Naomba neno moja tu la Kingereza ambalo halina tafsiri rasmi ya Kiswahili

Naomba neno moja tu la Kingereza ambalo halina tafsiri rasmi ya Kiswahili

Nashukuru kwa mchango wako. Je unaweza kusema "Orodha nyeusi" ndio tafsiri rasmi ya "Blacklist?" katika muktadha wa "Mwenye/wenye sifa mbaya iliyopitiliza?"
Hapana! Orodha nyeusi Si tafsiri sahihi ya neno blacklist. Tafsiri sahihi inapaswa kuwa ' orodha ya nchi korofi/ kaidi'.
 
Kwanini iwe "waya janja" na isiwe "waya hewa"?

Mchango mzuri.

Nimejibu jinsi nilivyofikia pendekezo langu. Naomba na wewe utuambie umefikiaje kwenye pendekezo lako la "waya hewa."

Mjadala unazidi kunoga. Tuendelee.
 
Hapana! Orodha nyeusi Si tafsiri sahihi ya neno blacklist. Tafsiri sahihi inapaswa kuwa ' orodha ya nchi korofi/ kaidi'.

"Blacklist" ni general word. Mtumiaji ndio anaweka muktadha au context. Kwa hiyo tafsiri rasmi ni ipi?
 
Phisics, kemia😂😂, geo, cjauvinism, cocastic, bambustic, fantastic, radio, bulb, bamboo, dance floor, lip sync, melanin, platelets, madamu, skimming, scanning, saini, gonolea, overloading, siesta, /, ni mengi aisee🥱
 
Mkuu unafanya utafiti hapo time ya Kiswahili, ?

Hapana ndugu. Kama nilivyosema mwanzo, nafikiri kuna haja ya kuwashirikisha wananchi au watumiaji wa lugha ya Kiswahili katika kutafuta au kuikuza lugha yetu. Sehemu yangu mimi baada ya kuona hii changamoto, nimeamua kuja na platform ambayo itatoa fursa hiyo kwa jamii. Kwa hiyo nataka kujua kama hiyo changamoto ipo kweli au ni mimi binafsi ndio nimepitwa na wakati.
 
Napendekeza bluetooth iitwe jongeohewa. Mfano wa sentensi Nirushie huu wimbo kwa jongeohewa

Umefikiaje hilo pendekezo lako la "Jongeohewa?" Je kuna kilugha hapo? Hebu tupe ufafanuzi kidogo ili umma uelimike.

Lina uhalisia wa Kibantu.

Asante.
 
Kiswahili hakikutakiwa kitumike kabisa

Moja ya utambulisho wa jamii fulani ni lugha yao. Kwasababu tuna msingi tayari, tuanzie hapo kukikuza zaidi.

Usikate tamaa
 
Kwa muda mrefu sana nimekuwa napata wakati mgumu ninapoona baadhi ya maneno ya Kingereza haswa katika Technology au professional fulani kukosa tafsiri rasmi. Hapa neno "tafsiri" nina maana ya translation. Mfano maneno kama, excavator katika context ya machinery au equipment; hearse katika context ya vehicle; au digital katika context ya technology.

Kwa maneno yenye tafsiri rasmi, nimekuwa najiuliza zinapatikanaje na mchango wa jamii ni kiasi gani. Mfano mdogo tu, dunia ilipoanza kutumia email kama njia ya mawasiliano, ilinichukua muda mrefu kujua tafsiri yake ni barua pepe. Pia nafikiri tafsiri rasmi ya Artificial Intelligence au AI, ni "Akili Mnemba." Kwa mara nyingine tena swali langu ni je, hizo tafsiri rasmi zimepatikanaje? Wananchi walihusishwa kwa kiasi gani?

Mfano mwingine ambao umenipa maswali mengi hivi karibuni ni wakati nasikiliza taarifa ya Habari ya saa mbili usiku kutoka redio moja maarufu, (bila kuitaja jina) hapa nchini. Katika kuwasilisha Habari kuhusu taifa fulani kugomea mkutano wa UN kwasababu nchi hiyo imewekwa kwenye "Blacklist", mtangazaiji alisema, (sio nukuu ya moja kwa moja), "Nchi X ilitoka nje ya mkutano kwasababu imewekwa kwenye listi nyeusi." Baada ya kusikia hivyo nikajiuliza, Je katika muktadha huo, kusema "Listi nyeusi" ndio tafsiri rasmi ya "Blacklist?"

Baada ya kusikia hivyo, ikaamsha tena chachu yangu ya kujua tunapataje tafsiri rasmi ya maneno magumu ya Kingereza na, ni jinsi gani wananchi wanaweza kujumuika katika kutatua changamoto hiyo.

Baada ya kusema hayo machache, swali langu kwako ni, je, unafikiri lugha yetu ya Kiswahili ina changamoto hiyo? Au wewe binafsi umeshawahi kukumbana nayo katika masomo yako, au kazi zako za kila siku? Kama jibu ni ndiyo, naomba neno moja tu la Kingereza ambalo unafikiri halina tafsiri rasmi. Kwa kufurahisha mjadala huu, ukiweza, pendekeza tafsiri ambayo wewe unafikiri itafaa kwa neno ulilopendekeza.

Kwanini nimeleta ombi hili kwenu? Nia kubwa iliyonifanya nilete ombi hili kwenu ni kwasababu, kwanza binafsi nafikiri hii changamoto ipo. Pili, nafikiri ingekuwa vema kama wananchi nao wangejumuishwa katika utafutaji wa tafsiri rasmi ya menono magumu au mapya ya Kingereza. Tatu, kwa kushirikisha jamii, watajiona nao ni sehemu katika kukuza Kiswahili.

Kwa kumalizia, nimepata muarobaini wa changamoto hii. Muda si mrefu, nataka niweke platform ambayo itakuwa rafiki kwa jamii nzima. Itajumuisha jamii yote ndani na nje ya nchi kwa ujumla katika kukabiliana na changamoto hii. Itasaidia kufanya watu wafikiri na kupanua mawazo.

Ndani ya siku 7, nitawajulisha jina la platform.

Nashukuru sana. Karibuni sote tujiunge kukuza Kiswahili.
Serendipity
"Serendipity" ni neno la Kiingereza linalomaanisha ugunduzi wa mambo mazuri kwa bahati au kwa nasibu, hasa mambo ambayo hayakutarajiwa au kutafutwa. Hali hii inapotokea, mtu anapata kitu kizuri bila kuwa amekikusudia au kukitafuta.
 
Back
Top Bottom