Naomba Msaada. Nifanyeje ili niweze kupona ini?

Naomba Msaada. Nifanyeje ili niweze kupona ini?

Nenda katibiwe hospitals kubwa kama Muhimbili Au Agakhan? Huyo Dr wa Amana uwezo wake ndo ulipoishia ila kuna vipimo vingi tu unapaswa kuvifanya na wataalaam wabobezi. Nenda Muhimbili uokoe maisha yako.
 
Mrejesho. Nilipost humu kuomba ushauri kuhusu hali yangu ya afya baada ya kuambiwa ini langu lina shida. OK ilibidi nirudi Amana na kuomba rufaa ya kwenda Muhimbili kuona na Dr bingwa wa ini. Baada ya kufika Muhimbili nilifanyiwa vipimo vyote muhimu vya awali vya utambuzi wa tatizo kwenye ini, kongosho, nyongo na figo. Pia nilifanya Utrasound ya tumbo na Endoscopy. Vipimo vyote havikuonesha dalili ya uharibifu ktk ini na viungo vingine vya ndani, hivyo Dr akiishia hapo kuwa ini halina shida hivyo hakuna haja ya kuagiza vipimo zaidi. Kuhusu maumivu ya tumbo upande wa juu kulia chini ya mbavu Dr alisema huenda ni sababu ya vidonda vya tumbo ambavyo viligundulika kwenye kipimo cha Endoscopy. Hivyo zoezi la uchunguzi kuhusu ini na viungo vingine vya ndani liliishia hapo na ugonjwa pekee uliotambuliwa ni ulcers ambapo nilipewa dozi ya wiki 6. Ahsanteni kwa ushauri wenu na pole mlizonipa.
 
Mrejesho. Nilipost humu kuomba ushauri kuhusu hali yangu ya afya baada ya kuambiwa ini langu lina shida. OK ilibidi nirudi Amana na kuomba rufaa ya kwenda Muhimbili kuona na Dr bingwa wa ini. Baada ya kufika Muhimbili nilifanyiwa vipimo vyote muhimu vya awali vya utambuzi wa tatizo kwenye ini, kongosho, nyongo na figo. Pia nilifanya Utrasound ya tumbo na Endoscopy. Vipimo vyote havikuonesha dalili ya uharibifu ktk ini na viungo vingine vya ndani, hivyo Dr akiishia hapo kuwa ini halina shida hivyo hakuna haja ya kuagiza vipimo zaidi. Kuhusu maumivu ya tumbo upande wa juu kulia chini ya mbavu Dr alisema huenda ni sababu ya vidonda vya tumbo ambavyo viligundulika kwenye kipimo cha Endoscopy. Hivyo zoezi la uchunguzi kuhusu ini na viungo vingine vya ndani liliishia hapo na ugonjwa pekee uliotambuliwa ni ulcers ambapo nilipewa dozi ya wiki 6. Ahsanteni kwa ushauri wenu na pole mlizonipa.
Kwahiyo kwa kifupi mda wote huo ulikua unatibu tatizo ambalo huna..?🙄
 
Back
Top Bottom