Naomba leo mniache niseme na Wasabato, nimeamua kuamka nao leo

Naomba leo mniache niseme na Wasabato, nimeamua kuamka nao leo

Baada ya kupumzika siku ya Saba siku ya nane aliendelea na kazi gani? Isije kuwa Mungu alivyomaliza mishe zake akapumzika

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
Yaa inaleta mantiki" sio waseme tu alipumzika, watuambie pia baada ya kupumzika aliendelea na kazi gani?
Usikute alivomaliza tu aliondoka zake ili akaendelee na kazi zake nyingine. Labda huku amepaacha pajiendeshe penyewe!
 
Uongo

Ukristo haukuanzia Roma ulianzia Israel Yesu alikozaliwa na kufanya huduma na kuteua mitume wake

Roman Catholic sio baba wa makanisa yote uongo

Mitume walitawanyika sehemu.mbali mbali kupeleka Ukristo Roma ikiwa sehemu mojawapo sio sehemu pekee
Yesu hakuacha dini ya Ukristo unalifahamu hili?

Wakristo wa kwanza siyo Waisrael.
 
Uongo

Ukristo haukuanzia Roma ulianzia Israel Yesu alikozaliwa na kufanya huduma na kuteua mitume wake

Roman Catholic sio baba wa makanisa yote uongo

Mitume walitawanyika sehemu.mbali mbali kupeleka Ukristo Roma ikiwa sehemu mojawapo sio sehemu pekee
Hawa jamaa wazushi kweli, wanajua kabisa ukristo ilianzia Israel, (kwa WAYAHUDI) , na hakukuwa kabisa na MKATOLIKI hata mmoja zama hizo, bali wayahudi na dini yao ya kiyahudi, YESU mwenyewe na MITUME wake wote walikuwa wayahudi kwa kabila na dini yao ilikuwa ya KIYAHUDI,

Lakini hawa jamaa kwakupenda ujiko watakwambia YESU alikuwa mkatoliki na PETRO alikuwa mkatoliki, ukiwauliza nipe ushahidi wa andiko hata mmoja kwamba petro alikuwa mkatoliki hawana!

Ukatoliko ulikuja kuanza zaidi ya miaka 300 ANNO DOMINO, baada ya kristo!
 
Neno ukristo walianza kuitwa kwa mara ya kwanza wakiwa DAMESKI, SIRIA, ni walewale wayahudi wakikristo (wafuasi wa kristo) waliokimbilia Syria , Damescus kukwepa mateso ya wayahudi dhidi yao!

Wao watakwambia ukristo ulianzia Vatican kwa papa!
 
Hawa jamaa wazushi kweli, wanajua kabisa ukristo ilianzia Israel, (kwa WAYAHUDI) , na hakukuwa kabisa na MKATOLIKI hata mmoja zama hizo, bali wayahudi na dini yao ya kiyahudi, YESU mwenyewe na MITUME wake wote walikuwa wayahudi kwa kabila na dini yao ilikuwa ya KIYAHUDI,

Lakini hawa jamaa kwakupenda ujiko watakwambia YESU alikuwa mkatoliki na PETRO alikuwa mkatoliki, ukiwauliza nipe ushahidi wa andiko hata mmoja kwamba petro alikuwa mkatoliki hawana!

Ukatoliko ulikuja kuanza zaidi ya miaka 300 ANNO DOMINO, baada ya kristo!
Wakati wa kutokea kwa Ukristo kawaida hujulikana kama 33 BK. NS. mwaka wa kusulubiwa kwa Yesu Kristo msalabani, hata hivyo, jina "Wakristo" halikupewa mara moja wafuasi wa dini mpya na likaanza kutumiwa kwa mara ya kwanza huko Antiokia mnamo 40-44.
 
Yesu hakuacha dini ya Ukristo unalifahamu hili?

Wakristo wa kwanza siyo Waisrael.
Wakristo wa kwanza walikuwa Waisrael

Wakristo maana yake wafuasi wa Kristo

Wafuasi wa kwanza wa Kristo walikuwa wote waisrael ambao ni mitume baadaye wakaongezeka siku ya Pentecoste walikuwali watu elfu tatu kuwa wafuasi wa KRISTO
Kasome.kitabu cha matendo ya Mitume na kanisa likazidi sana kuongezeka

Sema tu jina la Kuita Wakristo lilikuja baadaye lakini wafuasi wa.mwanzo wa Kristo hawakuwa warumi.

