Naomba tuungane kuanzisha Vitabu vya Dini ya Waafrika

Naomba tuungane kuanzisha Vitabu vya Dini ya Waafrika

Na wewe kwanini ukakubali kupelekwa utumwani?? Kwanini usipambane?? Huoni kupelekwa utumwani ilikuwa ni ujinga na uoga na uzembe wako mwenyewe!!-- inakuaje mtu atoke atokake aje nyumbani kwako na anakukamata kama swala na anaondoka na wewe kiulaini !!, isitoshe utumwa ilikuwa ni biashara iliyochukua muda mrefu je mlishindwaje kushirikiana nyinyi wenyewe na kuitokomeza??, waafrika tulikuwa hovyo na hadi leo tunanyanyaswa na kubaguliwa na kuporwa maliasili zetu ni muendelezo wa ujinga uleule tuliorithi kutoka kwa mababu zetu hivyo huna haja ya kumlaumu Mungu bure juu ya ujinga wako.
Ni kweli ndiyo maana nawashushia furushi la lawama wazee wetu
 
MUNGU ni mmoja duniani,hakuna Mungu wa Wafrika au Waarabu,Wazungu,rtc.

Huyohuyo anaitwa majina tofauti tu Mungu,Mlungu,Nyasae,Imana,n.k tunachoongelea hapa ni jinsi ya kumuabudu ambapo Wazunguzu wanataka tumuabudu kupitia yesu na waarabu tupitie mohamad wakati hao ni waasisi wa dini au imani zao.

Sisi pia tulikuwa na waasisi wetu kama Mwanamarundi,Kisukarumbele,Mirambo,nk ambao walimuamini Mungu huyohuyo na walikuwa na miujiza zaidi ya mohamed na yesu na walikuwa WAAFRIKA siyo wazungu wala waraabu.

MUNGU ni mmoja aliyeumba viumbe vyote vilivyohai na visivyohai ulimwenguni kote
Aaah kama uko familiar with Muhammad’s teachings utagundua Mungu wake sio sawa na wa machifu
 
Aaah kama uko familiar with Muhammad’s teachings utagundua Mungu wake sio sawa na wa machifu
Wewe ni binadamu ni mnyama uko kundi moja na mbwa,paka,ngombe,fisi,nyani,n.k. na aliyekufundisha hivyo ni mzungu ukaamini ,je umewahi kujiuliza Mungu wa hao wanyama wenzio ni nani?je ndiyo huyohuyo wa wazungu?
 
Hawa ndiyo Waaafrika wenye uwezo zaidi ya yesu na mohamad kwani maneno yao yalitabili kabisaaaa ujio wa wazungu na warabu na ikatimia ambao wameweza kutugawa na kuvunja nguvu zetu,sasa wewe Mwafrika wa leo nini kinakufanya uwaamini Manabii wageni na kuwakataa Manabii wenyeji.

Hivi vitabu ndivyo tutanatakiwa kuviunganisha na kuwa biblia ya AFRIKA na mabii wetu watakuwa mashujaa wote waliokatika vitabu hivi n.k.0

Tutafakari vitabu vyote vilivyoandika na WAAFRIKA kuelezea na kupinga madhara ya ukoloni viunganishwe na kuwa BIBLIA ya WAAFRIKA
JamiiForums-944991709.jpg
 
Wewe ni binadamu ni mnyama uko kundi moja na mbwa,paka,ngombe,fisi,nyani,n.k. na aliyekufundisha hivyo ni mzungu ukaamini ,je umewahi kujiuliza Mungu wa hao wanyama wenzio ni nani?je ndiyo huyohuyo wa wazungu?
Aisee kijana chuki yako kwa wazungu inakutia upofu

Ila usijisahaulishe hiyo simu unayotumia kupost ni hao hao wazungu waliumiza kichwa kuiunda
 
Habarini,

Baada ya kupitia mijadala mingi humu JF na mitandao mbalimbali nimeona sasa kunaumuhimu wa kuungana sisi wenyewe Waafrika na kuanzisha dini/kanisa la Imani ya Waafrika/Washindi wa Afrika/Africa Catholic nk.

Hii ni kutokana na uwazi kuwa sasa Waafrika tumeanza kujitambua hivyo inatubidi kuweka maandiko yetu ya kiimani na kuabudu yatakayofundisha mambo mazuri na kuyaendeleza na pia mambo mabaya na kuyaacha kwa kufuata mfumo uleule wa kuzikataa dini na imani tulizoletewa na wakokoni wote kwani siyo rahisi kuzikataa pasipo kuanzisha ya kwetu.

