Naogopa kuwa mama

Naogopa kuwa mama

Natumai wazima wote,.

Iko hivi, kila siku zinavyoenda ndivyo ambavyo naogopa kuja kuitwa mama hapo baadae( Mungu anisaidie niondokane na hii hofu😓🥹🙏), hiii inatokana na lifestyle ambayo namwona mama yangu anaishi..

Huyu mwanamke sielewi hua anapumzika mda gani, yeye ndie mtu wa mwisho kulala kila siku. Yaani hawezi kulala kama kuna mtu bado hajaingia nyumbani, na anahakikisha kila mtu amekula amelala anafunga milango ndipo na yeye alale., Na hata akiingia kulala halitapita nusu saa anapita tena vyumba vyote kuhakikisha mmefunga madirisha, mmeshusha neti na mmejifunika vizuri ( anaweza akaamka hata mara 4 kwa usiku mmoja)..

Haitaishia hapo, Bado kuna sisi ambao inabidi asubuhi tuende kazini na wengine shuleni, wanaoamka usiku kusoma na wanaoamka kusali, kila mtu anamtajia mda wake wa kumwamsha hajawahi kukataa wala kupitiliza kutuamsha, always anakua on time… , Sijawahi kushuhudia ni saa ngapi ameamka ila kila tukiamka asubuhi tayari tunamkuta akiwa macho, kashafanya usafi na kashapika chai tunakunywa tunamwacha Nyumbani,. Hatujawahi kuona au kushuhudia akilala mchana, Labda itokee anaumwa ( Napo ni mara chache sana ).. Sijui hua anapumzika mda gani

Hajawahi kuishi na msaidizi wa kazi maisha yake yote, lakini hakuna aliyewahi kufua, kudeki , kupika, kuosha vyombo wala kufagia. Sio kwamba hatutaki kumsaidia Hapana, ni kwamba hatujawahi kuona uwanja ukiwa mchafu, vyombo vichafu na mda wowote ukirudi nyumbani unakuta chakula tayari na usafi wote ushafanywa na nguo zote ziko kambani zinakauka,,..

Licha ya hayo yote vilevile bado hajawahi kuacha kwenda kazini na shughuli zake nyingine zote za ujasiriamali hajawahi kuacha kufanya, hajawahi kuacha kwenda kwenye jumuiya wala kanisani hata jumapili moja, na kwenye dharura zote iwe hospitali au kikao chochote atakachohitajika mzazi awepo basi ni yeye ndio atakuwepo tena kwa wakati.. Na sijawahi kumwona akilalamika, akinung’unika wala akimlaumu mtu kwamba hakuna anayemsaidia kazi hata siku moja,..

Haya maisha yake yananiogopesha na yananifanya niogope hata kuwaza jinsi nitakavyoishi na watoto wangu huko mbeleni., Sometimes i wish ningekua wakiume labda ningeishi tu kama baba yangu anavyoishi😓😓😓 ( Em assume mtu anafanya haya maisha yake yote)
Kuna kitu hujakitaja! Baba yako yupo au ni single mother? Kwa maangaiko haya hawezi kujiweka nadhifu kumvutia mumewe, hilo mosi! Pili, kwa umri ulionao huwezi msaidia mama yako inaonyesha jinsi gani kazaa kizazi zembe kitakachokuwa mzigo kwake mwenyewe nguvu zikiisha! Ndo maana hata wewe unaogopa kuolewa jinsi unavyomuona mama yako! Hopeless mama! Angetakiwa awe anawaamsha usiku saa10 mfanyekazi na kujiandalia mambo yao wenyewe na kuweka mambo ya nyumbani yaliyondani ya uwezo wao
 
Binadamu ameumbwa kufanya adaptation to current environment.
The day umebeba mwanao kuba hali flani itakuvaa ambayo itakufanya uweze kufanya kila kitu kwa ajili ya mtoto wako hata wawe kumi bila kuchoka.
Subiri nkupe ushuhuda, kipindi tuna date na wife, alikua mtu wa kulala vbaya mno. Yaan kwa mfano akiingia ndani ijumaa anaweza kutoka j3. Muda woote akimaliza tu kazi zake ni kitanda. Wakati mimi ndo kwanza siku inaanza. Tunaeza kula lets say saa moja usiku, yeye akimaliza tu anaenda kuzima. Mimi nasepa zangu narudi hata saa tano huko ndo nalala.
Lakn tulivopata tu mtoto, alibadilika ghafla. Yaani anaweza kuamka hata mara 9 kwa usiku mmoja. Atanyonyesha, mara kubadilisha diaper, mara kucheza na mtoto n.k.
Na asubuhi mapeema yuko live , mara apike chakula, sijui afue manguo, anijali na mimi na mavitu yote. No complains or anythng. Mtofo muda wote msafi, ana afya kubwa, nyumba iko standard n.k, vitu vyangu ameorganize, chakula on time na mashughuli yote.
So, hata kwako itakua hvyo. The joy of life inatokana na kuona uzao wako.
Kamwe usiogope, tena kama unaweza pata watoto mapema ili ufurahie kuona wakiwa wanakua.
Usitamani kua mwanaume, kuna vitu ambavyo tunapitia, ungeambiwa ungekimbia spidi ya fumanizi.
Kila la kheri
 
Back
Top Bottom