Naomba Ushauri: Nifanye nini niweze kuingiza Pesa kwa kutumia huduma za Intaneti? Isiwe Betting au Forex

Naomba Ushauri: Nifanye nini niweze kuingiza Pesa kwa kutumia huduma za Intaneti? Isiwe Betting au Forex

Mbna kwa sasa mambo ni mengi tu.
1. Nunua router tafta unlimited bundle unga wana kitaa
2. Unaweza kuanzisha online tv
3. Kuwa comedian post tik tok
4. Tumia internet kuchambua timu beti
5. Jiunge forex
6. Tumia internet kuongeza elimu yako kitaaluma
7.share ads upate kulipwa
8. Tafuta hela upate hela
Hk
 
Kwenye industry ya forex sio lazima utrade huku Kuna fursa nyingi nje ya kutrade na ukapiga pesa Safi
1. Unaweza kuwa agent wa malipo ya pesa , Hawa ni watu wanaowasaidia traders katika kudeposit na kuwithdraw, , baadh ya nchi ni ngumu sana kudeposit na kuwithdraw kupitia bank , Sasa brokers wameruhusu watu binafsi kupokea pesa kutoka Kwa traders na kufund kwenye account zao , hivyo hvyo wakati wa kuwithdraw .
Hapa unatakiwa kuwa mwaminifu tu , brokers wanakulipa commission Kwa kila amount utakayodeposit na kuwithdraw , na watu wanaish Kwa hii kazi .
2.Washawishi watu watumie broker
Umewahi kusikia Kuna kampun ukiwapelekea wateja wanakulipa kama yule mteja atafanya manunuzi kwao?? Sasa hiyo pia ipo Kwa brokers wote wa forex , ukimshawish mtu amtumie broker fulan wewe unalipwa Kwa kila trade atayoingia yule uliyempeleka , na sio mara moja ni siku zote anapotrade bas wewe Kuna commission unapokea direct , broker ndo wanakulipa , Yan unaamka asubuh unakuta kibunda kipo kwenye account yako mfano $12, $30, kutegemea na idadi uliyowashawishi na trades walizofanya

Deriv ndo broker ambaye Kwa Sasa Yuko popular sana hapa Africa ukiweza kuwashirikisha watu wamtumie broker huyu bas unaweza ukaendesha maisha yako bila stress ,
Sasa Kuna form unajaza Kisha unawatumia , wao watapitia taarifa zako Kisha watakupa go ahead na mfumo mzima wa kupokea pesa zako .
Form ipo kwenye link ukifungua bonyeza join now jaza taarifa zako Kisha submit halafu kaa Kwa kutulia
 
Mtandaoni kuna pesa nyingi sana muhimu kuyajua machimbo tu.

Kuna site za survery nyingi unazoweza kufanya na ukaingiza pesa kwa kiasi kikubwa.Ila site zinazolipa kwa kiasi kikubwa lazima uchange location ya kifaa chako isome USA kwa kutumia proxy

Ukiwa serious kuajiriwa utaona usumbufu wewe kutulia na device zako pc na simu unapiga kazi ndani mwako.

Ngoja nikupe site moja ya uhakika ukiwa na mda wa kufanya task humo kwa mwezi hukosi zaidi ya laki 3 na kuendelea inaitwa uTest

Zipo nyingi anza na hiyo kwanza
Taarifa zaidi mkuu kuhusu utest , vituvinavyohitajika na task zake ni zipi?
 
Wakuu.

Natamani kuingiza hela kwa upande wa internet naombeni msaada kwa wabobevu hata elfu 5 kwa siku

Toa Forex, betting
Zipo njia nyingi unazoweza kutumia ili kutengeneza kipato kupitia mtandao na baadhi ya njia hizo ni kuuza ujuzi na maarifa uliyo nayo mtandaoni

Unauzaje ujuzi wako ? Unatakiwa kwanza ujue jinsi ya kujiposition kwenye soko kupitia social media marketing

Kile kitu unachokijua ni biashara tosha ya kukuingizia pesa mtandaoni mfano inaweza kuwa wewe ni mtaalam kilimo au doctor wa mifugo

Ujuzi huo ni biashara tosha unachotakiwa kufanya ni kusimamia kipengele cha matokeo yanayopatokana baada ya walengwa wako kutumia huduma yako

Inaweza kuwa kuna mfugaji anachangamoto ya kuku wake kufa sana hivyo wewe ukawa unauza suluhisho la namna ya kudumisha Afya ya kuku na kuzuia tatizo la kuku kufa

Utaanzaje ?

1.Kwanza ni kujua soko gani unalenga (Je ni wafugaji wa kuku,je ni wafugaji wa mbwa,je ni wakulima wa mahindi ? Je ni wafanya biashara wanao safiri nje hawajui lugha ? N.k)

2.Mahitaji ya soko lako ni nini zaidi (Watu wanao sumbuka na changamoto ambayo wewe una suluhisho lake wanataka matokeo gani?)

