Naomba iwepo JF party kabla ya Septemba 30, 2024

Naomba iwepo JF party kabla ya Septemba 30, 2024

Acheni uboya! Mbona enzi za Twitter, majamaa walizindua kitu kinaitwa T.O.T bonanza, yaani "Tanzanians On Twitter Bonanza rasmi mnamo mwaka 2020... na mwitikio ulikuwa mkubwa tena very positively?! na ikawa inafanyika kila mwaka... Sijui saiv maana sijafatilia kitambo baada ya kuzidi kubanwa na mambo.

Hakukuwa na aliyetekwa, kupelekwa polisi wala kupotea na kufa na wala kuzodolewa ingawa wasema/wananga serikali wapo tele! Machawa na wanaotetea upumbavu na ushetani, wauza miili, Wakujipendekeza, Wanafki rangi mbili... Na wengineo wote walikuwemo na ililika starehe sio poa! Tena ulinzi wa kutosha!

Sasa nyinyi mnaogopa nini?!

ZINGATIENI:- "Serikali ikiamua kuwapateni nyie maboya itawapata tu!"

Hebu tuandae "Tanzanians on JF Bonanza" Ebo!!!!!
Kweli mkuu inawezekana kabisa na sion wala sijaona wabaya jf
 
tupendekeze mda mns mwezi mzuri tutakaowapataa hata wa nje wenye uwezo wa kubudhuria

2.tupendekeze sehemu ya kukutania hilo jambo jema mno

3uongozi wa jf usimamie haya na uulinz kwa pamoja

4.

5.

6

7

8...
 
King mrangi
Cc
Wapi upoo tupe posn nzuri pa kuji....
 
Kweli mkuu inawezekana kabisa na sion wala sijaona wabaya jf
Viwanja vya TTCL na Postal grounds Kijitonyama viko poa sana! Ningependekeza waite wafanyabiashara mbalimbali waje kutangaza brands zao... Kuwe na vinywaji, Vyakula na njonjo zingine kibao! Kama vipi liandaliwe bonanza maalum la soka lipigwe pale na michezo mingine kama kikapu, mpira wa pete, Tennis na kadhalika, mapema asubuhi kabla ya yote kuwe na jogging kwa ajili ya kupiga vita magonjwa yasioambukiza.... Usiku upigwe mziki mpaka majogoo ikiwezekana na tuite kama wasanii wawili watatu hivi ambao tutaweza kuwamudu

Maxence Melo
 
Back
Top Bottom