Naomba mapendekezo yenu wote wenye nia njema na Afrika kwa kuanza na jina lipi litumike kuiwakilisha dini/imani yetu ingawa naona kabisa madhebu yetu yanaweza kuegemea koo au makabila yenye mila na desturi zilizosawa na vitabu vyetu pia vinaweza kuwa hivyohivyo i.e. kitabu cha Wasukuma, kitabu cha Wachanga, n.k

Naomba kuwasilisha.
Walishajaribu sana na matokeo yake ndio hao Mungiki Kenya na wengine wengi sana Nigeria soma mtandaoni utaona. Imani huvuviwa na Mungu na sio kuanzishwa kwa akili ya kibinadamu tu.
 
Walishajaribu sana na matokeo yake ndio hao Mungiki Kenya na wengine wengi sana Nigeria soma mtandaoni utaona. Imani huvuviwa na Mungu na sio kuanzishwa kwa akili ya kibinadamu tu.
Mungu yupi anavuvia sasa mkuu???Maana mungu wapo wengi kutegemeana na imani husika
 
Hii mada ni nzuri na muhimu sana ila watu wanaleta utani na mizaha isiyo maana,wamemezwa na imani za kuletewa hawajui kwamba dini ndio muongozo wa kila kitu maishani
 
Mleta mada unatambua kwamba hivyo tayari vipo lakini katu mfumo uliowekwa haukuruhusu na hauwezi kukuruhusu wewe uyajue hayo?!

Mnaitambua maktaba kubwa iliyosheheni vitabu tele vyenye siri za ulimwengu huu na Afrika hii ambayo ilifungwa miaka mingi na ipo hapahapa barani Afrika nchini Ethiopia?!

To make story short na mfano mmoja aadhwiim kabisa... ilitengenezwa sinema inaitwa "BLACK PANTHER" mnajua ile story waliisoma kwenye kitabu ambacho kiliibiwa kwenye hiyo maktaba sasa haijulikani walikipeleka Marekani au kipo hapahapa. Kama mlitazama sinema ile vyema yale ni mafumbo ni kila kilichomo vilikuwepo/kilikuwepo na bado vipo/kipo barani Afrika. Wazungu wakagundua wakamaindi wakamwingiza kwenye kumi na nane "18" yule bwana/kijana aliyeshiriki kwenye ile sinema kama mtunzi na msimamizi mkuu kutengeneza sinema aliyeitwa "CHADWICK BOSEMAN" wakamuulia mbali na kansa ya kupandikiza. Na si yeye tu yoyote atakayejitia kimbelembele kufichua siri zilizopo hapa za Utajiri, teknolojia, dini, Uchawi, tiba, Siasa na kila kitu adhabu yako ni kukulia mbali!
 
Waafrika tumetekwa na kufanywa watumwa kwenye dini za waarabu na wazungu!!! Eti muafrica anamuua mwafrica mwenzie kisa sio muislamu au sio mkristo !?? Ulishaona wapi mzungu ,machina,mjapani ana muua mwenzie kisa sio dini moja!?? Waafrika tuwe na Imani yetu bana uislam ubakie arabuni ,ukristo ubakie ulaya
 
Ni WAPUMBAVU tu! Wimbi la vijana Jobless limekuwa kubwa sana humu.

Wengine wako chuo wanakuja kutuletea UJINGA UJINGA WAO HUMU!
Nikiwa njiani nikatupia macho kwenya banda moja la kubeti, asee kuna vijana wamejaa humo! Nguvu kazi mijini kubwa hupotea kwa kupoteza muda kwenye mambo ya kubeti, hawa wakitoka humo wakawa panya road msishangae.
Kwangu mimi ongezeko la panya road linaenda sambamba na kukua hizi ofisi za kubeti, sasa mashine za kamali zinaenea mpaka vijijini. Jamii isishangae kupata panya road mpaka vijijini siku za usoni.
 
Habarini,

Baada ya kupitia mijadala mingi humu JF na mitandao mbalimbali nimeona sasa kunaumuhimu wa kuungana sisi wenyewe Waafrika na kuanzisha dini/kanisa la Imani ya Waafrika/Washindi wa Afrika/Africa Catholic nk.

Hii ni kutokana na uwazi kuwa sasa Waafrika tumeanza kujitambua hivyo inatubidi kuweka maandiko yetu ya kiimani na kuabudu yatakayofundisha mambo mazuri na kuyaendeleza na pia mambo mabaya na kuyaacha kwa kufuata mfumo uleule wa kuzikataa dini na imani tulizoletewa na wakokoni wote kwani siyo rahisi kuzikataa pasipo kuanzisha ya kwetu.

Naomba mapendekezo yenu wote wenye nia njema na Afrika kwa kuanza na jina lipi litumike kuiwakilisha dini/imani yetu ingawa naona kabisa madhebu yetu yanaweza kuegemea koo au makabila yenye mila na desturi zilizosawa na vitabu vyetu pia vinaweza kuwa hivyohivyo i.e. kitabu cha Wasukuma, kitabu cha Wachanga, n.k

Naomba kuwasilisha.
Tanzania ina wajinga wengi sana
~Dr mollel
 
Back
Top Bottom