Naomba leo mniache niseme na Wasabato, nimeamua kuamka nao leo

Naomba leo mniache niseme na Wasabato, nimeamua kuamka nao leo

HISTORIA YA KANISA B.
Kati ya mwaka 700 - 1054 kulitokea mgogoro mkubwa wa Kanisa ambao hatimaye ulikuja kuligawa rasmi Kanisa hapa duniani katika mapande makubwa mawili mwaka 1054. Upande wa Magharibi uliitwa Western Roman Catholic Church na ulikuwa unamtambua Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) kama ndio kiongozi wao. Upande wa Mashariki uliitwa Eastern Othordox (Catholic) Church na ulikuwa ukimtambua Askofu Mkuu wa Constantinople (Patriarch) kama kiongozi wao.
Sababu zilizopelekea mgogoro na mpasuko ule zilikuwa nyingi zikiwemo: 1. Matumizi ya taswila na sanamu (images) katika ibada (the iconoclastic controversy). Kutokana na changamoto ya Uislamu eneo la Mashariki, mwaka 726, Mtawala wa Dola ya Byzantine alipiga marufuku matumizi ya taswira na sanamu (images) katika ibada. Askofu Mkuu wa Constantinople aliunga mkono. Kitendo kile kililaaniwa vikali sana na Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) kwa sababu kuu mbili; mosi, Magharibi hakukuwa na Uislamu hivyo hawakuwahi kushutumiwa na Waislamu kuwa walikuwa wanaabudu sanamu kama walivyokuwa wamatuhumiwa watu wa Mashariki ambako tayari Waislamu walianza kuiteka. Pili, Papa alisisitiza kuwa watawala wa kisiasa hawakupaswa kuingilia maswala ya Kanisa. Suala hili lilikuja kupungua nguvu mwaka 843 baada ya Mkutano (Mtaguso) Mkuu wa Kanisa la Mashariki kupitisha matumizi ya picha tu lakini sio sanamu katika ibada. Hata hivyo, tayari umoja wa Kanisa ulikuwa umeathiriwa sana.
2. Mgogoro kuhusu asili ya Roho Mtakatifu (the Filioque Controversy). Mkutano Mkuu wa Nikea ulishatoa msimamo wa kiimani kuwa "Roho Mtakatifu atoka kwa Baba ...". Baadaye, katika Mkutano Mkuu ambao haukuwahusisha Kanisa la Mashariki, Kanisa la Magharibi lilifanya marekebisho katika tamko la imani (amendment) na kuandika kuwa "Roho Mtakatifu atoka kwa Baba na kwa Mwana ...". Kitendo hiki kilipelekea Kanisa la Mashariki kulituhumu Kanisa la Magharibi kwa uasi! Kwao maamuzi kama yale yalihitaji Mkutano wa Kanisa zima ambao ungehusisha Maaskofu wote. Hadi leo, Kanisa la Mashariki linaikiri Imani ya Nikea kama ilivyokuwa mwanzo pasipo mabadiliko wakati Kanisa la Magharibi (pamoja na matawi yake) limeendelea kuikiri Imani ya Nikea iliyobadilishwa kipengere hicho. Baadhi ya Makanisa siku hizi hutambua kiri zote mbili.
3. Ugomvi wa Madaraka. Askofu Mkuu wa Rumi (Papa) alitaka atambuliwe kuwa ndiye Mkuu kuliko wote wakati Askofu Mkuu wa Constantinople (Patriarch) aligoma kumtambua naye akisisitiza kuwa walikuwa na mamlaka sawa.
4. Hakukuwa na mpaka rasmi kati ya mamlaka ya Rumi na mamlaka ya Constantinople hivyo kuzua mizozo ya kiutawala.
5. Mashariki, Kanisa lilikuwa linatii mamlaka ya Watawala wa Dola (serikali) wakati Kanisa la Magharibi lilisisitiza kutokuingiliwa na Dola na lilisisitiza viongozi wa Kanisa kuwasimamia viongozi wa serikali kuhusu maadili, nk.
6. Tofauti za kitamaduni: Magharibi walikuwa wakizungumza Kilatini wakati Mashariki walikuwa wakizungumza Kiyunani (Kigiriki). Pia kulikuwa na umbali wa maili 1000 kati ya Rumi na Constantinople.
7. Tofauti za ki-Liturgia: Hizi zilihusu mambo madogo madogo kama kutumia au kutokutumia mikate iliyochachushwa au isiyochachushwa katika sakramenti au ekaristi, kula mkate au kutokula mkate pamoja na divai wakati wa meza ya Bwana; Makasisi/Mapadre kunyoa au kutokunyoa ndevu na kuoa au kutokuoa, nk.
Mgogoro huo uliendelea hadi mwaka 1054 wakati Askofu Mkuu wa Rumi alipoandika waraka wa kumtenga Askofu Mkuu wa Constantinople kwa kutotii, naye Askofu Mkuu wa Constantinople akaandika waraka wa kumtenga Askofu Mkuu (Papa) wa Rumi. Hivyo Maaskofu Wakuu wa Makanisa Makuu ya Rumi na Constantinople wakawa wametengana na ndio Kanisa likawa limegawanyika rasmi. Kanisa la Magharibi liliendelea kugawanyika na kuzaa matawi kwa mfuatano ufuatao kuanzia lipi lilianza; Waldensian, Moravian, Lutheran, Mennonite, Presbyterian, Baptist, Anglican, Methodist, Assemblies of God, nk. Kanisa la Mashariki halijwahi kukumbwa na migogoro au migawanyiko ingawa lina matawi mengi kama vile Ethiopian Church, Coptic Church (Kanisa la Misri), Greek Orthodox, Russian Orthodox, Eastern Orthodox, Syrian Church, nk.
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Mkuu wa Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania (KMUT).
Hicho ulichoandika ni mgawanyiko.wa kanisa katoliki kuwa mawili na baadaye vikaja vipande vingine