3.Kupeleka suluhisho sokoni

Hapo sasa sulisho utakalo peleka inaweza kuwa kupitia huduma ya mafunzo kwa walengwa au kuwauzia vitendea kazi vyenye kuleta matokeo fulani ambayo hayapatikani kutokana na vitendea kazi vibovu au ukosefu wa elimu

Kipengele hiki kinahusisha marketing (kuuza huduma au bidhaa kwa walengwa wako ili uweze kuipata pesa yao)

Ntaandaa uzi maalum kwaajili ya hili jambo ambapo ntaelezea kwa undani kuhusu mbinu za kutengeneza kipato kupitia internet

Binafsi internet ndiyo inanisaidia kuendesha maisha yangu ikikosekana basi sina maisha
 
Kwa kuwa unapenda social media nitakupa mfano wa watu wanaotengeneza pesa kwenye social media bila kuuza bidhaa, hapa nitaongelea Instagram
1) Millard ayo anachaji 2.4M kurusha video ya tangazo 30 seconds(ana over 10M followers)
2) zamaradi anachaji 5M kukutangazia kwa mwezi. Anaweza kuwa anaingiza over 20m maana ana makampuni mengi. (7m followers).
Utasema hawa ni watu maarufu ndio maana wameweza, no
3)Bongo trending, hakuna mtu anamjua, ni anonymous guy, ana followers 1m, lakini hata kabla hajafikisha hao, alikuwa anachaji 50,000 kutangaza kwa wiki. Na ana matangazo ambayo kuingiza 1m kwa wiki siyo issue.
My point is, unaweza kukuza account ukawa unatangazia watu, sasa mbinu za kukuza account na kuwafanya watu watangaze na wewe ni somo lingine. Unaweza kujifanya kungwi kama kale kadada ukashangaa followers wanamiminika na watu wanakuletea matangazo.
Naamini kuna kitu umepata
 
Mkuu,Pamoja na kwamba UZI tayri umevamiwa ila nitaweka hapa namna bora ya Kuingiza Pesa Mtandaoni Hata hivyo ni lazima ujiulize unataka uingize Pesa kwa nmana gani maana Ili mtu akupe Pesa ni lazima umpe bidhaa au huduma yenye thamni ya Pesa unayotaka akupe.Sasa unapotaka kuingiza Pesa ni lazima Ujiulize Maswali yafuatayo:

  1. Je una bidhaa gani au huduma gani ambayo unaweza kuuza mtandaoni?
  2. Je bidhaa au huduma yako utamuuzia nani?
  3. Je unayetaka kumuuzia bidhaa au huduma ako anapatikana mtandaoni?
  4. Je bidhaa au huduma unaouza inauzwa na watu wengine au ni ya kipekee?
  5. Kama ni ya kipekee basi Jiulize Utaitangazaje ili watu waipate?
  6. Kama kuna watu wengine wanauza huduma au bidhaa kama hiyo wanauzaje?
Baada ya kujibu maswali haya unaweza sasa fuata utaratibu ufuatao ili kuuza bidhaa/huduma yako mtandaoni:
  1. Chagua majukwa ya mtandao ambayo utataka kutumia kuuza huduma/bidhaa yako mtandaoni
  2. Chagua mbinu ambao utatumia ili kufikia walengwa wa bidhaa au huduma yako
  3. Hakikisha unakuwepo Mtandaoni wakati wote na uwe na mawasiliano ya wakti wote kwa ajili ya kuhakisha kwamba hupotezi Fursa ya kufanya Mauzo
Iwapo labda hujajua ni aina gani ya Bidhaa uuze mtandaoni basi unaweza kuuza bidha/huduma ambazo zinauzwa na watu wengine kwa kupitia mfumo wa Dropshipping au affiliate marketing.Hapa ina maana kazi yako inakuwa ni kupata commision kwa njia a mtandao kupitia wateja ambao utawaunganisha na bidhaa au huduma fulani.

Pia unaweza kuamua kujifunza na kujiingiza katika uuzaji wa mifumo na huduma mbalimbali za mtanaoni kama vile hudua za mifumo ya usimamizi wa biashara,huduma za tovuti na email,huduma za mafunzo kwa njia ya tehama,huduma za uandihsi an ufasirimhuduma za utengenezaji wa maudhui mbalimbali kwa njia a mtandao na huduma ya kutaanga biashara za wenigne mitandaoni.

Kumbuka kwamba Inteneti imefungua FURSA nyingi sana ambazo kama ukifahamu kuzitumia unaweza kutengenza kipato kizuri tu cha kuweza kumudu gharama za maisha na maendeleo Binafsi.Cha muhimu ni uwe mbunifu upende kujifunza na Ujiamini.

NInakutakia kila heri
 
Mkuu hapa hakuna mtanzania mwenye akili timamu atakayekujibu,mitanzania mingi ni mibwatukaji tu lakini hakuna inachoelewa!
Akajifunze kwa wakina milardayo mitandaoni humu ni polojo tu kuigiza maisha

Asilimia 75% ya watu wanaoshinda mitandaoni ni jobless ukitaka kufanikiwa kwa Jambo lolote lazima uwe field eneo la tukio

Otherwise mitandaoni utaishia kulizwa tu wabongo Wana roho mbaya Sana .
 
Back
Top Bottom