Naomba mfano wa Taifa lililoshusha gharama ya maisha kwa kutumia Katiba?

Naomba mfano wa Taifa lililoshusha gharama ya maisha kwa kutumia Katiba?

Pengine ufahamu wangu una shida ya kuelewa polepole au kuna mambo yananipita kushoto. Kwa jinsi ninavyowasikiliza wanasiasa wanavyoizungumzia katiba mpya ni kana kwamba katiba mpya ikipatikana leo kesho changamoto zote zitakwisha, au chini ya katiba iliyopo hatuna uwezo wa kuivisha chochote.

Katiba mpya haitamaliza wizi, uzembe, majungu, ujinga, uvivu, nk

Mambo yanayolalamikiwa sana kwenye katiba iliyopo ni
Madaraka ya rais
Tume huru
Muungano
Nk

Hayo yoote sioni ni vipi yatashusha gharama ya maisha.

Labda wajuvi mje na taifa lililowahi kufanikiwa kushusha gharama ya maisha kwa kutumia KATIBA.
Katiba nzuri ndio inayotupatia viongozi wazuri na katiba ya hovyo hutupatia viongozi wa hovyo

Viongozi ndio wanatakiwa kutatua changamoto zetu kama maji,uchumi, biashara, chakula, miundombinu n.k.

wakipatikana viongozi wa hovyo hayo yote yatakuwa ndoto kama ilivyo Sasa miaka 60 ya uhuru bado maji,elimu na chakula ni tatizo sana kwa nchi yenye ardhi kubwa na heti kilimo ndio UTI wa mgongo

Katiba nzuri ni Ile inatoa usawa kwa watu wote inawajibisha kwa usawa na hakuna aliye juu ya sheria.

Viongozi ndio wanapanga hatima ya mwananchi katika Kila jambo.
 
Katiba nzuri ndio inayotupatia viongozi wazuri na katiba ya hovyo hutupatia viongozi wa hovyo

Viongozi ndio wanatakiwa kutatua changamoto zetu kama maji,uchumi, biashara, chakula, miundombinu n.k.

wakipatikana viongozi wa hovyo hayo yote yatakuwa ndoto kama ilivyo Sasa miaka 60 ya uhuru bado maji,elimu na chakula ni tatizo sana kwa nchi yenye ardhi kubwa na heti kilimo ndio UTI wa mgongo

Katiba nzuri ni Ile inatoa usawa kwa watu wote inawajibisha kwa usawa na hakuna aliye juu ya sheria.

Viongozi ndio wanapanga hatima ya mwananchi katika Kila jambo.
Inategemea unaposema miaka 60 unajilinganisha na nani maana nchi sio binadamu hata hivyo ukiangalia takwimu bila macho ya makengeza utajua Kuna hutua kubwa imepigwa japo htujafikia ubora tunaoutaka.

Katiba ni jambo moja na utendaji wa katiba ni jambo lingine kabisa najifunza sana Kwa jirani zetu Kenya pamoja na katiba nzuri sana lkn nadhani wanaongoza Kwa kuwa na viongozi wapigaji
 
Back
Top Bottom