Lakini kuna makanisa ambayo hayakuwa connected labisa na kanisa la Rumi wala hayakuwa sehemu yake yaliendelea na imani zao kwenye mataifa mbalimbali

Sema tatizo wana theolojia wengi hujikita tu kwenye historia ya ukatoliki wanasahau kuwa ukristo haukuanzia kwenye uromani katoliki

Wanasahau kufuatilia hizo branch zingine ambazo hazikuwa connected na kanisa katoliki
 
Ukristo asili yake ni Israel, kwa wayahudi! Na vitabu vyote ndani ya biblia vimeandikwa na wayahudi (ukiondoa LUKA ambaye hata hivyo bado kuna utata kama alikuwa myahudi au myunani mgiriki).

Maana LUKA hakuwa kati ya mitume wa yesu wale thenashara (12) lakini inadaiwa alikuwa ni mmoja wa wafuasi wa yesu nguli, wengine wanasema alikuwa daktari (tabibu) hapo bado wanazuoni wa biblia wanatofautiana!

Lakini vitabu vingine vyote ndani ya biblia vimeandikwa na wayahudi wenyewe, na Ukristo ulianzia uyahudi JERUSALEM siku ya pentekoste (ukiacha siku alizohubiri Yesu mwenyewe).

Japo baadae kwa mateso ya wayahudi wenye kushika dini ya kiyahudi ilibidi mitume wengi na wakristo wengi wa kiyahudi kukimbiloa nji jirani ya Siria, Damascus, wengine wakaenda Antiokia ambapo huko ndipo jina WAKRISTO lilipoanza kuitwa rasmini.

Sasa jamaa zangu wanakuja hapa na kupotosha watu kwamba eti BIBLIA IMEANDIKWA sijui na wakatoliki bla bla blaaaa!

Tuache huu upotofu na uzushi hausaidii kitu! Mungu ni mmoja, Bwana wetu Yesu Kristo ni mmoja na imani moja!

Inatosha! hayo ya uzushi na udhehebu hayana tija Sana!
 
Yamekukuta kama yangu inaniumga mpaka leo japo imepita miaka
nilitoka home pana umbali kidogo na huyo mama kwenda kununua sabuni nafik ananiambia aah leo sabato nikondoka kwa uchungu sana.
Wanasahau hata Yesu liwaulizaga watoto zenu sijui wanapunda wakizama mtoni hamtawatoa kisa sabato?
Kwamba ulikuta kafungua duka?
 
Sasa si ungeingia ndani akupe Maji yake aliyoweka akiba...
Yaani asikupe ya kuuza..
Simple tu
 
Ivi mfano unatakiwa kumeza dawa na huna maji , au unahitaji maji kusafisha jeraha, hayo yote cyo dharura , au unataka kupika na huna maji , au mmi ndo cjui dharura
Nenda hospital au kaombe kwingine
 
Shida ni kutoyaelewa maandiko,kiasi kwamba mtu/watu tunakuwa watumwa.Yesu alishasema "Sabato iliwekwa kwaajili ya watu na si watu kwaajili ya sabato".
Halafu hakuna kifungu chochote kinachotamka kwenye Biblia kuwa Sabato ni siku ya Jumamosi

Mungu alisema fanya kazi siku sita ya saba pumzika.Sabato iwe siku gani kwa wiki ni makubaliano ya jamii eneo husika cha msingi wafanye kazi siku sita ya saba wapumzike yaweza kuwa siku yeyote ya juma yaweza kuwa alhamisi,ijumaa,Jumamosi au jumapili au yeyote
 
Yaani yuko tayari mtu afe kwa kiu kisa sabato,huu mzigo.
 
Tafuta pesa acha makasiriko shida zako zisikulazimishe kuwapangia Watu namna ya kuishi kwanza wewe popo kweli yaani unakosaje maji ndani ya nyumba afu unaenda kwa msabato kumtengulia sabato yake kwa akili yako finyu.
 
Ungetumia energy hii kutukana serikali kuwaletea miundo mbinu ya maji tungefika mbali,ila mtu maji yake,imani yake,why umtusi?tafuta hela kijana,ukiwa lofa kila mtu utamuona KAVU
 
Well said mkuu,,

Hawa jamaa wanataka kupotosha watu kwa kulikuza dhehebu lao!

Sijui wanadhani watu wote ni wajinga kama wao?!

Wasome biblia waachane na mapokeo yasiyo na matunda!

Wokovu unatoka kwa wayahudi , sio Vatican!
Tatizo wana theolojia wengi hujikita zaidi kwenye historia ya kanisa katoliki sio historia ya Ukristo kwenye Biblia

Kwa hiyo wana theolojia wengi huelezea historia ya Ukristo kama historia ya kanisa la Roman Catholic

Wanaanza na u roman Catholic ulivyoanza na baadaye kugawanyika na kuongelea madhehebu yaliyoibuka kutokea Ukatoliki na kujifanya wasomi wa Historia ya kanisa

Historia ya kanisa haianzii kwenye mwanzo wa kanisa katoliki.Hilo lilianzishwa miaka kibao toka Yesu afe ,kusulubiwa na kufufuka ni dini ilikuja baadaye sana tena mno

Ndio maana hupotoka wakiongelea historia ya Ukristo

Wanajikita kuongelea historia ya kanisa la Roman Catholic badala ya historia ya Ukristo
 
Back
Top Bottom