. Ikumbukwe huyu ni miongoni mwa mabinti wadogo kabisa kutoka CCM walioteuliwa katika nafasi hiyo.

Mh. Rais alisema Mkurugenzi huyo amefanya vizuri sana katika utendaji kazi wake kwa ujumla na sifa nyingine kibao.

Leo Mh. Bashungwa (Waziri wa TAMISEMI) ametoa taarifa ya utendaji kazi wa Halmashauri zote nchini ambapo Halmashauri hiyo ya Malinyi haina sifa yoyote iliyostahili kupewa na Rais. Taarifa ya Bashingwa inaonesha kuwa;

Katika asilimia za ukusanyaji wa mapato kwa ujumla Malinyi ni ya 142. Katika wingi wa mapato ni 119. Katika kutoa mikopo ya wanawake, vijana na wenye ulemavu ni ya 96 na wala haijatoa 10% kama sheria inavyotaka.

Katika kujibu hoja za CAG ni ya 45 na tathmini ya jumla ya utendaji kazi Malinyi ni ya 103.

Sasa najiuliza Rais Samia alitumia kigezo gani kuimwagia sifa Malinyi na kuziacha Halmashauri nyingine zilizofanya vizuri zaidi. Au alidanganywa na vyanzo vyake?

Rais haoni kama anatengeneza mazingira ya sisi kutokuamini maneno yake mengine maana tutahisi yamejaa uongo?

Kauli ya Rais ni nzito yenye mamlaka na ya kuaminika, so asivunje sifa hiyo kwa sababu zozote zile.
Hangaya kama Jiwe tu; Uongo Uongo tu na janja janja, Uwezo wa Kuongoza zero!
 
Back
Top Bottom