Warumi waliukubali Ukristo baadaye sans.Ikumbukwe kuwa jaji aliyehukumu Yesu auawe alikuwa mrumi Ponsio Pilato na Askari waliomuua Yesu hawakuwa wayahudi walikuwa Askari wa Kirumi kutoka Roma

Wayahudi wala hawakumhukumu Yesu kufa wala kumuua warumi toka Roma ndio waliua Yesu sio.wayahudi
 
Bro,me lazma nimind kinoma noma mana ni upumbavu haiwezekani me nashida ya maji afu we uko nayo kisima kimejaa then unakataa kuniuzia sikuomb bure the worst part thehebu lako ndo sababu ya kuninyima maji tffff
Inabidi uwahi mapema ukijua watu unaoishi nao huwezi teseka
Huwezi wabadisha badilisha mfumo wewe
Yeye mwenyewe kunavitu anakosa kwa kuzingatia izo taratibu zake
 
Wakati wa kutokea kwa Ukristo kawaida hujulikana kama 33 BK. NS. mwaka wa kusulubiwa kwa Yesu Kristo msalabani, hata hivyo, jina "Wakristo" halikupewa mara moja wafuasi wa dini mpya na likaanza kutumiwa kwa mara ya kwanza huko Antiokia mnamo 40-44.
Nimeshajibu hii hoja angalia post yangu namba #121


Rudi kwenye hoja!

Umesema wakatoliki ndio unadai walioandoka biblia hebu basi nitajie hata jina la mkatoliki mmoja aliyeandika biblia?!

Au hata kitabu kimoja ndani ya biblia?!
 
Hawa jamaa wazushi kweli, wanajua kabisa ukristo ilianzia Israel, (kwa WAYAHUDI) , na hakukuwa kabisa na MKATOLIKI hata mmoja zama hizo, bali wayahudi na dini yao ya kiyahudi, YESU mwenyewe na MITUME wake wote walikuwa wayahudi kwa kabila na dini yao ilikuwa ya KIYAHUDI,

Lakini hawa jamaa kwakupenda ujiko watakwambia YESU alikuwa mkatoliki na PETRO alikuwa mkatoliki, ukiwauliza nipe ushahidi wa andiko hata mmoja kwamba petro alikuwa mkatoliki hawana!

Ukatoliko ulikuja kuanza zaidi ya miaka 300 ANNO DOMINO, baada ya kristo!
Ni matapeli wa kidini kupenda kupora sifa zisizo zao
 
Wakristo wa kwanza walikuwa Waisrael

Wakristo maana yake wafuasi wa Kristo

Wafuasi wa kwanza wa Kristo walikuwa wote waisrael ambao ni mitume baadaye wakaongezeka siku ya Pentecoste walikuwali watu elfu tatu kuwa wafuasi wa KRISTO
Kasome.kitabu cha matendo ya Mitume

Sema tu jina la Kuita Wakristo lilikuja baadaye lakini wafuasi wa.mwanxo wa Kristo hawakuwa warumi.

Warumi waliukubali Ukristo baadaye sans.Ikumbukwe kuwa jaji aliyehukumu Yesu auawe alikuwa mrumi Pondio.Pilato na Askari waliomuua Yesu hawakuwa wayahudi walikuwa Askari wa Kirumi.kutoka Roma

Wayahudi wala hawakumhukumu Yesu kufa wala kumuua warumi toka Roma ndio.waliua Yesu sio.wayahudi
Pamoja na yoooote haya Israel dini kuu ni dini ya Kiyahudi, Wakristo ni wachache sana, Tena waislamu ni wengi Israel kuliko Wakristo.
 
Wakristo wa kwanza walikuwa Waisrael

Wakristo maana yake wafuasi wa Kristo

Wafuasi wa kwanza wa Kristo walikuwa wote waisrael ambao ni mitume baadaye wakaongezeka siku ya Pentecoste walikuwali watu elfu tatu kuwa wafuasi wa KRISTO
Kasome.kitabu cha matendo ya Mitume

Sema tu jina la Kuita Wakristo lilikuja baadaye lakini wafuasi wa.mwanxo wa Kristo hawakuwa warumi.

Warumi waliukubali Ukristo baadaye sans.Ikumbukwe kuwa jaji aliyehukumu Yesu auawe alikuwa mrumi Pondio.Pilato na Askari waliomuua Yesu hawakuwa wayahudi walikuwa Askari wa Kirumi.kutoka Roma

Wayahudi wala hawakumhukumu Yesu kufa wala kumuua warumi toka Roma ndio.waliua Yesu sio.wayahudi
Well said mkuu,,

Hawa jamaa wanataka kupotosha watu kwa kulikuza dhehebu lao!

Sijui wanadhani watu wote ni wajinga kama wao?!

Wasome biblia waachane na mapokeo yasiyo na matunda!

Wokovu unatoka kwa wayahudi , sio Vatican!
 
