Naomba Ushauri: Nifanye nini niweze kuingiza Pesa kwa kutumia huduma za Intaneti? Isiwe Betting au Forex

Naomba Ushauri: Nifanye nini niweze kuingiza Pesa kwa kutumia huduma za Intaneti? Isiwe Betting au Forex

Mbna kwa sasa mambo ni mengi tu.
1. Nunua router tafta unlimited bundle unga wana kitaa
2. Unaweza kuanzisha online tv
3. Kuwa comedian post tik tok
4. Tumia internet kuchambua timu beti
5. Jiunge forex
6. Tumia internet kuongeza elimu yako kitaaluma
7.share ads upate kulipwa
8. Tafuta hela upate hela
 
Mbna kwa sasa mambo ni mengi tu.
1. Nunua router tafta unlimited bundle unga wana kitaa
2. Unaweza kuanzisha online tv
3. Kuwa comedian post tik tok
4. Tumia internet kuchambua timu beti
5. Jiunge forex
6. Tumia internet kuongeza elimu yako kitaaluma
7.share ads upate kulipwa
8. Tafuta hela upate hela
Asante sana kaka Mungu akubariki ushauri mzuri sana
 
Wakuu.

Natamani kuingiza hela kwa upande wa internet naombeni msaada kwa wabobovu hata elfu 5 kwa wiki.

Toa Forex, betting
Ili ufanikiwe lazima ujue kwanza malengo yako ni yapi. Nitakusaidia kidogo japo mimi sijawekeza kwenye project za mtandaoni. Ikiwa nigekua ni mimi nataka kufanya hio project ningejiuliza haya yafuatayo
1.Je malengo yangu ni kuingiza sh ngapi kwenye project za mtandaoni?Mfano kama ni kuingiza laki 1 kwa mwezi, swali linalofuata ni mtandao gani au ni project gani inaweza ikaingiza hio laki ndani ya mwezi 1?Mfano, unaweza chunguza je blog, freelancing, network marketing, online shop ipi inaweza nipa laki kwa mwezi?
2.Natafuta mtu ambaye amefanikiwa kupitia hio internet project husika na anaingiza kuanzia laki na kuendea kwa mwezi 1. Watu wengi wanadhani unaweza ukafanikiwa ukiwa mwenyewe tu,yani MAN ALONE. Hii ni ngum sana mana utajikuta unawekeza sehem ambayo sio na utakuja kulia kama mbwa koko.
3 . Nitamtumia huyu mtu anifundishe kwa undani ili nipate elimu yakutosha kuhusian na hio online project husika. Waswahil wanasema akili/Maarifa ndo mtaji wa kwanza katika kufanikiwa. Wengi wanafeli kwasababu hawana elimu ya kutosha na kile wanachokifanya mwishoe wanafeli wanaanza kusingizia ni UCHAWI AU KUROGWA.
4.Baada ya kupata elimu jambo linalofuata ni kuchukua hatua za awali za kutekeleza jambo langu. Hapa nitajitahid nisiwe na papara naanza kuwekeza kidogo kidogo maana nitakua nishapewa elimu niwekeze sh ngapi ili nipate hio laki kwa mwezi.
5. Ikiwa inaenda vizuri naongeza zaid uwekezaji ili nipate zaidi kutimiza malengo yangu ya kuingiza hio laki kwa mwezi.
ASANTE, NAOMBA KUWASILISHA🙏
 
Sitarajii kuunganisha kwa Uzi huu.
Nimeona mdau akiuliza namna ya kuingiza pesa kupitia mtandao. Naomba nikujibu na njia kadhaa lakini ukae ukijua kupata japo $1 kwenye mtandao sio rahisi hata kidogo Yani Kama ndio njia unayotarajia upate pesa yakula baada ya kuanza lazima ulale njaa. Kwanza itakuchukua muda mrefu kuanza na kuielewa vizuri pia unaweza kuanza na kukata tamaa baada ya kutoambulia kitu kwa muda mrefu. Uvumilivu na consistent nimuhimu Sana.
1. Affiliate marketing , hapa utapromote huduma ya kampuni fulani halafu wao watakulipa mrabaha. Yapo makampuni mengi yenye hiyo huduma nje na ndani ya Tanzania. Jiulize unaweza kupromote bidhaa za Aina gani mtandaoni au huduma. Commission kwa kampuni nyingi Ni kuanzia 5%-40%

2. Content creator
a) YouTuber fungua channel ya YouTube post content upate subscribe na saa 4000. ukidhi hivyo vigezo utaomba kujiunga na matangazo ya AdSense , baada ya hapo utatakiwa kuweka contents za kutosha za kuwavutia watazamaji ili upate hela. (Tafuta taarifa zaidi Google)
B) blogging , chapisha content Kama Google wanavyotaka ukishapata visitors wakutosha utajiunga na makampuni mbalimbali ya matangazo , au matangazo binafsi

c) Twitter , tafuta follower wakutosha twiter (X) verify account yako , jiunge na programs Yao ya matangazo wataanza kukulipa.

D) Facebook page

3. Kuwa freelancer , katika mitandao ya upwork freelancer n.k huku unajisajili then unatafuta kazi unayoiweza kulingana na zilizopostiwa. Mfano graphics design , article writing, translation. N.k

4. Direct link Promotion
Hapa unajiunga na kampuni za matangazo direct watakupa link yenye matangazo kazi yako Ni kuishare au kutafuta traffic kwaajili ya hayo matangazo kwa njia yoyote unayoijua wewe

Kampuni hizo Ni
1 . Adsterra
2. Monetag
Click kampuni husika kusoma zaidi. Kwa wale wenye follower wengi Twitter au x hii itakuwa rahisi kwao
5. Kuwa na idia ya App
6. Kuna online survey
7. Kindle publishing : hii Kama wewe Ni maandishi unaweza kuandika mswada mzuri then unauaplod kwenye kampuni ya Amazon then watauuza utapokea pesa. Kwa waandishi ambao hawana Majina ningumu kuuza japo copy moja.

Hizo Ni baadhi na maelezo sijaweka ya kutosha lakini utatakiwa kujifunza zaidi na zaidi. Hizi njia Ni rahisi kwa MTU ambaye tayari ana watu wakutosha kwenye mitandao ya kijamii, Kama hauna ningumu Sana na unaweza kuachia njiani Muhimu nikupambana . Pia nimuhimu kusoma Sheria za nchi yako zinasemaje katika njia husika
 
 
Back
Top Bottom