Naombeni ushauri: Nataka kumzuia mama yangu asiolewe tena baada ya baba kufariki

Naombeni ushauri: Nataka kumzuia mama yangu asiolewe tena baada ya baba kufariki

Hautakuwa sahihi kuingilia hiyo hali mkuu,vipi kama mama angefariki yeye na mzee akaleta mama mwingine hapo ndani,nayo ungefanyaje...?
Kwa mila zetu za kiafrika, hairuhusiwi mama kuleta mwanaume aolewe naye ndani ya nyumba kama hiyo, anapaswa kuondoka kwenda kuanza maisha mengine na mwanaume huyo kama ataamua kuolewa naye. na ninaamini hii ilikuwa kuepusha vurugu za baade hasa mirathi, kwa mfano mama katangulia mbele ya haki, huyo baba mpya atakua na haki gani?!?
 
Fikra zangu ni sawa na zako.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
Huo ni umri mdogo katika kundi la wazee. Mwenyezi MUNGU akikujaalia kufikia umri huo utajua kuwa sex na faraja ya jinsia nyingine bado ni hitaji la msingi kwa mwanadamu, na hapo ndio utajua kuwa ulikuwa unamfanyia ukatili mama yako. Mwache mama aolewe, hilo ni hitaji muhimu kwa mwanadamu. Kikubwa wekeni terms and conditions za kumsapoti baada ya kuolewa, maana malezi na kila kitu kinapaswa kubebwa na huyo mume mpya.
 
hayo ni mawazo ya kimasikini

halafu hii story hata haijabalance,huo mzee naye tungesoma uzi wake ndio tungejua kama huyu bwana anayeona wivu mama yake kuolewa yuko sahihi au la ila nina hakika huyu mzee siyo hohehahe kiasi cha kuja hapo kusaka ganda la ndizi
Sawa niache na mawazo yangu ya kimasikini, ila ndio hivyo, sitaki akae kwenye nyumba aliyofia mzee. Kwangu No!

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Habari ndugu zangu. Naombeni ushauri wenu juu ya mada tajwa.

Mzee wetu amefariki miezi 8 iliyopita baada ya maisha yake yote kuwa katika ndoa na mama yetu. Mama Sasa ana umri wa miaka 68. Kwa kipindi chote tangu sisi watoto wake tuanze kujitegemea tumekuwa tukijitahidi kuwawekea mazingira mazuri ya wazee wetu. Pamoja na kuwajengea nyum
Kuna mahitaji mengine wewe kama mtoto huwezi kukidhi kwa mama yako,ni huyo mzee ndiyo anayeweza kukidhi.na kwa taarifa yako ukimzuia kuolewa utaanza kuingia cost za matibabu za magonjwa yasiyoeleweka ya mama .By the way usikute mama anaishi mkoa wenye baridi.Sema inabidi mumuulize kama watafunga ndoa yao lini maana kuolewa ni pamoja na ndoa kuwa halali.

Huyo atakuwa ni baba yenu
 
Pole sana mkuu. Kuna watu hawaelewi hii kitu hasa wale ambao hawajapitia hali ya kufiwa na baba.

Kuna watu wana comment ili mradi wafurahishe jamii wakati wanawaumiza wengine.

Ki ukweli ni aibu na inaumiza sana kisaikolojia na kwa kweli inaondoa ile freedom ya watoto kwa mama.

Pole sana na fanya kadri uwezavyo kulizuia hilo
 
Mkubalieni kuolewa lakini mwambie ahame hapo akakae na huyo Mzee kwake. Msipoangalia huyo Mzee atabadilisha hata hati za viwanja na nyumba,Mashamba yenu yayakuwa yake
 
Hilo huliwezi kama wewe ni muislamu. Mtume anasemaje katika hilo?...jibu liko hapo.

Kama ni Mkristo, mwambie point blank kuwa kuolewa baada ya baba kufa ni umalaya! Haimpi heshima. Mwambie waziwazi!
Usimtafutie mwenzio laana. Kama baba amekufa mama akiwa na 30 yrs ina maana asiolewe eti ni umalaya? Huo ni ukristo au wendawazimu?
 
"ACHA UJINGA"
Kikubwa Kama Mama yenu Mungu Akimpenda timueni huyo baba wa kambo Ila kwa Sasa ACHA
Unafikiri naye huyo baba wa kambo atakuwa mjinga kama wewe? Yupo kimahesabu, huenda ana watoto wake wakubwa tu nao watataka kudai mali hapo baadaye. Tumia akili, kuepusha haya yote ni mzee kumchukua bibi wakaishi nyumbani kwa huyo mzee.

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Habari ndugu zangu. Naombeni ushauri wenu juu ya mada tajwa.

Mzee wetu amefariki miezi 8 iliyopita baada ya maisha yake yote kuwa katika ndoa na mama yetu. Mama Sasa ana umri wa miaka 68. Kwa kipindi c
Jamani huyu mrembo 68 years anataka nini? Au mzee huna watoto wa kumkeep bize bibi? Nashauri mhamishie mjini aje kucheza na wajukuu. Huyo babu/ mchumba ni opportunist tuu anataka mtelemko. Ila pia bibi aambiwe ukweli akitaka kuolewa akukabidhi funguo. Tena mwambie mta-msend off kabisa ajue kwenu kaondoka
 
Pole sana mkuu. Kuna watu hawaelewi hii kitu hasa wale ambao hawajapitia hali ya kufiwa na baba.

Kuna watu wana comment ili mradi wafurahishe jamii wakati wanawaumiza wengine.

Ki ukweli ni aibu na inaumiza sana kisaikolojia na kwa kweli inaondoa ile freedom ya watoto kwa mama.

Pole sana na fanya kadri uwezavyo kulizuia hilo

hapana mkuu,mambo mengine ni wewe tu ulivyoamua kuchukulia,inaumiza nini mama kuolewa kama yeye anahisi bado anaweza?
sasa afadhali aolewe ionekane ana mume mwingine au awe anaenda huko mitaani kutafuta mwanaume yeyote!...huyo ni mtu mzima anajua anachokifanya kuingilia maamuzi yake ni kuingilia haki zake za msingi

kikubwa ni kukaa chini kujadiliana mfumo wa maisha utakuaje baada ya hapo...kumkataza ni kujitafutia laana
 
Bibi yangu kaolewa akiwa na miaka 50 na kitu na mzee mwenzie.
Bibi alipofariki mama zangu wadogo na wajomba wakamwambia ukweli Yule baba yao.
Mama kaondoka na wewe Safari yako imeishia hapa.
Kwa kuwa nyumba kaikuta imeshajengwa.
Ila kwa kuwa wewe kichwani ni MATOPE huyo baba anaweza kukudhulumu
Unafikiri naye huyo baba wa kambo atakuwa mjinga kama wewe? Yupo kimahesabu, huenda ana watoto wake wakubwa tu nao watataka kudai mali hapo baadaye. Tumia akili, kuepusha haya yote ni mzee kumchukua bibi wakaishi nyumbani kwa huyo mzee.

Sent from my A50s using JamiiForums mobile app
 
Uyu maza nae 68 years anataka kuolewa.
Mwacheni aolewe ila asiguse mali ya mzee wenu na ahamie kwa uyo mumewe mupya.
Mambo ya ajabu kabisa aya
 
Back
Top Bottom