Ni matapeli wa kidini kupenda kupora sifa zisizo zao
HISTORIA YA KANISA B.
Kati ya mwaka 700 - 1054 kulitokea mgogoro mkubwa wa Kanisa ambao hatimaye ulikuja kuligawa rasmi Kanisa hapa duniani katika mapande makubwa mawili mwaka 1054. Upande wa Magharibi uliitwa Western Roman Catholic Church na ulikuwa unamtambua Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) kama ndio kiongozi wao. Upande wa Mashariki uliitwa Eastern Othordox (Catholic) Church na ulikuwa ukimtambua Askofu Mkuu wa Constantinople (Patriarch) kama kiongozi wao.
Sababu zilizopelekea mgogoro na mpasuko ule zilikuwa nyingi zikiwemo: 1. Matumizi ya taswila na sanamu (images) katika ibada (the iconoclastic controversy). Kutokana na changamoto ya Uislamu eneo la Mashariki, mwaka 726, Mtawala wa Dola ya Byzantine alipiga marufuku matumizi ya taswira na sanamu (images) katika ibada. Askofu Mkuu wa Constantinople aliunga mkono. Kitendo kile kililaaniwa vikali sana na Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) kwa sababu kuu mbili; mosi, Magharibi hakukuwa na Uislamu hivyo hawakuwahi kushutumiwa na Waislamu kuwa walikuwa wanaabudu sanamu kama walivyokuwa wamatuhumiwa watu wa Mashariki ambako tayari Waislamu walianza kuiteka. Pili, Papa alisisitiza kuwa watawala wa kisiasa hawakupaswa kuingilia maswala ya Kanisa. Suala hili lilikuja kupungua nguvu mwaka 843 baada ya Mkutano (Mtaguso) Mkuu wa Kanisa la Mashariki kupitisha matumizi ya picha tu lakini sio sanamu katika ibada. Hata hivyo, tayari umoja wa Kanisa ulikuwa umeathiriwa sana.
2. Mgogoro kuhusu asili ya Roho Mtakatifu (the Filioque Controversy). Mkutano Mkuu wa Nikea ulishatoa msimamo wa kiimani kuwa "Roho Mtakatifu atoka kwa Baba ...". Baadaye, katika Mkutano Mkuu ambao haukuwahusisha Kanisa la Mashariki, Kanisa la Magharibi lilifanya marekebisho katika tamko la imani (amendment) na kuandika kuwa "Roho Mtakatifu atoka kwa Baba na kwa Mwana ...". Kitendo hiki kilipelekea Kanisa la Mashariki kulituhumu Kanisa la Magharibi kwa uasi! Kwao maamuzi kama yale yalihitaji Mkutano wa Kanisa zima ambao ungehusisha Maaskofu wote. Hadi leo, Kanisa la Mashariki linaikiri Imani ya Nikea kama ilivyokuwa mwanzo pasipo mabadiliko wakati Kanisa la Magharibi (pamoja na matawi yake) limeendelea kuikiri Imani ya Nikea iliyobadilishwa kipengere hicho. Baadhi ya Makanisa siku hizi hutambua kiri zote mbili.
3. Ugomvi wa Madaraka. Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) alitaka atambuliwe kuwa ndiye Mkuu kuliko wote wakati Askofu Mkuu wa Constantinople (Patriarch) aligoma kumtambua naye akisisitiza kuwa walikuwa na mamlaka sawa.
4. Hakukuwa na mpaka rasmi kati ya mamlaka ya Rumi na mamlaka ya Constantinople hivyo kuzua mizozo ya kiutawala.
5. Mashariki, Kanisa lilikuwa linatii mamlaka ya Watawala wa Dola (serikali) wakati Kanisa la Magharibi lilisisitiza kutokuingiliwa na Dola na lilisisitiza viongozi wa Kanisa kuwasimamia viongozi wa serikali kuhusu maadili, nk.
6. Tofauti za kitamaduni: Magharibi walikuwa wakizungumza Kilatini wakati Mashariki walikuwa wakizungumza Kiyunani (Kigiriki). Pia kulikuwa na umbali wa maili 1000 kati ya Rumi na Constantinople.
7. Tofauti za ki-Liturgia: Hizi zilihusu mambo madogo madogo kama kutumia au kutokutumia mikate iliyochachushwa au isiyochachushwa katika sakramenti au ekaristi, kula mkate au kutokula mkate pamoja na divai wakati wa meza ya Bwana; Makasisi/Mapadre kunyoa au kutokunyoa ndevu na kuoa au kutokuoa, nk.
Mgogoro huo uliendelea hadi mwaka 1054 wakati Askofu Mkuu wa Rumi alipoandika waraka wa kumtenga Askofu Mkuu wa Constantinople kwa kutotii, naye Askofu Mkuu wa Constantinople akaandika waraka wa kumtenga Askofu Mkuu (Papa) wa Rumi. Hivyo Maaskofu Wakuu wa Makanisa Makuu ya Rumi na Constantinople wakawa wametengana na ndio Kanisa likawa limegawanyika rasmi. Kanisa la Magharibi liliendelea kugawanyika na kuzaa matawi kwa mfuatano ufuatao kuanzia lipi lilianza; Waldensian, Moravian, Lutheran, Mennonite, Presbyterian, Baptist, Anglican, Methodist, Assemblies of God, nk. Kanisa la Mashariki halijwahi kukumbwa na migogoro au migawanyiko ingawa lina matawi mengi kama vile Ethiopian Church, Coptic Church (Kanisa la Misri), Greek Orthodox, Russian Orthodox, Eastern Orthodox, Syrian Church, nk.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania (KMUT).
 
Back
Top Bottom